Mizengwe ya Kupindishwa

Geeque

JF-Expert Member
Aug 17, 2007
936
316
Nchi yetu ni ya Wadanganyika ambao wanakubali kila kitu kutoka kwa viongozi MAFISADI. Hakuna tumaini lolote nchini Tanzania kwa sasa litakaloletwa na CCM au wanachama wake, tusitegemee chochote kipya kutoka kwa MAFISADI na washirika wao ambao wanapindisha mizengwe na uongo wa kila aina kuwahadaa Watanzania. Nadhani siri pekee wanayoijua ni kuwa watanzania ni waoga, wajinga na ni watu wa kuitikia ndio kila kitu ambacho MAFISADI watakachosema. Hakuna tumaini lolote na kilichobaki hivi sasa ni mabadiliko makubwa katika uongozi pale nchini. Dr. Slaa ndio mtu anaetufaa kutuongoza mwaka 2010, jamani wakati ndio huu na hakuna ngoja ngoja, tumuombe sana Dr. Slaa agombee hii nafasi. Ningeomba Invisible uifungulie ile topic yangu ya Dr. Slaa for President ili tuendelee kuichangia. Hakuna Tumaini kutoka CCM. Hakuna tumaini lolote pale ambapo Mizengwe Inapindishwa Mchana Kweupe ili kuwahadaa wananchi. Tusitegemee MAFISADI kuchukuliwa hatua zozote kwenye suala la EPA, Richmond, BOT,Kiwira, TTCL na uchafu mwingine wowote.

Wakati mwingine demokrasia haiji kwa amani, haiji kwa kujaribu kutumia vyombo sahihi vya umma, haiji kwa kufuata utaratibu unaotakiwa, haiji kwa kutegemea CCM watabadilika, haiji kwa kukaa kusubiri mwingine afanye mabadiliko. Sasa ni muda muafaka wa kuanza kutumia njia mbadala ambazo zinaweza kuwa si za kidemokrasia lakini dhumuni lake kubwa ni kuleta demokrasia nchini kwetu.
 
Dr Slaa? Rais? Huyu ni padre mstaafu ambaye anatumia philosophy na canon law aliofundishwa seminari kuhadaa umma. Poleni sana hamumjui huyu mtu. Ana kipaji cha ulaghai na ujanja ujanja. Itafitini historia yake ya zamani. Hafai hafai hafai
 
Dr Slaa? Rais? Huyu ni padre mstaafu ambaye anatumia philosophy na canon law aliofundishwa seminari kuhadaa umma. Poleni sana hamumjui huyu mtu. Ana kipaji cha ulaghai na ujanja ujanja. Itafitini historia yake ya zamani. Hafai hafai hafai

Dr. Wilbroad Slaa ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake ambaye anapigana kila siku katika kuhakikisha haki inatendeka nyumbani Tanzania. Upadre wake hauna madhara yeyote kabisa kwa yeye kupigania haki kwa watanzania wote, ni mtu ambaye amefumbua macho watanzania wengi kuhusiana na ushenzi na unyama unaofanywa na serikali ya Chama Cha Mafisadi (CCM). Nadhani haumtendei haki kabisa Dr. Slaa kwa kashfa zako ambazo hazina kichwa wala miguu, kujitolea kwake kutetea watanzania dhidi ya MAFISADI ni kwa manufaa ya wote. Mungu Akubariki Sana Dr Slaa na Uendelee na Moyo Huo Huo.
 
Safu ya kina slaa haifai kuwepo katika kiwango cha Uraisi ,kuna watu ambao ni wastahiwa katika International level na walioko nje wanatushangaa tunapowapiga na chini watu hawa ,hata hao akina Slaa wanawajua ni akina nani ,na kama Slaa atawekwa kiti moto basi anaweza moja kwa moja kukubali juu ya kuwepo kwa watu hao na yeye akawaunga mkono.
Watu kama akina Slaa na Zitto si vizuri kabisa kuelekea katika nafasi za Uraisi ,hawa ni watu wa kubakia kwenye level ambazo zitawafanya kama kuwa walinzi na waratibu wa nyendo za walioko madarakani yaani liwepo kama baraza la Wazee ambalo litaweza kumjadili yeyote bila ya kumuonea na kumdhibiti mtu yeyote anaekengeuka maadili katika nafasi za uongozi bila ya kuwepo na chuki au majungu.
kwa mfano hizi pilika pilika za ufisadi kama Baraza hili lingekuwepo basi hawa mafisadi wasingelifika mbali ,wangeitwa wakahojiwa kwa kina na kila ushahidi uliopatikana ungelipelekwa kwenye baraza na mhusika kuitwa kujitetea kwa mapana na marefu na badala yake Baraza la wazee hili haina maana watakaoliunda wote watakuwa wazee ,la hasha ila watakuwa watu wenye uchungu na nchi hii ambao wapo mstari wa mbele katika kulitetea kwa kila hali ,wako wabunge machacha ambao kwa mtazamo wa bunge letu la leo Wazee watakao unda Baraza hilo wamo toka sehemu zopte mbili za upinzani na CCM.
Hivyo hawa akina Slaa na wenzao wangeliunda baraza hili ambalo lingekuwa na mamlaka maalumu dhidi ya viongozi wa Serikali na vyombo vyake vyote.
Pale tu zinapozuka shutuma dhidi ya viongozi wa Serikali basi kwa nguvu ilizonazo itamwita Kiongozi na kumhoji bila ya kuwa na pazia kwa Wananchi kama itatumika Televisheni kurusha mahojiano hayo kwa Nchi nzima ili kila mmoja wetu asikie kinachohojiwa na kinachojibiwa.
Haya ni maendeleo ambayo tunayahitaji katika Tanzania ya leo ,ambayo inaonekana kila mmoja ana lake ,kila mmoja anataka kumkomoa mwenzake ,kila mmoja anampikia jungu mwenzake ,kumaliza matatizo haya ambayo yanaelekeza nchi yetu pabaya naona kuna umuhimu wa kuunda Baraza hili litakalojulikana kama la Wazee ili kuinusuru Nchi na majungu ya wenyewe kwa wenyewe ambayo hayamsaidii kitu Mwananchi wa kawaida zaidi ya dhiki na shida.
Naomba kuwasilisha hoja.
 
Back
Top Bottom