Mitihani ya mock nchini isimamiwe na Baraza la mitihani NECTA kuiongezea TIJA

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,463
17,291
Wadau wa elimu nchini.

Ipo haja mitihani hii isimamiwe na NECTA ILI kuiongezea TIJA na mkazo mashuleni KULIKO ulivyo Sasa.

Napendekeza yafuatayo kufanyika.

1. RATIBA

Ratiba ya ufanyikaji wake iwe sawa kote nchini ILI kuepusha ratiba kutofautiana toka mkoa mmoja hadi Mwingine kama Sasa. Hii italeta uwajibikaji wa pamoja(collective responsibility) kwa walimu kiufundishaji na utimizaji wa syllabus KWA wakati ILI kuwaandaa vijana na mitihani huo! Napendekeza Ratiba iwe fixed Mwezi wa nane au wa Tisa miezi miwili kabla ya mitihaniya Taifa. Hii itaepusha kila mkoa KUWA na mitihani yake na ratiba zake.

2. UTUNGAJI WA MITIHANI
Mitihani itungwe na Baraza kwa kufuata utaratibu kama ile ya Taifa, iwe yenye TIJA na kuwapima wahusika kidato cha nne, pili na Darasa la saba! kuepusha utungaji holela wa mitihani kama Sasa tena kwa zimamoto. Walimu wanapigiwa simu ghafula watunge mitihani haraka haraka matokeo yake unakuwa chini ya kiwango. Napendekeza Baraza litunge mitihani hii.

3. RASILIMALI FEDHA
Baraza litaagiza watahiniwa wasajiliwe mapema kama kawaida, wajue idadi yao mapema halafu liombe kibali toka hazina kuingizwa fedha za elimu Bure automatic kutokana na idadi ya ya watahiniwa kwa KILA Shule nchini, Fedha hizo zitatumika kuandaa mitihani! Napendekeza sh.7000/= kwa KILA mwanafunzi. Itasaidia kuepuka sarakasi na ubadhirifu wa fedha hizi unaofanywa na Maafisa elimu na kufanya mitihani hii kutokuwa na tija KWA watahiniwa,

4. USAHISHAJI NA USIMAMIZI
Mitihani isahishwe kimkoa vitengwe vituo maalumu KWA usahishaji chini ya uangalizi wa Baraza kea kuteua wawakilishi wasimamizi wakuu wa zoezi Hilo!

Wasahishaji wawachague wenyewe kwa KUTUMIA database yao KWA KILA mkoa.Hii itawapa fursa na exposure walimu wengi na kuwajengea uzoefu na uweledi katika utendaji KULIKO ilivyo Sasa ambapo walimu wanaosahisha MITIHANI ya NECTA ni wachache ukilinganisha na idadi yao nchini.

Usimamizi upewe uzito kama mitihani ya NECTA ilivyo kuongeza tija KWA mitihani hii.

NB: Napendekeza kile kikosi KAZI cha mtaala mpya wa elimu nchini kiharakishe mchakato, wimbi la vijana wasio na ajira nchini linaongezeka kwa Kasi Sana.

"Mzee Warioba arudishwe kwenye kikosi kazi cha mkandala mchakato wa katiba mpya ukamilike"
 
Kuna mkoa keshokutwa wanaanza mock ya tatu (mock mbili na pre-necta moja tayari), hiyo itakuwa ya wilaya na baada ya hapo kutakuwa na mock iv itakayoandaliwa na mkoa kabla ya kukutana na mtihani wa taifa.

Ni kwamba wanafunzi hawa wa kidato ii na iv ni kama vile walimu wameshanyang'anywa kwa mwaka huu maana sijui kama kuna muda tena wa kukutana nao kutokana na ratiba hz.
 
Kuna mkoa keshokutwa wanaanza mock ya tatu (mock mbili na pre-necta moja tayari), hiyo itakuwa ya wilaya na baada ya hapo kutakuwa na mock iv itakayoandaliwa na mkoa kabla ya kukutana na mtihani wa taifa. Ni kwamba wanafunzi hawa wa kidato ii na iv ni kama vile walimu wameshanyang'anywa kwa mwaka huu maana sijui kama kuna muda tena wa kukutana nao kutokana na ratiba hz.
Utitiri wa mitihani ni ulaji wa maafisa Elimu wilaya na mkoa!

Ndio màana Wana tunga mitihani kibao!!
 
Kuna mkoa keshokutwa wanaanza mock ya tatu (mock mbili na pre-necta moja tayari), hiyo itakuwa ya wilaya na baada ya hapo kutakuwa na mock iv itakayoandaliwa na mkoa kabla ya kukutana na mtihani wa taifa. Ni kwamba wanafunzi hawa wa kidato ii na iv ni kama vile walimu wameshanyang'anywa kwa mwaka huu maana sijui kama kuna muda tena wa kukutana nao kutokana na ratiba hz.
Inakera kweli.
 
Yani ni sawa sawa na mandonga na mwakinyo wawe na pambano mwezi December la kushindania taji fulani, halafu kabla ya pambano hilo...
Ungejua UPUUZI uliopo usingeandika hicho ulichoandika!;

Yaani vurugu hakuna weledi! unaweza kurupushwa USIKU utunge mitihani KESHO inahitajika!

Na WEWE utakurupuka kama kawa!!
"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"
 
Ungejua UPUUZI uliopo usingeandika hicho ulichoandika!;

Yaani vurugu hakuna weledi! unaweza kurupushwa USIKU utunge mitihani KESHO inahitajika!

Na WEWE utakurupuka kama kawa!!
"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"
Mwaka jana 2021, mock mkoa wa Iringa iliyofanyika mwezi wa 5 ndiyo ikawa pre - necta ya mkoa wa Dodoma mwezi wa 8.

Kiufupi, mock ni copy and paste ya mitihani ya taifa miaka iliyotangulia au mock ya mikoa mingine (inatumwa kwenye magroup whatsapp).
 
Yani ni sawa sawa na mandonga na mwakinyo wawe na pambano mwezi December la kushindania taji fulani, halafu kabla ya pambano hilo...
Umemaliza kaka!! Upo sahihi sana!!

Hata mimi siungi mkono hoja za mtoa mada, kwa kweli itakuwa haina maana!!
 
Huo mchango wa shilingi elfu saba kwa kila mwanafunzi unadhani unatosha kuendesha shughuli zote???bado ni pesa kidogo sana labda ungesema kila mwanafunzi atoe elfu thelathini ..
 
Maslai ya Walimu yazungumziwe pia
Mitihani ya taifa watoto wanafaulu hamna shida
 
Elimu yetu bado inashida sana! mock ya mkoa mzima unapanga walimu 17 wamark script elfu 20 za civics kwa siku 8 is it possible?
 
Back
Top Bottom