Misri na Ethiopia zipo katika hati hati ya kuingia vitani juu ya bwawa la kufua umeme linalojengwa na Ethiopia

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
35,845
40,433
Bwawa la Grand Renaissance Dam ambalo limekuwa likijengwa nchini Ethiopia kwa zaidi ya miaka 10 sasa linatajwa kuwa ndio litakuwa kubwa kabisa Afrika kwa sasa.

Bwawa hili limefikia hatua ya ujazaji maji, na Misri analalamika kwamba kiwango cha maji ya mto Nile yanayowafikia kitapungua na hivyo kuhatarisha maisha yao, na aametishia kuingia vitani dhidi ya Ethiopia juu ya suala hilo.

Pamoja na vitisho hivyo, Ethiopia wamedai wako tayari kupambana hadi tone la mwisho la damu ya Ethiopia litakapomwagika, ndio watakubali kusitisha mradi.

Leo anatokea mtu mmoja atuambie miradi ya ufuaji umeme kwa kutumia mabwawa ya maji umepitwa na wakati, halafu mnataka tumchekee?
Video ina maelezo ya ziada

 
HEP is outdated in the modern world hata huu wa kwetu hauna tija ni suala la muda tuuu !! Hata uwanja wa ndege chato mliudifia hiv hivi hata zole ndege mlipiga mayowe na kuandamana mpaka eapot leo vipi!??? Miradi ya jiwe ni faken yote
 
Warabu watawaweza wale wahabeshi ndugu na wasomali.Ujue etheopia hawana cha kupoteza, wahabeshi ndio mafarao wa kale hawa warabu wanajifanya hawajui eti! Ngoja tuone,wao wagombane sie tutawauzia mahindi na mpunga.
Turejee kitabu kinachouywa "the great pond" by chinua achebe kama sijasahu.
 
Ethiopia atasimama.na wengi maana Misri anataka kujimilikisha mto nile kimabavu..hiv Tz tukiamua kuanzisha kilimo kikubwa cha umwagiliaji Shinyanga Geita na Tabora kiasi cha kuounguza kabisa maji yanayoelekea Misri na sisi tutavamiwa?
 
Ethiopia atasimama na wengi maana Misri anataka kujimilikisha mto nile kimabavu..hiv Tz tukiamua kuanzisha kilimo kikubwa cha umwagiliaji Shinyanga Geita na Tabora kiasi cha kuounguza kabisa maji yanayoelekea Misri na sisi tutavamiwa?
 
MISRI ni wajinga sana, umpige Ethiopia kabisa, israel atakuwa amelala usingizi? wanataka kusababisha mzozo usio na umuhimu. mtu maji yanatoka kwako wewe uliyeko c hini unataka kuleta kibesi, wakiweka sumu si utakunywa sumu? kwa gharama waliyotumia ethiopia kujenga anafikiri akipiga mabom kulibomoa kidonda hicho ethiopia atakubali kukaa kimya? hata kama wanayo madege na maguvu lakini hata tembo kuna wakati huwa anakamatika na chura (anapoingia kwenye pua lake lile) na tembo hujingongesha mwenyewe hadi kufa. ethiopia ni wadogo ila sio wa kubeza na lazima walipokuwa wanajenga walijandaa kwa jambo hili. sio wajinga.
 
MISRI ni wajinga sana, umpige Ethiopia kabisa, israel atakuwa amelala usingizi? wanataka kusababisha mzozo usio na umuhimu. mtu maji yanatoka kwako wewe uliyeko c hini unataka kuleta kibesi, wakiweka sumu si utakunywa sumu? kwa gharama waliyotumia ethiopia kujenga anafikiri akipiga mabom kulibomoa kidonda hicho ethiopia atakubali kukaa kimya? hata kama wanayo madege na maguvu lakini hata tembo kuna wakati huwa anakamatika na chura (anapoingia kwenye pua lake lile) na tembo hujingongesha mwenyewe hadi kufa. ethiopia ni wadogo ila sio wa kubeza na lazima walipokuwa wanajenga walijandaa kwa jambo hili. sio wajinga.
Kwakweli, yaani watu wamejibana kimkanda mkanda kwa miaka 10 tena kwa pesa za ndani kujenga bwawa, halafu uje tu kupiga bomu kirahisi rahisi tu? Mbona hilo bwawa litajazwa kwa damu za waMisri badala ya maji
 
Wamisri wabinafsi sana hata TZ ilipotaka kuchukua Maji Ziwa Victoria walijifanya Hawataki. Uzuri haya maji sio ya nchi moja atavutana na ethiopia lakini ataachia mwisho wa siku na Bwawa litajengwa tuu...!
 
Bado sijapata picha hii vita itakuwa ya namna gani,? watarushiana missel au watatumia ndege za kivita. Ama itabidi majeshi ya misri yavuke nchi ya sudan kask yaingie kuipiga Ethiopia vita ya ardhin
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom