Mizengo Pinda: Chonde chonde Watanzania dumisheni amani

MAKOLE

JF-Expert Member
Feb 5, 2012
618
280
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewataka Watanzania na waumini wa dini zote nchini humo kudumisha amani na utulivu. Mizengo Pinda amesisitiza kuwa, Watanzania wanapaswa kukataa suala la kuiingiza nchi katika vurugu na kukataa vishawishi vitakavyosababisha uvunjifu wa amani.

Waziri Mkuu wa Tanzania amewaomba viongozi wa dini mbalimbali nchini humo kufanya juhudi za kuwafundisha waumini wao elimu inayozingatia misingi ya imani za dini zao na kukemea tabia ya wanasiasa kufanya siasa bila kutilia maanani suala la amani.

Mizengo Pinda amebainisha kwamba, Watanzania wana mchango mkubwa katika kuhakikisha nchi haiingii kwenye vurugu kwa kutokubali na kutoshawishika na vishawishi vitakavyovuruga amani ya nchi.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelaani vikali vitendo vya kinyama vya kuchinjwa maalbino kwa imani na kishirikina na kusisitiza kwamba, watu wanaofanya vitendo vya kinyama kama hivyo hawana imani na Mwenyezi Mungu na ndio maana wanajitumbuikiza katika vitendo hivyo vinavyokinzana na ubinadamu.



CHANZO: Mizengo Pinda awataka Watanzania kudumisha amani

MY TAKE: Hivi kwa kashfa ya ESCROW haoni kwamba naye ni mmoja wa wanaochochea/ wanaoweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini?
 
huwezi sema watanzania wanamchango mkubwa kwakuwa hii nchi ni yao hapa kimantiki anamaanisha nchi ni ya kundi flani na watanzania ni kundi jingine . watanzania wana wajibu mkubwa-------
 
Nikimsikiaga tu anaongea ktk TV nahamisha mara moja channel...au nazima kabisa...Nasty...ptuuuuh..!!!!

Nikiona gazeti limeandika habari zake, nakwepesha macho...!!!
 
Wajawazito_Temeke_Hospital.jpg

View attachment 209730
 
Hawa viongozi wetu wananifurahishaga hapo tu watafanya mauzauza weee mwisho wa siku wakiona maji ya shingo wanakimbilia kujifuniaka na mwavuli wa amani na sisi mimacho kodoo masikio mwaaa sijui nani katuloga .
 
Wanahubiri amani huku wamekula pesa za wananchi.

Dawa Hospitalini hakuna, watu wanakufa kuliko nchi yenye vita

Watu wanafanya kazi, wanakatwa PAYE

PAYE ya Tanzania ni kubwa kuliko nchi zote Africa Mashariki.

Yule Mwenyekiti wa CHama cha Waajiri ATE alisema mafisadi wa ESCROW wachukuliwe Hatua.

Kodi za Watanzania million 45 ziende kwa Familia 10 tu (Mafisadi wa ESCROW)!!!!

Kumbuka kila utakacho nunua umekatwa VAT ya 18% (tia akili) ewe Mtanzania

Watanzania wengi sana wanakufa kwa kukosa dawa na huduma bora Hospitali.... Akina mama wanalala chini wakati wa kujifungua. Kuna amani gani wakati watu wanakufa kuliko nchi za Vita kama DRC na Somalia!!!

Wananchi wakidai haki wanaitwa majina ya uchochezi, magaidi n.k

Elimu imedorora kwa DIV 00 aka Div 5, ajira kwa vijana hakuna...

Wanaingiza sukari nchini kuua viwanda vya ndani kwa minajili ya 10% kujaza tumbo zao--- WAPIGWE tuuuu


Kisa tu kutafuta pesa za kununua kanga na Tshirt za Kijana zilizo (nenewa) maneno ya kuiabudu Csiem.... Ili watanzania masikini wadanganywe nazo
 
Wanahubiri amani huku wamekula pesa za wananchi.

Dawa Hospitalini hakuna, watu wanakufa kuliko nchi yenye vita

Watu wanafanya kazi, wanakatwa PAYE

PAYE ya Tanzania ni kubwa kuliko nchi zote Africa Mashariki.

Yule Mwenyekiti wa CHama cha Waajiri ATE alisema mafisadi wa ESCROW wachukuliwe Hatua.

Kodi za Watanzania million 45 ziende kwa Familia 10 tu (Mafisadi wa ESCROW)!!!!

Kumbuka kila utakacho nunua umekatwa VAT ya 18% (tia akili) ewe Mtanzania

Watanzania wengi sana wanakufa kwa kukosa dawa na huduma bora Hospitali.... Akina mama wanalala chini wakati wa kujifungua. Kuna amani gani wakati watu wanakufa kuliko nchi za Vita kama DRC na Somalia!!!

Wananchi wakidai haki wanaitwa majina ya uchochezi, magaidi n.k

Elimu imedorora kwa DIV 00 aka Div 5, ajira kwa vijana hakuna...

Wanaingiza sukari nchini kuua viwanda vya ndani kwa minajili ya 10% kujaza tumbo zao--- WAPIGWE tuuuu


Kisa tu kutafuta pesa za kununua kanga na Tshirt za Kijana zilizo (nenewa) maneno ya kuiabudu Csiem.... Ili watanzania masikini wadanganywe nazo

Dah, umenitoa machozi!
 
Amani ni TUNDA la haki, huitaji kuihubiri ni kuipnda tu, timiza haki amani itatawala, lakini ule escrow wewe na familia yako, jirani yako anaihi chini ya dola moja? Haiwezekani.
 
Imekuwa ni kawaida kwa viongozi wetu wa kisiasa kusema wananchi tudumishe amani, wakati huo huo wao wanaendelea kuhubiri chuki katika majukwaa na kuendelea kukusanya wananchi ili wawaeleze mambo ambayo kimsingi yanahimiza chuki kati ya wananchi ili waweze kufikia malengo yao. Hivi ni nani anayevunja amani kati ya wewe unayehubiri uadui na mimi ambaye kwa sababu za njaa yangu nakubali kutekeleza mahubiri ya chuki yanayofanywa na viongozi wetu tena wajuu kabisa?
 
Unaowaita viongozi nao ni raia wa Tanzania...nadhani Watanzania ndio wana wajibu wa kulinda na kudumisha amani nchini!
 
kudumisha amani na utulivu ni desturi ya watanzania ambayo CCM na Serikali yake inapenda kuona ikivunjika, najua haya ni maneno mazito lakini huu ndio ukweli, namna ambavyo Serikali ya awamu ya nne ilivyoruhusu wizi MKUBWA kufanyika tena mchana kweupe na huu ni udhibitisho wa hayo, pamoja na wizi MKUBWA kufanyika, wahusika kujulikana watanzania walitarajia hatua kali dhidi yao, lakini wao ndio wamegeuka mashujaa. Sijui ni lini kila aliye CCM ataona hatari iliyoko mbele kwa wizi huu kuendelea, la kusikitisha wengi wao wakiutetea humu jamvini, ni aibu kwa taifa jinsi ambavyo Serikali imeonyesha ulegevu katika kusimamia rasilimali za taifa, hivyo kushindwa kuboresha maisha ya watumishi wake, angali jinsi askari polisi wanavyoishi, natamani kulia kila mara napowaangalia, nafikiri na majeshi mengine ni hivyo hivyo, hospitalini hali ni mbaya, elimu ni ya mashaka, soko la ajira bado sio imara. Kwa kweli CCM mna kazi kubwa ya kugeuza mioyo ya wenye akili kuamini vinginevyo, kwa sasa wenye akili wanajua mmeshindwa kufanya kazi mliyotumwa. Hongereni kwa kuiweka Tanzania katika ramani ya wauza madawa ya kulevya na majangili wa Tembo, hongereni sana.

Kuna siku mtaelewa haya maneno yangu.
 
na kudumisha amani ni sambamba na kuiweka ccm madarakani. ukiamua watoke madarakani wako tayari hata hiyo amani ipotee ili wabaki madarakani. huu wimbo wa amani wala hauna mashiko tena...
 
Watanzania wanafaidi amani isiyo na faida-unprofitable peace kwa lugha ya malkia elizabeti.Where are peace dividends? Mungu na mtume sijui.
 
Back
Top Bottom