jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Wanajamvi,
Kwanza kabisa, niseme kama COVID-19 ingekuwa mbaya Tanzania, Lissu asingepata huu umati wa ajabu wenye Watanzania wenye hamasa ambayo sidhani kama nimeshawahi kuiona kwenye siasa za Tanzania. Hili ni la kumshukuru Mungu! Amejibu maombi kwa namna ya ajabu kabisa!
Amejibu maombi kwa namna ya ajabu, sambamba na kufanya muujiza mkuu kwa maisha ya Lissu. Hili, ni pamoja na kwamba maombi ya kumuombea ndugu Lissu ili Mungu amuepushe na mauti iliyokuwa ikimkabili, yalizuiliwa na serikali ambayo juzi tu rais amepewa “tuzo ya corona”🤦🏾♂️ Hili hata yeye mwenyewe “alijihisi”, akasema “tuzo hii ni ya Mungu”.
Lissu nimemsikia akizungumza yote yaliyotokea baada ya kutaka kuuwawa kwa kumiminiwa risasi 16 mwilini! Lakini sijamsikia akigusia hili la wananchi kuzuiwa kumuombea! Kwa wengi wenye imani, limetushangaza sana! Makanisa haya haya, yamesahau? Kwa sababu hata dini zenyewe zinatutaka tuwaombee wote! Hata wale waliotukosea! Lakini kwenye hili la kushambuliwa kwa Lissu, hayo makanisa yalikuwa kimya! Na juzi yakaibuka na issue ya “Amani”, lakini hawataki haki! Ndiyo maana dhuluma na kila aina ya uchafu na wachawi wamejaa kwenye nyumba za ibada!
Sasa kwenye siasa za Tanzania, ulianza muujiza wa Lissu, kisha wa Corona, halafu sasa ni siasa za Tanzania! Kwa wale ambao watakuwa wameshasoma maandishi yangu humu, nilisema kitambo kabisa kuwa “siku Tundu Lissu akitua nchini, basi siasa za Tanzania zinabadilika papo hapo”.
Kinachotokea sasa ni muujiza mwingine! Mungu akitupa uzima, hii thread mtaniambia kama Lissu haendi Ikulu. Najuwa wengi watabeza! Lakini “time will tell”, tena siyo muda mrefu! Nimeona hamasa ya vijana wa Tanzania, wakike kwa wakiume! Wababa watu wazima, wazee, na wamama wengine wamebeba watoto migongoni wakihatarisha usalama wao na watoto wao! Wakiwa na hamasa ya kumona tu na kumsikia Lissu! Kwenye video clip moja, nimeona wakiimba kwa hamasa ya hali ya juu sana! Wakisema “Hatuogopi bunduki”. Sijui kama ni kule Mbozi ambapo OCD alitaka kuwazuia wananchi kwenda kumuona Lissu! Baadaye akagwaya kwa “nguvu ya umma”.
Kwa wale viongozi wa dini, nadhani wapokee ushauri wa Dkt. Bagonza, kwamba “Amani ni tunda la Haki”
Kwa wale wanaobeza, naomba watambuwe kuwa, salama ya Taifa letu, ipo kwenye “uchaguzi huru na wa haki”.
Niishie hapa kwa sasa, nikiamini kwamba, wale wote watakaoinuka kinyume na nguvu za haki ya Mungu wa miujiza, wataangamia!
Kwanza kabisa, niseme kama COVID-19 ingekuwa mbaya Tanzania, Lissu asingepata huu umati wa ajabu wenye Watanzania wenye hamasa ambayo sidhani kama nimeshawahi kuiona kwenye siasa za Tanzania. Hili ni la kumshukuru Mungu! Amejibu maombi kwa namna ya ajabu kabisa!
Amejibu maombi kwa namna ya ajabu, sambamba na kufanya muujiza mkuu kwa maisha ya Lissu. Hili, ni pamoja na kwamba maombi ya kumuombea ndugu Lissu ili Mungu amuepushe na mauti iliyokuwa ikimkabili, yalizuiliwa na serikali ambayo juzi tu rais amepewa “tuzo ya corona”🤦🏾♂️ Hili hata yeye mwenyewe “alijihisi”, akasema “tuzo hii ni ya Mungu”.
Lissu nimemsikia akizungumza yote yaliyotokea baada ya kutaka kuuwawa kwa kumiminiwa risasi 16 mwilini! Lakini sijamsikia akigusia hili la wananchi kuzuiwa kumuombea! Kwa wengi wenye imani, limetushangaza sana! Makanisa haya haya, yamesahau? Kwa sababu hata dini zenyewe zinatutaka tuwaombee wote! Hata wale waliotukosea! Lakini kwenye hili la kushambuliwa kwa Lissu, hayo makanisa yalikuwa kimya! Na juzi yakaibuka na issue ya “Amani”, lakini hawataki haki! Ndiyo maana dhuluma na kila aina ya uchafu na wachawi wamejaa kwenye nyumba za ibada!
Sasa kwenye siasa za Tanzania, ulianza muujiza wa Lissu, kisha wa Corona, halafu sasa ni siasa za Tanzania! Kwa wale ambao watakuwa wameshasoma maandishi yangu humu, nilisema kitambo kabisa kuwa “siku Tundu Lissu akitua nchini, basi siasa za Tanzania zinabadilika papo hapo”.
Kinachotokea sasa ni muujiza mwingine! Mungu akitupa uzima, hii thread mtaniambia kama Lissu haendi Ikulu. Najuwa wengi watabeza! Lakini “time will tell”, tena siyo muda mrefu! Nimeona hamasa ya vijana wa Tanzania, wakike kwa wakiume! Wababa watu wazima, wazee, na wamama wengine wamebeba watoto migongoni wakihatarisha usalama wao na watoto wao! Wakiwa na hamasa ya kumona tu na kumsikia Lissu! Kwenye video clip moja, nimeona wakiimba kwa hamasa ya hali ya juu sana! Wakisema “Hatuogopi bunduki”. Sijui kama ni kule Mbozi ambapo OCD alitaka kuwazuia wananchi kwenda kumuona Lissu! Baadaye akagwaya kwa “nguvu ya umma”.
Kwa wale viongozi wa dini, nadhani wapokee ushauri wa Dkt. Bagonza, kwamba “Amani ni tunda la Haki”
Kwa wale wanaobeza, naomba watambuwe kuwa, salama ya Taifa letu, ipo kwenye “uchaguzi huru na wa haki”.
Niishie hapa kwa sasa, nikiamini kwamba, wale wote watakaoinuka kinyume na nguvu za haki ya Mungu wa miujiza, wataangamia!