Mixed Education System: Upi ni wakati sahihi wa kumsomesha mtoto katika Private School kwa mzazi wa kipato cha chini?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,316
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Eti ndugu zangu watanzania;

Upi ni wakati sahihi wa kumsomesha mtoto katika Private School kwa mzazi wa kipato cha chini? Primary Level au Secondary Level?

Tanz Facts 2.jpg


Ninapoongelea mzazi wa kipato cha chini kwenye muktadha huu nina maana kwamba ni yule ambaye anatamani mtoto wake asome katika Private School ila hawezi kumudu gharama za kuanzia darasa la kwanza mpaka form six. Yeye anaweza kumudu Level moja tu baaas.

Kama mtoto atasoma primary level katika Private School basi secondary level atasomea katika shule ya Serikali na vice versa.

Kuna jirani yangu nipo nae hapa anadai ni bora mtoto aanzie elimu ya msingi katika Private School ili apate msingi bora wa lugha ya kiingereza hata akienda secondary anaelewa masomo kwa ufasaha.

maxresdefault.jpg


Classmate wangu Beautiful Nkosazana yeye alikuwa anadai eti ni bora mtoto akaanza Primary Level katika shule ya serikali ili akienda Secoary katika Private School anakuwa tayari amekomaa vema kiakili na anaweza kujimudi.

HII IMEKAA VP NDUGU ZANGU?

WEWE UNANISHAURIJE KAKA/DADA YANGU?

OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Primary msomeshe shule za kawaida, Sekondari mpeleke Private, then A-level atajipeleka mwenyewe shule za serikali baada ya kufaulu vizuri Olevel.

Shule ya msingi asome private. Ukiangalia syllabus za primary private zinacover secondary Kwa asilimia zaidi ya 70. Mtafute alie darasa la sita mpe paper za form 2, civics,geography, English, biology uone atakachotenda. Pia secondary hapambani kukariri, lugha anaijua hivyo masomo hayawi magumu sana kwake
 
Shule ya msingi asome private. Ukiangalia syllabus za primary private zinacover secondary Kwa asilimia zaidi ya 70. Mtafute alie darasa la sita mpe paper za form 2, civics,geography, English, biology uone atakachotenda. Pia secondary hapambani kukariri, lugha anaijua hivyo masomo hayawi magumu sana kwake
 
Primary ndio msingi mkuu. Changamoto inayowakumba wanafunzi wengi wa sekondari ni uwezo mdogo wa kuelewa na kujieleza kwa lugha ya kiingereza. Hivyo basi, akitoka na msingi mzuri primary school atamudu masomo yake akiwa sekondari. Wengi wakiwa sekondari wanakariri kwa sababu lugha inawapiga chenga.
 
Option nionazo ni mbili kwa upande wangu.
1.Mpeleke primary shule ya government Ila hakikisha unamsimamia kila nukta huku unawekeza ktk tuition, secondary mpeleke private maana ndo life linaanzia hapo.


2.Aanzie darasa la awali mpaka class 3 private Kisha mrudishe government aingie la4 mpaka la7.
Secondary mpeleke private.
Darasa la3 kwa shule nzuri ya English medium inatosha kabisa kwa mtoto kuwa vizur ktk lugha.

Kwa government tatzo la watoto wetu wanajisahau na mwisho wa siku wanaangukia pua hasa kidato Cha nne.
Na Kama ukimuanzisha primary ya private basi hata secondary ni private.
Nina ushahidi wa watoto wengi walokua private kwa primary Kisha wakafaulu government,ndani ya muda mfupi walipotea mazima.Nina wadogo zangu watatu walisoma private kwa primary na tena huyo mmoja alikua kipanga hasaaa na kufaulu shule kubwa ya government,Ila lastly alikuja kuumia.
Nafikir hakuna ufuatiliaji wa kimasomo na uangalizi ni mdogo Sana huku watoto wengi wakiwa hawana morali yakusoma.Labda advanced government ndo hua na spirit kubwa ya usomaji.
 
Nakushauri aanzie primary English medium,apate lugha ya malkia vizuri then sec mpeleke serikalini
 
Sawa kaka. Asante. Ngoja niwasikilize na wengine wanasemaje
Mimi nitakwambia kutokana na experience yangu, Primary school nimesoma shule bora kabisa Tanzania na nje ya Tanzania, sekondari nikasoma shule za serikali. Nilikuwa ninawaburuza darasani japokuwa nilikuwa mtoro, siyo mtu wa kujisomea lakinimsingi niliotoka nao huko ulifanya maisha yangu ya sekondari ya we marahisi sana. Wale wote walioniiga walifail siyo O'level wala advance. Ila msingi ulikuwa wa primary. So msomeshe primary apate msingi bora, samaki mkunje angali mdogo.
 
Mimi nitakwambia kutokana na experience yangu, Primary school nimesoma shule bora kabisa Tanzania na nje ya Tanzania, sekondari nikasoma shule za serikali. Nilikuwa ninawaburuza darasani japokuwa nilikuwa mtoro, siyo mtu wa kujisomea lakinimsingi niliotoka nao huko ulifanya maisha yangu ya sekondari ya we marahisi sana. Wale wote walioniiga walifail siyo O'level wala advance. Ila msingi ulikuwa wa primary. So msomeshe primary apate msingi bora, samaki mkunje angali mdogo.
Sasa hivi upo Halmashauri gani Kikazi?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom