Mjadala Huru: Je ERP ni chanzo cha Umasikini wa Watanzania?

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Wengi tumekuwa tukistaajabu kwa umasikini unavyozidi kulisulubu taifa letu, unaweza kuwadhani baadhi ya Watanzania kama vile walikuwa uhamishoni kwa jinsi wanavyo lalamika kwa ugumu wa maisha, lakini hilo si wao tu bali ni kila mmoja, hata Jakaya ukimuuliza kuwa kwanini Tanzania ni masikini atakuambia SIJUI.


Mimi narejea nyuma baada ya uhuru, Tanzania ilikuwa na uchumi endelevu na wastani mzuri wa idadi ya watu, Unaweza usiamini lakini ni ukweli uliowazi kuwa enzi hizo Taifa lilitegemea Tumbaku, Pamba na Mkonge kupata pesa za kigeni, na ilimudu kwa kiwango kikubwa kuwapa wanachi wake hudumu muhimu kama hospitali na shule.

Chini ya vita ya ujinga, maradhi na umasikini, Tanzania ilianza kukua kiuchumi hasa ikiabudu na kuakisi mifumo ya uchumi wa kijamaa sanjari na kuchagiza uzalendo halisi kwa wakaazi wa Tanzania bila shuruti,

Machipuko mema na ndoto imara za Mtakatifu Julius K. Nyerere zilianza kuzaa matunda hasa baada ya Tanzania kuzaliwa na kuitwa nchi ya viwanda vidogovidogo vyenye kuwalisha watanzania uhalisia wao.

Lakini ndoto na machipuko hayo yalikabiliana na upinzani wa mabeberu wa ndani waliofanikiwa kupenyeza sera zao na zikafanikiwa kuingia nakuliangusha rasmi taifa na ndoto huru za mtakatifu J.k. Nyerere zikatutoka na leo hatujui kwanini sisi ni masikini.

Miaka ya 1980+ paliibuka sera iliyoitwa Economy Recovering Program (ERP), mpango huo ulipendekeza viwanda “ambavyo wao waliviita havina tija” vifungwe. Hakika hili lilipelekea idadi kubwa ya viwanda vyetu kufungwa na hata vile vilivyobaki serikali ilivitelekeza kasha wakaibua dili lingine walilolipa jina la uwekezaji lakini mimi nasema WIZI.
Mimi najaribu kutafakari huku nikistaajabu ya Musa, hawa waliokuja nasera hii ya ERP ndio leo wanaojiita wawekezaji kwa mwamvuli wa nje.

Jambo lakushangaza kama taifa, bado hatujajua wapi tulikosea ili tujisahihishe.

Wadau naomba tusaidiane kujibu huenda jibu langu ni tofauti na lako, Kwanini watanzania ni masikini? Tumlaumu nani?
 
Duuuuh, lakini unaonekana unahoja ya msingi moyoni, hebu fafanua mkuu
Nyerere alianzisha sera na mambo mengi na ambayo yalikuwa mazuri, tatizo ni kuwa hakubuni mbinu wala systeam hata kama yeye hayu wasaidizi wake wayaendeshe, yani bila yeye hakuna kitachotendeka.
 
Nyerere alianzisha sera na mambo mengi na ambayo yalikuwa mazuri, tatizo ni kuwa hakubuni mbinu wala systeam hata kama yeye hayu wasaidizi wake wayaendeshe, yani bila yeye hakuna kitachotendeka.
Bado nahitaji ujipambanue zaidi, nasita kuamini kuwa ndio chanzo cha umasikini wetu.

Tafadhari mkuu naomba nilala kesho nitaamka na maada hii tujadili zaidi
 
Sawa bwana, huo ndioukweli wa umasikini wetu
Mkuu naona unajisahau na huenda wewe ni miongoni mwa wanaofaidika na matunda ya ufisadi Kama Ritz Zomba Chama na Pro-ccm wengine humu jamvini. Rais ambaye JK anaweza kujipima naye ni Ali Hassan Mwinyi labda na Mkapa kidogo. Rais wa kwanza Mwl. Nyerere pamoja na kutokuwepo rasilimali nyingi wakati huo alijenga kiwanda karibia kila mkoa. Alijenga nyumba za serikali ambazo wezi Mkapa na Magufuli wamekuja kuuza, alijenga bandari Dar, Tanga, Mtwara, Mwanza, ALIONGOZA SERIKALI YENYE NIDHAMU AMBAYO RUSHWA ILIKUWA NI MWIKO. Alileta umoja wa kitaifa kwa kuongoza serikali bila kujali dini wala. Wakati wake elimu ilikuwa inatolewa bure tena kwa ubora wa hali ya juu. Wakati wake shule zilikuwa na vifaa na waalimu. Wakati wa Kikwete elimu katika shule za msingi na sekondari imekuwa na mzaha tu.
 
Ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Tumefeli kwenye siasa na uongozi.
 
Mkuu naona unajisahau na huenda wewe ni miongoni mwa wanaofaidika na matunda ya ufisadi Kama Ritz Zomba Chama na Pro-ccm wengine humu jamvini. Rais ambaye JK anaweza kujipima naye ni Ali Hassan Mwinyi labda na Mkapa kidogo. Rais wa kwanza Mwl. Nyerere pamoja na kutokuwepo rasilimali nyingi wakati huo alijenga kiwanda karibia kila mkoa. Alijenga nyumba za serikali ambazo wezi Mkapa na Magufuli wamekuja kuuza, alijenga bandari Dar, Tanga, Mtwara, Mwanza, ALIONGOZA SERIKALI YENYE NIDHAMU AMBAYO RUSHWA ILIKUWA NI MWIKO. Alileta umoja wa kitaifa kwa kuongoza serikali bila kujali dini wala. Wakati wake elimu ilikuwa inatolewa bure tena kwa ubora wa hali ya juu. Wakati wake shule zilikuwa na vifaa na waalimu. Wakati wa Kikwete elimu katika shule za msingi na sekondari imekuwa na mzaha tu.

Asante mkuu kwa kuturejeshea kumbukumbu hii inayosisimua na kutia hasira sana, napata hasira hasa nikikumbuka hawa mumiani walivyoua viwanda vyetu kwa mbeleko ya ERP
 
Back
Top Bottom