Misukosuko ya Ndoa na Mshauri wa ndoa

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Ndugu wapendwa

Leo hii nimekuja kutoa Mawazo yangu kidogo jinsi ya kuokoa ndoa za watanzania,,, leo hii ndoa si kama wazee wetu walivyokuwa wakipendana kutoka moyoni,.... ndo zao leo hii zimejaa madhumuni kibao ambayo mengine yanawekwa kwenye imani yatatokea baada ya ndoa na hatari ni pale mambo yanapoenda kinyume harusi za leo zinaisha ndani ya siku saba,.

Nimekaa nkaona tusiporekebishana haya mambo hata sie wahudhuriaji makanisani tutaishia kubeba dhambi juu ya awa wanandoa wa leo kama mpenda maendeleo ya wanandoa ningeshauri kuwepo na jukwaa la wanandoa ama kama una mawazo yoyote ama umekumbana na misuko suko ukafanikiwa kuichomoa embu karibu hapa tupe dondoo tupate kushare jinsi ulivyofanikiwa kuhimili vishindo.

....wewe msomaji bwana harusi mtarajiwa unakaribishwa kupata hints nini cha kufanya na je baada ya ndoa kuna soln yoyote yakitokea matatizo....

Nawatakia ndoa njema zenye utulivu,tusaidiane kutoa mawazo endelevu jamani na kusaidia ndoa zetu,..yapo matatizo mengi katika ndoa ,...kama ni mwathirika mmoja wapo karibu jukwani tupate mawazo yako
 
...nasema hivi, sometimes inapotokea umri kwenda kombo hasa kwa akina dada, huamua kucheza karata zake zote na kumpata yeyote kwa njia yeyote ili afunge naye ndoa. hapo panakuwa na mapenzi ya uongo kwa ajili ya kupata sehemu ya kujishikizia. Baada ya muda mchache ndoa kufungwa mapenzi huporomoka kama barafu ya juani, na ndio ndoa nyingi za siku hizi.
 
Ninatafakari......nina ndoa ya 8yrs lakini mmmmmh kam vileninaenda salendaer kwa manyoya ya paka.
......Nitarudi jukwaa likianzishwa. Mx na invizibo mmesikia?
 
jamani nawaomba wenye uwezo kutuwezesha hili mi nina mengi sana
hivi natoka salender club kuhojiana na wanandoa tuliowasimamia pale
azania mwezi wa 11 sasa sijui...nasema sijui kama tutafika tusipoamka
wenyewe....
 
nasema hivi, sometimes inapotokea umri kwenda kombo hasa kwa akina dada, huamua kucheza karata zake zote na kumpata yeyote kwa njia yeyote ili afunge naye ndoa. hapo panakuwa na mapenzi ya uongo kwa ajili ya kupata sehemu ya kujishikizia. Baada ya muda mchache ndoa kufungwa mapenzi huporomoka kama barafu ya juani, na ndio ndoa nyingi za siku hizi.


yawezekana mpwa lakini wakngu imekuwa tofauti
mi nilikaa na kadada kabichi nkajua nimepata baada ya miezi mitatu nikashtuka nimepatikana baada ya muda nikamwomba mungu anisaidie kabla ya kunionyesha mwanamke alienizidi 2 yrs nina miaka 5 sasa naishi kama niko mbinguni
mcha mungu aibi,anamjua na kumpenda Mungu hela yake yangu yangu yake we acha tu
kwangu nikaja kujua age nayo iliniathiri kukimbilia vidogo maana nilikaita kama miaka miwiwli....we acha tu tuzaliwe tuyaone
 
...mwanahalisi, kukuzidi miaka 2 haimaanishi kuwa umri wake wa kupata mwenzi ulikuwa umeshapita! Labda utueleze alikuwa na umri gani wakati huo.
 
...nasema hivi, sometimes inapotokea umri kwenda kombo hasa kwa akina dada, huamua kucheza karata zake zote na kumpata yeyote kwa njia yeyote ili afunge naye ndoa. hapo panakuwa na mapenzi ya uongo kwa ajili ya kupata sehemu ya kujishikizia. Baada ya muda mchache ndoa kufungwa mapenzi huporomoka kama barafu ya juani, na ndio ndoa nyingi za siku hizi.

Huwa imatokea hata mwanaume umri kwenda kombo na kuamua kucheza karata kumpata yeyote ili afunge naye ndoa. Hapo inakuwaje bwana Mundu.
 
Hakuna kitu kizuri au jambo zuri au tamu duniani kama ndoa, yaani we acha tu.LAKINI hakuna maudhi,mateso,dhiki, unyama, ukatili unaoweza kuupata popote ukazidi wa kwenye ndoa.Waliomo wanataka kutoka na walionje wanataka kuingia.Ndoa ni kama umekata bahati nasibu, lakini huwezi kuichana ticketi baada ya kugundua hukushinda
Wazo zuri sana la kuanzisha jukwaa la wana ndoa, ndoa nyingi ni NDOANA, mjanja anamvua mwenzie na kwa vile samaki hawezi kuishi nchi kavu muda mwingi, mwisho hufa, hata ndoa ni hivyo hivyo baada ya mikwaruzo mingi mwisho ndoa HUFA
 
Ndugu wapendwa
leo hii nimekuja kutoa Mawazo yangu kidogo jinsi ya kuokoa
ndoa za watanzania,,,leo hii ndoa si kama wazee wetu walivyokuwa
wakipendana kutoka moyoni,....
kwanza naomba nikueleze kwamba ndoa za zamani nilikuwa na matatizo kama za sasa ila ni unyanyasaji na mfumo dume uliwanyima sana haki ya kuhoji wanawake wakati kwa sasa awareness na movement za usawa zimesaidia wanawake kujua na kutetea haki zao... vitu kama vipigo, matusi na masimango kwa sasa vimetungiwa sheria na pia akina mama wanaelimu na wengine wanafanya biashara nk. hivyo relevance ya paragraph one as far as i am concerned ni "qualified"
ndoa zao leo hii zimejaa madhumuni kibao ambayo mengine yanawekwa kwenye imani yatatokea baada ya ndoa na hatari ni pale mambo yanapoenda kinyume
hapo tuko pamoja sana, siku hizi ndoa nyingi ni circumstantial na pesa imepata mwenyewe (imeingia kwenye madhumuni ya ndoa, hii ni kwa tafiti kadhaa zhasa ulaya wanaweka haya mamo na sababu zake, kama sikosei...ukisoma Times online kwenye upande wa mahusiano kuna shule tamu sana ya haya mambo

harusi za leo zinaisha ndani ya siku saba,.
nimekaa nkaona tusiporekebishana haya mambo hata sie wahudhuriaji
makanisani tutaishia kubeba dhambi juu ya awa wanandoa wa leo
kama mpenda maendeleo ya wanandoa ningeshauri kuwepo na jukwaa
la wanandoa ama kama una mawazo yoyote ama umekumbana na misuko suko ukafanikiwa kuichomoa embu karibu hapa tupe dondoo tupate kushare jinsi ulivyofanikiwa kuhimili vishindo......wewe msomaji bwana harusi mtarajiwa unakaribishwa kupata hints nini cha kufanya na je baada ya ndoa kuna soln yoyote yakitokea matatizo....
Nawatakia ndoa njema zenye utulivu,tusaidiane kutoa mawazo endelevu jamani na kusaidia ndoa zetu,..yapo matatizo mengi katika ndoa ,...kama ni mwathirika mmoja wapo karibu jukwani tupate mawazo yako
ndoa has to be made for right reasons, kama sio righ reasons hata ufanyeje haitakuwa right, na solution ni wawili tu!!!

ushauri ni kwamba divorce ziwe zinaruhusiwa iwapo hakuna right reasons za kuwa pamoja, tusifanye wanawake watumwa kwenye ndoa zetu they have rights too; na akina mama wasifanye wababa mapunda kwenye ndoa kama haiwezekani, then tutambae
 
Huwa imatokea hata mwanaume umri kwenda kombo na kuamua kucheza karata kumpata yeyote ili afunge naye ndoa. Hapo inakuwaje bwana Mundu.

Moja ya wrong reasons kuingia kwenye ndoa
 
Nasema anzisheni hili jukwaa na liwekewe restrictions kama kule kwa wakubwa; ni muhimu sana!
Nina mengi ya kushea
 
Huwa imatokea hata mwanaume umri kwenda kombo na kuamua kucheza karata kumpata yeyote ili afunge naye ndoa. Hapo inakuwaje bwana Mundu.
Labda tujiulize kwanza, nani anakuwa na presha kubwa ya umri kati ya mwanaume na mwanamke?
 
ndoa ni kitu chema na kimeanzishwa na mungu mwenyewe na shetani anapigana sana na ndoa kwani anajua akishavuruga ndoa amavevuruga maisha na familia kwani mwanaume ukishindwa kwenye ndoa utashindwa pi kwenye maisha tunaitaji kujifunza kwanza kuhusu ndoa kabla ya kuingia kupitia vitabu,mahubiri shuhuda nk ikiwa mtu unakwenda kusomea digrii,masters na phd kwa miaka kadhaa inakuwaje unataka kuingia kwenye ndoa wiki moja tu na ufaidi naona hapo ndo shida inaanzaga
 
...nasema hivi, sometimes inapotokea umri kwenda kombo hasa kwa akina dada, huamua kucheza karata zake zote na kumpata yeyote kwa njia yeyote ili afunge naye ndoa. hapo panakuwa na mapenzi ya uongo kwa ajili ya kupata sehemu ya kujishikizia. Baada ya muda mchache ndoa kufungwa mapenzi huporomoka kama barafu ya juani, na ndio ndoa nyingi za siku hizi.
kwenda kombo ndio nini?
 
Back
Top Bottom