Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 218,501
- 911,136
Gazeti la "Habari Leo" la leo limetuhabarisha ya kuwa mitihani ya kidato cha pili imeibwa....................Hili sakata za kuvuja kwa mitihani Baraza la Mitihani sasa limekuwa ni ngonjera ambayo pamoja na jitihada mbalimbali za kuziba mianya ya kuibwa kwa mitihani yaelekea uongozi uliopo pale siyo bunifu na ungepaswa kuondolewa......................lakini katika utamaduni wa kupeana vyeo serikalini kwa kujuana jitihada za kuwaondoa viongozi butu hizo ni ndoto za alinacha........................Tutaendelea kudhoofisha elimu yetu kila siku kwa kushindwa kutofautisha mahusiano kazini na mahitaji ya kitija.....................