Mitandao ya Twitter na YouTube haipatikani Tanzania bila VPN | Septemba 07, 2021

sijaelewa alikuwa anapataje siri wakati wa JPM ,Sasa hivi unaona kabisa na yeye pia anategemea connection
Unajuwa JPM katika mambo alikuwa dhaifu alikuwa hana break hata siri za intelligence alikuwa anaropoka tu sio kwa nia mbaya ila hakujuwa kuweka kifuani kitu. Kama unakumbuka sijui wakati wa kupokea report ya madini akasema huyu mwenzetu hana hatia kwa maana ni jasusi au siku alipokwenda Airport kukagua machine akamwambia yule Mama hivi wewe hujiulizi kwanini nimekuja kukagua hii machine? unajuwa Rais taasisi kubwa na anapata info nyingi sana daily ila mzee hakuwa na kifua za kuweka siri ndio maana ilikuwa rahisi sana kujuwa anafanya nini maana alikuwa na majibu ya hapo kwa hapo alikuwa na nia safi tu au hulka ya mtu kuna watu hawajui kuweka siri anaweza asilale mpaka aseme ndio usingizi unakuja. Mama sio muongeaji sana na kaweka team mpya ndio maana jamaa kahamia ugomvi wa Simba na Yanga kawa chawa na yeye apate kuishi.
 
Wameanza ujinga uliokithiri sasa, aliyewaambia watu wote wanatumia YouTube na Twiter kufuatilia siasa ni nani, then kama wanajiamini wapige kazi, woga hautawapeleka popote, ndo wanazidi kuharibu zaidi.
 
Wameanza ujinga uliokithiri sasa, aliyewaambia watu wote wanatumia YouTube na Twiter kufuatilia siasa ni nani, then kama wanajiamini wapige kazi, woga hautawapeleka popote, ndo wanazidi kuharibu zaidi.
Nafikiri hii ndio maana halisi ya slogan 'kazi iendelee'!
 
Katika hali ya kushtusha Leo 7/9/2021 majira ya kuanzia saa 5 na nusu, mitandao maarufu ya kijamii Twitter na YouTube haipatikani bila VPN.

Mtumiaji atalazimika kuwasha VPN ili kuendelea kufurahia kutumia mitandao hiyo. Mitandao hiyo siku za karibuni imekuwa ikitumika kama platform ya chama upinzani(CHADEMA) kujadili ajenda zake, mfano CHADEMA wamekuwa wakitumia jukwaa maarufu la Twitter lijulikanalo kama SPACE na Pia imekuwa iktumia mtandao wa YouTube kushea matukio yake mbalimbali.

Chama kikuu cha upinzani kimelazimika kutumia zaidi mitandao ya kijamii kwa shughuli zake za ukuzaji chama baada ya mazingira ya kukutana ana kwa ana ndani ya nchi yao kutokua rafiki.

Katika hali ya kushtusha Leo 7/9/2021 majira ya kuanzia saa 5 na nusu, mitandao maarufu ya kijamii Twitter na YouTube haipatikani bila VPN.

Mtumiaji atalazimika kuwasha VPN ili kuendelea kufurahia kutumia mitandao hiyo. Mitandao hiyo siku za karibuni imekuwa ikitumika kama platform ya chama upinzani(CHADEMA) kujadili ajenda zake, mfano CHADEMA wamekuwa wakitumia jukwaa maarufu la Twitter lijulikanalo kama SPACE na Pia imekuwa iktumia mtandao wa YouTube kushea matukio yake mbalimbali.

Chama kikuu cha upinzani kimelazimika kutumia zaidi mitandao ya kijamii kwa shughuli zake za ukuzaji chama baada ya mazingira ya kukutana ana kwa ana ndani ya nchi yao kutokua rafiki.
Afadhali ungeandika taarifa kuhusu utabiri wa hali ya hewa- maana imetangazwa kuwa mvua itakuwa kidogo au kwenu huko mnakula twitter. Ni MAONI YANGU TU. usije ukaja na jibu kuwa NISIKUAMURIE CHA KUANDIKA- ila mimi na wewe jambo moja tu linatuanganisha- KULA.
 
Back
Top Bottom