BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,009
Mitambo ya Songas yafikia kikomo kuzalisha gesi |
Thursday, 28 July 2011 20:59 |
Said Powa, aliyekuwa Kilwa Mwananchi KAMPUNI inayochimbaji, kusafirisha na kuzalisha umeme wa gesi ya Songas, imesema haina uwezo wa kuongeza uzalishaji wa gesi kwa sababu uwezo wa mitambo yake, umefikia kikomo. Akizungumza na waandishi wa habari katika Kisiwa cha Songosongo, wilayani Kilwa juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Chris Ford, alisema uwezo wa mitambo iliyopo ni kuzalisha gesi, umefikia kiwango cha mwisho licha ya kwamba bado visima vilivyoko vina gesi ya kutosha. "Mahitaji ya gesi ni makubwa kutokana na kuongezeka kwa matumizi yake na kwa sababu hiyo hata hiyo mitambo ya megawati 100 ambayo serikali imeinunua haitapata gesi na hakuna njia ya haraka kuweza kutatua tatizo hili," alisema Mkurugenzi huyo. Ford alisema kwa msingi huo, serikali inapaswa kutafuta njia mbadala ya kuzalisha umeme na si kwa kutegemea gesi.Mkurugenzi huyo alisema mpango uliopo kwa sasa ni kujenga kituo kingine cha kusafisha gesi kitakachogharimu zaidi ya Dola 170 millioni za Marekani na kwamba kazi hiyo itachukuwa zaidi ya miezi 18 kukamilika. Ford pia alisema matumizi ya gesi kwa kampuni binafsi katika Jiji la Dar es Salaam, yameongezeka hadi kufikia asilimia 35."Kutokana na matatizo yaliopo, nadhani wakati sasa umefika kwa serikali kuruhusu kampuni binafsi kuzalisha umeme (Mhhhhh!) , ili kukabiliana na upungufu uliopo katika nashati hiyo," alisema Ford. Wakati huohuo Kaimu Meneja Mkuu wa Pan African, William Chiume, amekanusha taarifa kwamba visima vya gesi na mabomba ya kusafirishia, yamejaa kutu na hivyo kushindwa kuzalisha.Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) imesema imeleta mtambo wa kufulia umeme utakaotumia gesi na kwamba mtambo huo una uwezo wa kuzalisha megawati 100. Chiume amesema matatizo yaliyokuwapo katika kisima kimoja kati ya visima sita vinavyozalisha gesi na kwamba hadi sasa bado kimefungwa kikisubiri kufanyiwa ukarabati maalum. |