Mjadala: Gharama na njia nafuu za kujenga nyumba ya kuishi Tanzania

Tumia interlocking bricks mkuu, na kupaua tumia style ya hiden rooftop, dirisha zako za aluminium na milango ya mchina, tires siku hizi bei kitonga pamoja na gypsum.....itawezekana tu, lakini punguza ukubwa wa nyumba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesahau sebule ambalo mara nyingi ni kubwa sana, chumba cha wazazi ambacho nacho ni kikubwa na kina kuwa self-container, chumba cha kulia chakula,vyoo , bafu, jiko, stoo, korido, sehemu inayochukuliwa na kuta, gereji n.k.! Nyumba ya vyumba vitano VYA KULALA kwa matashi ya kitanzania haitapungua mita za mraba 200!

Ukizidisha hiyo na hizo namba zinazotajwa utajikuta uko kwenye milioni 500! Dawa ni kuwa realistic kitu ambacho kinatushinda wengi. Mfano ni kuita nyumba yenye vyumba vya kulala vitano kuwa ya kawaida! Itakuwa ya kawaida tu kama utaijenga mithali ya nyumba zetu za kiasili za kiswahili. Vyumba bila kutofautisha, korido katikati, ua na jiko, bafu na choo nje!

Amandla.......
chumba cha wazazi wakienda wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mada imepamba moto; naombeni kujua, hivi kwa hapa Tanzania nikitaka prefabricated houses zinapatiakana? Kwa yeyote mwenye kufahamu naomba anisaidie kujua katika hilo kwa undani
 
Kwa mahitaji ya Mbao kwa Bei nafuu tuwasiliane 0674344436View attachment 1026672

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, nina kiwanja cha square kilometer 400, nimeshazungusha ukuta upande mmoja bado pande tatu ni kama tofali elfu 2 kasoro hivi za nchi 5 na 6 jumla.
Nipeni gharama zake au fundi mzuri aende aone site then tuongee bei.
Contacts 0716282670.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nasikia hata gereji watu hawataki tena kuiweka pamoja na nyumba. Wanapenda iwe pembeni. Vipi wakuu hili mnalionaje? Kuna sababu za kiufundi, kiusalama au ni maamuzi ya watu tu?
Nahisi hii ya kuweka garage kwa nyumba ni zile plans tunazo copy and paste kutoka Ulaya
Inawezekana wao huweka hivyo kutokana na hali ya hewa(wakati wa barafu) au kuna wezi werevu sana wa magari kuliko huku kwetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sijasoma post zote zilizotangulia kama narudia points samahanini ndugu zangu
Mimi nyumba ya vyumba 5, vyoo 2- kimoja self container, nimejenga kwa milioni 15 na kidogo kuanzia kiwanja, ramani, msingi, kuta (incuding baraza ya mbele na nyuma), paaa na gutters. Imesimama kwa sasa ...nimetumia mafundi hawa wa mitaani baada ya kuona kazi zao kwa macho yangu au kupata good report kutoka kwa wenye nyumba, na nikasimamia mwenyewe... personally, na hii ndio taabu yake, inabidi kusimamia kweli maana mafundi hawa wa mitaani wanaiba sana...

mfano, kuna siku fundi alipanga njama na muuza mbao ... fundi akanitajia idadi ya mbao kuliko kiasi kinachohitajika mimi nikanunua mbao za kutosha na extra kidogo just in case!, kesho yake asubuhi jirani yangu akaniambia nilipoondoka jioni yule muuza mbao alirudi jioni na gari yake akachukua sehemu ya zile mbao, nikampigia simu fundi kumuuliza aliruka na hakurudi tena kazini, sikuwa na muda wa kufuatilia saaana kwa hiyo nikabadilisha fundi na duka la vifaa...hopeful utajifunza kitu kutokana na experience yangu..kama unasimamia mwenyewe inabidi pia uwe na rough idea ya kiasi cha vifaa kinachohitajika la sivyo utatapeliwa
Yeah akikwambia mbao ni kiasi fulani lazima a justify amefikiaje kwango hicho au tiles au bati
Kuna mmoja alinifanyia estimations za gypsum aka overestimates makusudi ili zitazobaki azivushe
Bahati nzuri nilikuwa nakopa kwa jamaa yangu ana Hardware akaniuliza unajenga nyumba ya ukubwa gani nikamuelekeza akaniambia ni nyingi sana zaidi ya 1/3 ya mahitaji zichukue lakini tight ulinzi na kweli nika tight ulinzi kuna kijana mmoja nilimuweka mlinzi akaniambia fundi huwa anakuja saa 4:00 usiku anadai amesahau kitu flani hivi then akajaribu kumshirikisha jamaa kwenye issue ili wachukue zile gypsum zilizobaki. Mlinzi akamwambia jamaa kila saa anasililizia mimi mwenyewe hapa kuna watu wananilinda
Kweli ilipofika mwisho more than 1/3 ya gypsum nilizirudisha
Wana overestimates ili wavushe mzigo au wana underestimate kama anajua uko busy kazini anakupigia simu saa 5 asubuhi bwana kazi zimesimama huku tofali zimeisha anajua huwezi toka utamtumia pesa au utamtuma sehemu akachukue tofali sehemu ya kwenda chukua tofali 300 atachukua 500
Hao ndio mafundi wetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
BY then hapo kwa mchanganuo wa mdau cjaona aweke cost za water system,electricity na hata toilets (amesema just masink tena ya ukutan or yanauzwa yakiwa complete na vyoo vyake?) .kama vp atusaidie please.
Hata hapo kwenye ma Sink ameweka
Masink 30 bei 45,000= 135,000
Ukicheck sio 135,000/= bali 1,350,000/=
Halafu masink 30 hiyo imekuwa boarding School
Au alikimaanisha masink 3

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuuuu,tupe progress baada ya kuweka madirisha,miundombinu ya maji taka,safi,milango,ceiling boards n.k,huko ndio kwenye balaa,mbona kupandisha boma sio kazi,kazi finishing mkuu,hapo ndo utakapotoa macho utakapoambiwa wiring tu milioni unusu na ndipo utakapoanza kuwachukia mafundi
Kuna psychological relief unaipata ukifikia hapo. Unakuwa uko tayari hata kushindia mkate ili ufikie finishing

Sent using Jamii Forums mobile app
 
My Opinion
Hapa Tanzania kuwa na nyumba ni suala la KIJAMII zaidi. Yaani kuna heshima fulani mtu akiwa na nyumba yake. Watu wengi huifuata hiyo heshima, hata kama hana hitajio la nyumba wakati huo.
Nakupa mfano, kuna mtu amejenga mbezi ya kimara ndani ndani huko akahamia vizuri tu. Kilichotokea ni kwamba analazimika kuamka saa 10 alfajir na hurud saa 4 usiku akawa anawaona watoto wake na kufanya mambo ya kifamilia weekend tu. Kahama kaacha nyumba karudi kupanga karibu na mjini. Sawa unakaa kwako, unajua opportunity cost ya kukaa kwako? Subiri uzeeke utaenda kukaa huko fo the rest of ur life!!!
Unawajua wahindi na waarabu wa pale katikati ya mji wa Dar? Wangapi wanamiliki nyumba? Hawana uwezo wa kujenga wale? Tena wapo nchi hii tangu Nyerere alipotaifisha baadhi ya nyumba zao, kwa hiyo wanaijua vizuri Tanzania. Jitazame, kama huna hitajio la nyumba binafsi kuishi kwa wakati huu, jenga pole pole tu. Usikurupuke eti kisa upate heshima. Hata Mungu hakuumba ulimwengu siku moja, ipo siku utahamia kwako comfortably.
Lipa kodi kwa baba mwenye nyumba, jenga polepole.
MullaX
Unachokizungumza you are more than correct. Tatizo kubwa linalotufanya tukipata pesa kukimbilia kujenga ni kwamba hatuna confidence ya kukaa na pesa na tukazifanya pesa zikatutumikia badala ya kuzitumikia(ref Kiyosaki) nitakupa case studies 2

1.Kulikuwa na Dada nafanya nae kazi maeneo ya Muhimbili alikuwa akiishi Mbagala Charambe, ili kuwahi ofisini inabidi aamke saa 10 usiku, jioni akitoka saa 11:30 anafika home saa 4:30 usiku ana mtoto mchanga na ndio amemaliza ile likizo yao ya kunyonyesha hivi huyu Mwanamke anamuangalia mumewe saa ngapi ? watoto jee ?? Kutwa anasinzia kazini sikwambii poor decisions anazozifanya kwa kutopata muda wa kupumzila
Jaribu kuangalia gharama na adhabu anayoipata for the sake of Personal Status kwamba na yeye amejenga nyumba

2. Kuna kijana mwingine anaitwa Hassan huyu sio Mwarabu wala Muhindi yeye Mluguru. Anafanya biashara ya jumla ya mitumba ananunua kwa dealers wa Kihindi ambao akinunua mzigo wa 30m wanamkopesha mwingine wa 30m kutokana na uaminifu alioonyesha
Haya haya mambo ya Social Status akafanya matusi yake akajenga kitu kinafika 110m Mbezi. Baada ya muda wale wahindi wakaanza kumshangaa spidi ya kuchukua mzigo imekata wakamtahadharisha na unajua mtu ambaye alikuwa ananunua mzigo wa 30m anakuja nunua mzigo wa 7m hata kama ulikuwa unamkopesha unaanza kuogopa. Jamaa akakaa chini akatafakarii akaona biashara anayofanya ni kama ya miaka 5 iliyopita. Akagundua kuwa ujenzi umekata mtaji yaani umemrudisha nyuma kibiashara miaka 5.
Akapiga moyo konde na ashukuru Mungu alishtuka mapema akaiuza ile nyumba iliyogharimu 110m kwa 70m akaenda kupanga Magomeni upande mmoja wa nyumba. Nawapa history ya mtu ninaemjua na hayo yamemtokea kama miaka 2 au 3 iliyopita hivi sasa ukiacha ile biashara ya mwanzo ana maduka mengine mawili kariakoo na huwezi kuamini ile pesa aliyokuwa anatumia mbezi kwa petrol kutokana na distance inazidi kodi ya nyumba ya Magomeni

Kitu ambacho jamaa kimemsaidia sio mshamba wa hela anajua kuizungusha na pesa haimuendeshi yeye ndio anaiendesha




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabongo hawatakuelewa ila kwa uchunguzi Mdogo ni kwaba wanawake hushawishi waume wao kujenga baada ya umbea kwenye makutano yao vicoba au bombani na sentensi "NINA KWANGU" imekuwa kama siasa za UKUTA na vunja ukuta bila kuangalia mbele.
Jamaa wawili walifanya kazi ofisi moja. Mmoja akaanza kujenga na wa pili akaanza biashara ya kilimo chenye miundombinu ya umwagiliaji kiasi kwamba habahatishi. Ile kazi mradi ulifika mwisho wrote wakarudi kijiweni. Aliyejenga alianza kutafuta kazi huku mkulima akinyanyua nyumba bila wasiwasi na bila shaka ya chanzo cha kipato. NI VIGUMU SANA KUANZISHA BIASHARA IKAKOMAA ILA NI RAHISI KUJENGA. Amua unaanza na kipi.
"Tengeneza shamba lako kabla ya nyumba yako" Wafalme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom