Misri: Msanii wa kike aliyeonekana kwenye video ‘akila ndizi kwa mbwembwe’ akamatwa na polisi

Rosh Hashannah

JF-Expert Member
Sep 13, 2017
3,415
2,042
Screen-Shot-2017-11-21-at-14.52.17.png
Screen-Shot-2017-11-21-at-14.52.17.png
Msanii wa kike wa muziki wa Pop nchini Misri ajulikanaye kwa jina la, Shyma amejikuta mikononi mwa polisi Jumamosi ya wikiendi iliyopita baada ya kuachia video ya wimbo wake mpya ujulikanao kwa jina la ‘ I have Issues’ kwa kosa la kuonekana akila tunda aina ya ndizi kwenye video hiyo kwa mbwembwe mbele ya wanaume.


Moja ya kipande cha video hiyo kikimuonesha Shyma akila ndizi.

Mrembo huyo kwenye video hiyo ambayo ilipata views milioni 1.2 ndani ya masaa 14 kwenye mtandao wa YouTube alionekana akila ndizi kwa mbwembwe mbele ya wanafunzi wake huku akichora namba ‘#69’ ubaoni kitu ambacho kiliamsha hisia kali kwa wanaume nchini Misri.



Polisi wamesema wanamshikilia kwa kosa la kukiuka maadili ya dini ya kiislamu na tamaduni za nchi ya Misri huku wakidai kutaka kumuhoji kujua zaidi alimaanisha nini kufanya hivyo kwenye video hiyo.

Shyma ambaye jina lake kamili ni Shaimaa Ahmed baada ya kuona anashambuliwa na mashabiki wake mtandaoni aliamua kutolea maelezo kupitia ukurasa wake wa Facebook akieleza kuwa hakuwa na wazo kama watu walivyofikiria na kuomba radhi.



Leo Jumatano Polisi mjini Cairo wamesema watatoa taarifa rasmi baada ya kufanya nae mahojiano kwa siku mbili mfululizo (Jumatatu na Jumanne).

Mwaka 2015 Densa mmoja nchini humo alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela na faini kwa kosa la kucheza akiwa amevaa nguo fupi huku akikatika viuno kwenye sakafu.

Tayari video hiyo imeshatolewa kwenye mtandao wa YouTube lakini hapa chini unaweza ukaangalia baadhi ya vipande ambavyo vimemuweka rumande msanii huyo kama vilivyofanyiwa uchambuzi na Waandishi wa Habari.
 
nimeona Kipande cha huo wimbo ..... soma hapa .....................

sijafuatilia sheria za Nchi ya Misri lakin na fahamu ni nchi inayofuata misingi ya sheria za kiislamu ,,, yamkini ndio maana wameifungia lakin sion sababu ya kuifungia kaz ya msanii huyo pamoja na kumweka kizuizin maana yeye n celebrity anafanya kile anachohisi kinawapendeza mmafanc wake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom