Mitungi ya gesi sasa kuundwa nchini Tanzania

elivina shambuni

JF-Expert Member
May 31, 2018
461
295
1571754411905.png


KAMA unatumia mtungi wa gesi ya kupikia nyumbani kwako, basi fahamu kwamba mtungi huo umeundwa nje ya nchi. Lakini muda si mrefu, mitungi ya aina hiyo itaanza kutengenezwa Tanzania na gharama zake zinatarajiwa kuwa nafuu kuliko ilivyo sasa.

Akizungumza katika Maonesho ya Viwanda Mkoani Pwani, Meneja Masoko wa kampuni ya Lake Gas ambayo ni kampuni tanzu ya Lake Group, Ramadhani Siasa alisema kampuni yao inatarajia kuanza uzalishaji wa mitungi ya gesi mwezi Desemba mwaka huu. “Kwa sasa mitungi ya gesi za majumbani zinazotumiwa na makampuni mbalimbali inatoka nje.

Sisi tutaanza uzalishaji na hayo makampuni yatakuja kununua kwetu na kupaka rangi zao,” alisema Siasa. Maonesho ya Viwanda mkoani Pwani yaliyofunguliwa Oktoba 17 na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, yanatarajiwa kufungwa kesho na Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda. Watu wanaotembelea maonesho haya wamekuwa wakijionea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na viwanda mkoani Pwani na kupata nafasi ya kujinunulia baadhi ya bidhaa hizo kwa bei rahisi.


Chanzo: Habarileo
 
Nina kuambia utakuja niambia kama kutakuja kuwa na unafuu wowote ule, hiyo Cement ya dangote tuliaminishwa nini wakati kiwanda kinajengwa?? Yaani wanasiasa baada ya shetani kuchomwa moto, watafuata wao!! Waliwaaminisha watu eti mkoa wa mtwara mfuko utakuwa shilingi 4000!!!,inshu sio bidhaa inatengenezwa wapi, tatizo la tz ni gharama kubwa za uzarishaji bidhaaa pamoja na kodi kubwa!!!! Ndio zinapandisha bei!!! Vitu vingapi vinatoka Pakistan, brazil vinakuwa na bei ndogo kuliko kitu kinachozalishwa vingunguti?!! Halafu mwanasiasa anakwambia tupende vya kwetu!!!! Ndio uzalendo, kwa mtu masikini hata tofauti ya tsh,,500 ni kubwa mno kwake!!!
 
Nina kuambia utakuja niambia kama kutakuja kuwa na unafuu wowote ule, hiyo Cement ya dangote tuliaminishwa nini wakati kiwanda kinajengwa?? Yaani wanasiasa baada ya shetani kuchomwa moto, watafuata wao!! Waliwaaminisha watu eti mkoa wa mtwara mfuko utakuwa shilingi 4000!!!,inshu sio bidhaa inatengenezwa wapi, tatizo la tz ni gharama kubwa za uzarishaji bidhaaa pamoja na kodi kubwa!!!! Ndio zinapandisha bei!!! Vitu vingapi vinatoka Pakistan, brazil vinakuwa na bei ndogo kuliko kitu kinachozalishwa vingunguti?!! Halafu mwanasiasa anakwambia tupende vya kwetu!!!! Ndio uzalendo, kwa mtu masikini hata tofauti ya tsh,,500 ni kubwa mno kwake!!!
Jiwe anapenda kula pakubwa
 
Zinaweza zikaindwa tanzania na gharama zijwa juu. Ni kma cement inayotengnezwa tz bei juu kuliko inayotoka nje.
 
Hiyo mitungi itachomelewa na wachoma welding halafu gesi lazima ivuje...kinachofuata mnakifahamu

Mitungi lazima ifanyike robotic TIG/MIG welding ili ilipe. Testing yake lazima pia ifanyike ili kujua kama itafanya kazi kwa ubora na bila shida, especially pressure test.
Ila wawekezaji wenye uthubutu kama huyo sio wakubezwa. Some of those things can be done. Knowledge yake sio kitu cha ajabu sana
 
Nina kuambia utakuja niambia kama kutakuja kuwa na unafuu wowote ule, hiyo Cement ya dangote tuliaminishwa nini wakati kiwanda kinajengwa?? Yaani wanasiasa baada ya shetani kuchomwa moto, watafuata wao!! Waliwaaminisha watu eti mkoa wa mtwara mfuko utakuwa shilingi 4000!!!,inshu sio bidhaa inatengenezwa wapi, tatizo la tz ni gharama kubwa za uzarishaji bidhaaa pamoja na kodi kubwa!!!! Ndio zinapandisha bei!!! Vitu vingapi vinatoka Pakistan, brazil vinakuwa na bei ndogo kuliko kitu kinachozalishwa vingunguti?!! Halafu mwanasiasa anakwambia tupende vya kwetu!!!! Ndio uzalendo, kwa mtu masikini hata tofauti ya tsh,,500 ni kubwa mno kwake!!!
Nimekukumbuka kweli
 
Back
Top Bottom