Misuguano ya ulaji yaibuka bandarini

Tina

JF-Expert Member
Jul 9, 2007
572
579
Misuguano ya ulaji yaibuka bandarini

MSUGUANO umeibuka ndani ya Bandari Tanzania (TPA) kutokana na kuwepo tuhuma za maandalizi ya manunuzi ya kifisadi kupitia kitengo cha manunuzi cha mamlaka hiyo, imefahamika.

Tuhuma hizo zimeibuka baada ya kuwapo kwa hatua za kufanya mabadiliko katika kitengo hicho na kuingizwa kwa watu ambao waliingia TPA katika mazingira tata, wakitokea maeneo alikotokea mmoja wa viongozi wa mamlaka hiyo.

Kabla ya kuingia kwa uongozi mpya chini ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Madeni Kipande, ziliibuka tuhuma za kuunda kitengo cha manunuzi (Management Procurement Unit-PMU) kwa ajili ya maslahi binafsi.

“Kilichofuata ni Kipande akiungwa mkono na wizara kuvunja PMU na Bodi za Ununuzi Bandari ya Dar es Salaam na Makao Makuu na kuunda Bodi Kuu ya Zabuni (CTB) wakidai uamuzi huo utakuwa muarobaini wa rushwa na ufisadi na hakutakuwepo athari zozote kiutendaji. “Wahenga husema mtoto akililia wembe mpe ajikate na sasa mambo yamebadilika,” anasema ofisa mwandamizi wa TPA.

Imeelezwa kwamba ndani ya mwaka mmoja sasa Kipande ameanza kulaumu kuwa Bodi ya Zabuni ya TPA inakwamisha ununuzi na hivyo kukwamisha ufanisi ndani ya TPA.

“Lawama hizo hata hivyo hazikuwa za ukweli kwa vile sheria ya ununuzi iko wazi, na CTB ilikuwa inaeleza wazi kuwa inaongozwa na sheria hiyo.

“Kipande na watu wake wakashindwa kufanya wanachotaka wao na sasa wanazirudisha zile bodi zilizovunjwa na kuweka watu wao,” anasema ofisa huyo ambaye yuko karibu na Kipande kiutendaji.

Habari ndani ya TPA na nyaraka ambazo Tanzania Daima imeziona zinaeleza kwamba Kipande ameunda bodi hizo zikisheheni watu kutoka TANROADS alikotokea.

Bodi mpya ya Ununuzi ya Bandari ya Dar es Salaam inaongozwa na Alois Matei, ambaye ni Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA (Miundombinu) kutoka Makao Makuu alitokea TANROAD S alikokuwa akifanya kazi na Kipande kabla ya TPA huku Bodi Kuu (CTB) ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu ambaye kwa muundo uliopo anafanya kazi chini ya Matei.

Kwa muundo huu Matei atawajibika kwa CTB ambayo iko chini ya “mfanyakazi” wake!

Mbali na hayo, Kipande pia kamteua ofisa mwingine kwenye Bodi ya Ununuzi ya Bandari ya Dar es Salaam ambaye ni William Shila, Kaimu Mkurugenzi wa Uhandisi ambaye naye aliletwa TPA akitokea TANROADS .

“Hivi hawa viongozi walioko makao makuu wanaingia vipi Bodi ya Ununuzi ya Bandari ya Dar es Salaam kama sio kwa lengo la kufanya ufisadi?

“Maajabu mengine ni kuwa mtumishi mmoja kateuliwa kuajiriwa bila usaili wowote pamoja na ukweli ambao umedhihirika kuwa hana uzoefu katika fani ya ununuzi jambo ambalo sheria ya manunuzi inakataza.

“Isitoshe mtumishi huyo pamoja na kutokuwa na sifa za kazi hiyo, ndiye kateuliwa na kuwa Katibu wa Bodi ya Ununuzi ya Bandari ya Dar es Salaam na kuwaacha wafanyakazi wazoefu na wenye uwezo wa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia sheria ya ununuzi,” anasema ofisa huyo akisema ni vyema serikali kuu ikafuatilia.

Tayari TPA imeingia kwenye misuguano ya muda mrefu toka kuingia kwa uongozi mpya kiasi cha bodi ya mamlaka hiyo kutaka kumsimamisha Kipande kabla ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kuivunja na kuunda mpya.

moja ya tuhuma ambazo bodi iliyovunjwa iliuhusisha uongozi wa Kipande ni pamoja na kuingiza kinyemela mradi wa tozo ya ufuatiliaji wa mizigo kwa mtandao (Eletronic Cargo Tracking Note, e-CTN) bila kufuata sheria na kanuni.

Tayari Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Majini na Nchi Kavu (Sumatra) ilishazuia mradi huo wa e-CTN usitishwe hadi taratibu zitakapofuatwa lakini habari sasa zinaeleza kwamba TPA iko kwenye mkakati wa kubadilisha baadhi ya vipengele kwenye sheria ya TPA ili iweze kutekeleza miradi yake bila udhibiti wowote.

.....
Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/misuguano-ya-ulaji-yaibuka-bandarini/
 
BW MADENI KIPANDE KWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA WAKAMIKISHA SAFU YA UFISADI KWA KUUNDA BODI YA UNUNUZI BANDARINI MAHSUSI KWA ULAJI.

Haujapita muda mrefu tangu umma wa Watanzania kufahamishwa kuwa uongozi wa TPA uliopita kabla ya Bwana Madeni Kipande ulituhumiwa kuunda Kitengo cha Management Procurement Unit (PMU) kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Kilichofuata ni Bwana Kipande ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, kuvunja PMU na Bodi za ununuzi Bandari ya DSM( port managers office) na Makao Makuu ( TPA Head quarters ) na kuunda Central Tender Board (CTB) moja. Bw. Madeni Kipande pamoja na waziri wake Mwakyembe walijigamba kuwa ununuzi kupitia CTB moja utakuwa ni muarobaini wa rushwa na ufisadi na kuwa hakutakuwepo athari zozote kiutendaji. Wahenga husema: mtoto akililia wembe mpe!

Ni ndani ya mwaka mmoja sasa , Bw. Kipande ameanza kulaumu kuwa CTB inakwamisha ununuzi na hivyo ufanisi ndani ya TPA. Lawama hizo hata hivyo hazikuwa za ukweli kwa vile sheria ya ununuzi iko wazi, na CTB ilikuwa inaeleza wazi kuwa inaongozwa na sheria hiyo. Bw. Kipande na waandani wake wakashindwa kufanya ufisadi wao.

Hivi sana Bw. Kipande na waandani wake wakijua wanalindwa na wizara wamekuja na mkakati mpya na kurudisha Bodi ya ununuzi Bandari ya DSM badala ya (TPA head quorters) na pia kufanya uteuzi wa wajumbe wa bodi hiyo ambao watakidhi matakwa yake ya kufanya ufisadi kadri anavyotaka kwa kuvunja sheria za manunuzi. Azma hii ya Bwana Kipande itatekelezwa kwa kuzingatia “composition” ya Bodi ya manunuzi aliyoiteua hivi karibuni. Bodi hiyo inaongozwa na Bwana Alois Matei, ambaye ni Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA (Miundombinu) kutoka Makao Makuu aliyeletwa Tpa akitokea TANROAD S alikokuwa akifanya kazi bwana Kipande kabla ya kuletwa TPA. CTB ambayo ni chombo cha juu cha kushughulikia masuala ya ununuzi ndani ya TPA kinaongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Raslimali Watu, ambaye kwa muundo uliopo anafanya kazi chini ya Bwana Matei. Lakini kwa muundo huu, Bwana Matei atawajibika kwa CTB ambayo iko chini ya “mfanyakazi” wake!

Mbali na hayo, Bwana Kipande pia kampachika swahiba wake mwingine kwenye Bodi ya Ununuzi ya Bandari ya DSM ambaye ni Bwana Shila, Kaimu Mkurugenzi wa Uhandisi aliyeletwa TPA akitokea TAN ROADS pia. Hivi hawa viongozi walioko makao makuu ( TPA head quarters) wanaingia vipi Bodi ya bandari ya DSM kama sio kwa lengo la kufanya ufisadi? Maajabu mengine ni kuwa Bwana James H. Gwagula, kateuliwa na Bwana Kipande kama Kaimu Meneja Ununuzi na Ugavi bandari ya DSM akitokea Serikalini akiwa ameajiriwa bila interview yoyote pamoja na ukweli ambao umedhihirika kuwa hana sifa za fani ya ununuzi na hajawahi kusomea fani hiyo na sheria ya manunuzi pia inakataza. Isitoshe, Bwana Gwagula pamoja na kutokuwa na sifa za kazi hiyo, ndie kateuliwa na Bwana Kipande kuwa Katibu wa Bodi ya Ununuzi ya Bandari ya DSM; na kuwaacha wafanyakazi wazoefu na wenye uwezo wa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia sheria ya ununuzi.



Inasitikisha sana kuona kuwa NJAMA ZA WAZI WAZI ZA KULA RUSHWA NA UFISADI kama huu huko TPA; ambayo ni taasisi inayohusisha manunuzi yenye thamani kubwa sana kwa kutumia fedha za walipa kodi zikijumuisha uvunjaji wa sheria ya ununuzi; zinaendelea kufanyika bila kuzuiliwa, achilia mbali kukemewa na Mamlaka husika awiwemo Waziri Mwakyembe anaejipambanua kama ni mpinga ufisadi kumbe na yeye ni sehemu ya tatizo .

Jamani tahadhari kabla ya hatari, na rai ya umma wa Watanzania ni kuwa njama hizi ni lazima zimulikwe mapema na vyombo vingine vya juu ili wahusika wawajibishwe mapema. Ufisadi mwingine ambao unapangwa kufanyika upya ni ule " Eletronic Cargo Tracking Note" ambao Kipande kwa kushirikiana na Waziri Mwakyembe waliingia mkataba na kampuni ya Ubelgiji bila kufuata sheria za manunuzi na pia bila wadau muhimu kuhusishwa.

Sumatra kwa mamlaka ya kisheria waliyo nayo waliingilia kati na kuusimamisha mradi kwa kuwa haukuwa na manufaa yoyote kwa walaji na hata kwa nchi. TPA kwa sasa wako kwenye mkakati wa kubadilisha baadhi ya vipengele kwenye TPA ACT ili waweze kutekeleza miradi yake pasipo kuingiliwa na Sumatra!! Waraka unaandaliwa upelekwe kwenye Bodi mpya ya TPA iliyozinduliwa huko Mtwara hivi majuzi baada ya ile Waziri aliyoiweka kwa mbwembe kuondolewa kwa kile kilichoelezwa ni kutaka kumwajibisha kaimu mkurugenzi mkuu bwana Kipande kitu ambacho Waziri
 
TINA ww uko kikazi zaidi toka umeanza ww ni bandari, Kipande na Dr Mwakyembe..ama kweli unaijua kazi yako..basi uwe unatupa na mazuri yanayoendelea hapo bandarini maana nina uakika yako!!
 
Undumila Kuwili wa Bw Madeni Kipande

Madeni Kipande anaendelea na mikakati yake ya kula rushwa na kujineemesha bila wasiwasi kwa vile analindwa na Mh. Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi pasipo kificho sasa, kutokana na yaliyobainishwa na Waraka wa Ulanga na pia Gazeti la Tanzania Daima la tarehe 27 Novemba 2014.

Isitoshe, sasa hivi anatoa vitisho kwa wakandarasi wanapotaka malipo yao aidha yawe ni genuine au ya kimchongo ili na yeye akatiwe rushwa. Mfano ulio hai ni pale alipojigamba kwa viapo kuwa hatalipa madai ya ziada ya kampuni ya Canopies International inayojenga gati huko Kiwira kiasi cha shilingi180.0.

Duru zetu zimegundua kuwa hii ilikuwa ni janja yake tu ili kujionyesha kwa wafanyakazi kuwa yeye ni mtu safi anaepiga vita rushwa kwa dhati kumbe ni muongo. Fedha hizi sasa zimelipwa kwa mkandarasi huyo bila kupungua hata senti tano tena kwa idhini yake yeye mwenyewe na kwa kuhimiza malipo hayo yafanyike haraka bila kucheleweshwa!

Hii inathibitisha UNDUMILA KUWILI WA KIPANDE ambaye kauli zake mara zote anazojifagilia kwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari na wananchi walipa kodi kuwa yeye ni mtu safi wakati ukweli ni kwamba FIKRA NA VITENDO VYAKE muda wote vinalenga kumnufaisha yeye binafsi na wanaomlinda.

SIO SIRI Madeni Kipande anafahamika kuwa ni mla rushwa MZOEFU wa kupindukia toka huko alikotoka Wizara ya Ujenzi.

Akiwa Ujenzi alikuwa akilazimisha wateja au mtu yeyote aliyekuwa anahitaji huduma anayosimamia yeye kutoa rushwa. Hii imeendelea kujidhihirisha wazi wazi akiwa huko bandarini kama ambavyo tumekuwa tukiwajulisha na pia tutaendelea kuwajuza mikakati yake hiyo ya kula rushwa hadi wazalendo wa nchi hii tuzinduke.

Kipande anakula rushwa bila woga mbali na kupokea kitita cha zaidi ya shilingi milioni 26.0 kwa mwezi kwa ajili ya mshahara (16m) na marupurupu kibao!.
 
Back
Top Bottom