Misungwi: Walimu wawili wa shule za msingi wafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kubaka na kuwapa mimba wanafunzi mawili

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
746
3,058
Walimu wawili wa shule za msingi Mwagimagi na Kifune wilayani Misungwi mkoani Mwanza, wamefikishwa mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kubaka na kuwapa ujauzito wanafunzi wawili.

Walimu hao ni Telepholy Revocatus (32) wa Shule ya Msingi Mwagimagi na Peter Ferdinand (35) wa Shule ya Msingi Kifune.

Akisoma hati ya mashitaka mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi Mfawidhi, Erick Marley, mwendesha mashitaka wa polisi Ramsoney Salehe kwa kesi namba 117/ 2018 amedai mshtakiwa mwalimu Revocatus alitenda kosa hilo kati ya Januari na Februari, 2018.

Amedai mshtakiwa alimbaka na kumtia mimba mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwenye umri wa miaka 17 katika Sekondari ya Ilujamate wilayani hapo kinyume na kifungu cha 130(1) 2(e) na 131sura ya adhabu 16 iliyorekebishwa mwaka 2002.

Salehe alimsomea tena kesi ya jinai namba 107 /2018 Peter Ferdinand kwa kosa kama hilo la kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la saba wa Shule ya Msingi Kifune.

Watuhumiwa wote wako nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ambayo yalikuwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini bondi ya shilingi milini moja kila mmoja.

Hakimu Marley aliziahirisha kesi hizo hadi Septemba 26,2018

Chanzo: Mwananchi
 
Hivi wanafunzi wana starehe gani wakuu? Yaani unasukuma 'steki' kabisa Kwa mwanafunzi...ni vile vichuchu vilivyosimama Kwa nguvu ya damu au?
 
Kuna misemo inawaponza hawa walimu ..
Eti ..
1. Mbuzi kula kwa urefu wa Kamba yake ..
2. Vya madhabahuni huliwa na wa madhabahuni
.... Ongeza na wewe .. hii ni misemo hatarishi; walimu ni marafiki zangu, tunaishi wote mitaani tunashirikiana katika mambo mbalimbali lakini katika hili siswaungi mkono hata kidogo; achene watoto wasome ..
Lakini aliwahi tokea rais akatamka eti .. wanafunzi wana viherehere ... hii ndo Bongo.
 
Walimu wawili wa shule za msingi Mwagimagi na Kifune wilayani Misungwi mkoani Mwanza, wamefikishwa mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kubaka na kuwapa ujauzito wanafunzi wawili.

Walimu hao ni Telepholy Revocatus (32) wa Shule ya Msingi Mwagimagi na Peter Ferdinand (35) wa Shule ya Msingi Kifune.

Akisoma hati ya mashitaka mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi Mfawidhi, Erick Marley, mwendesha mashitaka wa polisi Ramsoney Salehe kwa kesi namba 117/ 2018 amedai mshtakiwa mwalimu Revocatus alitenda kosa hilo kati ya Januari na Februari, 2018.

Amedai mshtakiwa alimbaka na kumtia mimba mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwenye umri wa miaka 17 katika Sekondari ya Ilujamate wilayani hapo kinyume na kifungu cha 130(1) 2(e) na 131sura ya adhabu 16 iliyorekebishwa mwaka 2002.

Salehe alimsomea tena kesi ya jinai namba 107 /2018 Peter Ferdinand kwa kosa kama hilo la kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la saba wa Shule ya Msingi Kifune.

Watuhumiwa wote wako nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ambayo yalikuwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini bondi ya shilingi milini moja kila mmoja.

Hakimu Marley aliziahirisha kesi hizo hadi Septemba 26,2018

Chanzo: Mwananchi
1. Kubaka mtoto (<18yrs old) kitu kinachodhibitishwa ni "PENETRATION OF PENIS INTO A VAGINA, However slight might be" pekee.

2. Kumpa mimba mwanafunzi kinachoangaliwa ni je mjamzito ni:-
(a) Mwanafunzi aliesajiliwa ama ana namba ya usajili katika shule ngazi ya hadi shule ya upili (both O'level & A'level).

(b) Ujauzito alipewa na mshitakiwa.

MADHARA WATAKAYOPATA WATUHUMIWA ENDAPO WATAKUTWA NA HATIA.

i/ Kutumikia kifungo cha miaka 30 kwa kila kosa adhabu ambayo itaenda sambamba. (Yaan watakaa jera miaka 20 sio 30 kamili)

ii/ Kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma (Na. 8/2002, kanuni zake za mwaka 2003 pamoja na kanuni za kudumu za mwaka 2009. Wataachishwa kazi katika utumishi wa umma.
IMG_20180919_170133_340.JPG
View attachment 871265
IMG_20180919_171048_769.JPG
 
Hii kesi imekaa vibaya sana...huyu Peter (mwlm wa Kifune) nilikutana nae siku tatu kabla ya mitihani ya Taifa japo sikupata nafasi ya kupiga nae story lkn nashindwa kuamini kwa jinsi ninavyomfaham...ni mtu fulani mtanashati,mtu wa watu
Mungu amsaidie sana ndugu yangu Peter!
 
Back
Top Bottom