Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,419
- 21,245
SERIKALI imesema suala la kutaifisha mitambo ya umeme ya Dowans kwa ajili ya kukabili hali ya mgawo wa umeme, si sera ya Serikali ya CCM, kwa kuwa hutekeleza kila jambo kwa mujibu wa sheria.
Aidha, imewahadharisha viongozi na wanasiasa kuacha kutumia tatizo lililopo la umeme kutoa matamko ya kujitafutia sifa na badala yake wazingatie zaidi mustakabali wa Taifa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alipozungumza na HABARILEO katika mahojiano maalumu kuhusu hali ya umeme nchini.
Kuhusu kutaifisha mitambo ya Dowans, nasema wazi na nataka ieleweke, hii si sera ya Serikali ya CCM, tukiendekeza mambo ya kutaifisha, leo tutataifisha Dowans kesho tutakwenda hadi kwenye mali za wananchi, alisema Ngeleja.
Alisema Tanzania inaongozwa kwa misingi ya utawala bora ambayo inazingatia utawala wa sheria.
Katika mazingira haya, ili utaifishe mali ya mtu lazima upitie mchakato wa kisheria tena kwa kuzingatia sheria za nchi zilizopo.
Alisema kwa mgawo wa umeme sasa, kumekuwa na kauli mbalimbali za wanasiasa ambazo hazina tija na nyingi zimejaa kujipatia umaarufu, hali ambayo ;haisaidii kutatua tatizo halisi lililopo.
Ombi langu, tujadili suala hili la upungufu wa umeme na juhudi za utatuzi wake kwa kuzingatia misingi tuliyojiwekea, naomba wananchi wapuuze kauli zinazotolewa na wanasiasa zenye majibu ya mkato kwa mambo mazito, alisema.
Aliwataka wanasiasa kuacha mara moja kutumia nafasi hiyo ya upungufu wa umeme kupotosha Watanzania na ulimwengu kwa kutaka sifa au umaarufu kisiasa.
Nasisitiza haya nikitambua kwamba katika mazingira yaliyopo ya mgawo wa umeme na hasira walizonazo wananchi kutokana na tatizo hilo, ni rahisi kwao kupotoshwa na wanasiasa wanaotaka sifa bila kuzingatia mustakabali wa nchi yetu, alisema Ngeleja.
Pia Ngeleja aliomba wananchi waunganishe nguvu kupitia viongozi wao wa dini, ili angalau mvua zinyeshe na mabwawa yanayozalisha umeme kwa kutumia maji yajae.
Akizungumzia suala la kauli yake aliyoitoa bungeni kuhusu umeme, alikanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa hali ya umeme itatengemaa mwaka 2033 na kuongeza kuwa huo ni uzushi na kwamba upo mpango mkakati wa miradi ya umeme unaoanzia mwaka 2009 hadi 2033.
Alisema mpango mkakati huo unajumuisha miradi mingi ya muda mrefu, kati na mfupi, ambayo mingine tayari imekamilika na kutoa umeme akitolea mfano mradi wa umeme wa Ubungo wa megawati 100 na wa Tegeta wa megawati 45.
Alisema inasikitisha kuwa wapo baadhi ya watu wanaodhani kuwa Serikali haijafanya lolote kuhusu umeme ambapo alisema kama lisingekuwapo tatizo la umiliki katika mgodi wa Kiwira wa megawati 200 kuanzia mwaka 2005 hadi 2010, Serikali ingekuwa na nyongeza ya umeme wa megawati 645.
Ngeleja alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya wabunge kutoa hoja ya kuikodi kwa miezi mitatu au kutaifishwa kwa mitambo ya Dowans ili kumaliza tatizo la umeme akiwamo Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, January Makamba.
Februari 16 pia baadhi ya wanasheria waandamizi nchini walisema mitambo ya Dowans haiwezi kutaifishwa kwa sababu kampuni hiyo haikabiliwi na kesi ya uhujumu uchumi lakini pia kuingia mkataba mwingine na kampuni hiyo ni mzigo kwa Serikali.
Aidha, imewahadharisha viongozi na wanasiasa kuacha kutumia tatizo lililopo la umeme kutoa matamko ya kujitafutia sifa na badala yake wazingatie zaidi mustakabali wa Taifa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alipozungumza na HABARILEO katika mahojiano maalumu kuhusu hali ya umeme nchini.
Kuhusu kutaifisha mitambo ya Dowans, nasema wazi na nataka ieleweke, hii si sera ya Serikali ya CCM, tukiendekeza mambo ya kutaifisha, leo tutataifisha Dowans kesho tutakwenda hadi kwenye mali za wananchi, alisema Ngeleja.
Alisema Tanzania inaongozwa kwa misingi ya utawala bora ambayo inazingatia utawala wa sheria.
Katika mazingira haya, ili utaifishe mali ya mtu lazima upitie mchakato wa kisheria tena kwa kuzingatia sheria za nchi zilizopo.
Alisema kwa mgawo wa umeme sasa, kumekuwa na kauli mbalimbali za wanasiasa ambazo hazina tija na nyingi zimejaa kujipatia umaarufu, hali ambayo ;haisaidii kutatua tatizo halisi lililopo.
Ombi langu, tujadili suala hili la upungufu wa umeme na juhudi za utatuzi wake kwa kuzingatia misingi tuliyojiwekea, naomba wananchi wapuuze kauli zinazotolewa na wanasiasa zenye majibu ya mkato kwa mambo mazito, alisema.
Aliwataka wanasiasa kuacha mara moja kutumia nafasi hiyo ya upungufu wa umeme kupotosha Watanzania na ulimwengu kwa kutaka sifa au umaarufu kisiasa.
Nasisitiza haya nikitambua kwamba katika mazingira yaliyopo ya mgawo wa umeme na hasira walizonazo wananchi kutokana na tatizo hilo, ni rahisi kwao kupotoshwa na wanasiasa wanaotaka sifa bila kuzingatia mustakabali wa nchi yetu, alisema Ngeleja.
Pia Ngeleja aliomba wananchi waunganishe nguvu kupitia viongozi wao wa dini, ili angalau mvua zinyeshe na mabwawa yanayozalisha umeme kwa kutumia maji yajae.
Akizungumzia suala la kauli yake aliyoitoa bungeni kuhusu umeme, alikanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa hali ya umeme itatengemaa mwaka 2033 na kuongeza kuwa huo ni uzushi na kwamba upo mpango mkakati wa miradi ya umeme unaoanzia mwaka 2009 hadi 2033.
Alisema mpango mkakati huo unajumuisha miradi mingi ya muda mrefu, kati na mfupi, ambayo mingine tayari imekamilika na kutoa umeme akitolea mfano mradi wa umeme wa Ubungo wa megawati 100 na wa Tegeta wa megawati 45.
Alisema inasikitisha kuwa wapo baadhi ya watu wanaodhani kuwa Serikali haijafanya lolote kuhusu umeme ambapo alisema kama lisingekuwapo tatizo la umiliki katika mgodi wa Kiwira wa megawati 200 kuanzia mwaka 2005 hadi 2010, Serikali ingekuwa na nyongeza ya umeme wa megawati 645.
Ngeleja alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya wabunge kutoa hoja ya kuikodi kwa miezi mitatu au kutaifishwa kwa mitambo ya Dowans ili kumaliza tatizo la umeme akiwamo Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, January Makamba.
Februari 16 pia baadhi ya wanasheria waandamizi nchini walisema mitambo ya Dowans haiwezi kutaifishwa kwa sababu kampuni hiyo haikabiliwi na kesi ya uhujumu uchumi lakini pia kuingia mkataba mwingine na kampuni hiyo ni mzigo kwa Serikali.