scatter
JF-Expert Member
- Feb 15, 2013
- 1,667
- 925
Waziri Mkuu amedai bungeni muda huu kwamba mshahara wake hauzidi Tsh. 6mil na akadai wanaodai analipwa zaidi ya hapo ni uzushi mkubwa kiasi kwamba yeye ni mkopaji tu katika mabenki na kuwa mshahara huo ni pamoja na mapato ya mkewe.
Source: leo bungeni -tbc
Source: leo bungeni -tbc
Akijibu maswali ya papo kwa papo, Mh. Waziri Mkuu amesema anapata take home ya shng. milioni 6 za tz.. Anasema mshahara wake na wa Mh. Rais na makamu wake, hauna tofauti kubwa, haizidi tshng. Mil. 1.. Amemjibu Zito kwamba kwa kutaja uongo kiasi cha mshahara wake, Mungu atamhukumu.
Kaongezea kwamba yeye ni kati ya viongozi wanaokopa sana mabenki, pale maisha yanapomzidia. Na juzi juzi amechukua mkopo CRDB na NMB..