Omari Frank
Member
- Jul 22, 2022
- 14
- 4
Mada Kuu: MISINGI YA UKUAJI KIUCHUMI KWA MTAZAMO NA UZOEFU WANGU.
Nimefurahi kupata nafasi ya kueleza jambo kuhusu uchumi kwasababu binafsi nimejikita katika shughuli za kiuchumi kwa muda mrefu hivyo basi ninaweza kuwa na jambo la kusema kwa wadau wa maendeleo na wanajamii Forums.
Kimsingi maendeleo ya kiuchumi huanza na mtazamo aliokuwa nao mtu kichwani mwake, uwezo wa kuona, kuvumbua au kutengeneza fursa, uthubutu na nidhamu.
Kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja ndio msingi haswa wa kukua kwa uchumi wa Taifa zima. Tukianza kuangalia ni namna gani sasa mtu anaweza kukuza uchumi wake basi tutaangalia mambo yafuatayo:-
MFANO: Saluni ya kike unaweza ukaanza kwa kusuka kibarazani tu nje ya nyumba unayoishi, Shule ya malezi ya watoto chini ya umri wa miaka mitano pia unaweza ukaanzisha chini ya mti, kwenye kibaraza cha nyumba au Frame kubwa. Hiyo ni mifano tu ambayo inaonesha kwamba unaweza ukawa hauna mtaji lakini bado ukaanza biashara hata kwa kuunga unga kabisa na inawezekana.
MFANO HALISI
Mimi ni mwalimu lakini pia ninamiliki biashara ndogo ndogo za vyakula yaani mabanda ya chipsi pamoja na mama ntilie, Sabasaba na Mawenzi mkoani Morogoro.
Niliiona fursa ya biashara za vyakula katika maeneo hayo ambapo ndipo ninapoishi, licha ya kwamba wapo wengine lakini na mimi nikaja na ubunifu wangu ambao kwa kuzingatia mambo niliyoeleza hapo juu leo hii kwa mwezi ninafunga kiasi ambacho pengine nikisema hapa kila mtu atasema nadanganya.
Na bado nina malengo ya kuendelea kufungua biashara nyingi katika maeneo mengi zaidi ili niendelee kukuza uchumi wangu binafsi na taifa kwa ujumla. Nina mpango wa kuanza kulima mpunga, mahindi na kilimo cha mboga mboga ili vyote viwe vinatumika katika mabanda yangu.
Hakuna lisilowezekana, changamoto ni nyingi sana ikiwemo kukosa mitaji na elimu na ujuzi juu ya shughuli za kiuchumi kama ufugaji lakini penye nia pana njia, unaweza kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kama vile Vocha, Soda na Bia, n.k kisha ukakusanya pesa zako na kuanza kidogo kidogo kwasababu wafanya biashara wengi tunaanza hivyo.
Niishukuru JamiiForums kwa kutoa fursa hii, licha ya kwamba kuna kitita kinashindaniwa lakini naamini kwa sehemu kubwa sana kuna elimu itasambaa na kuwafikia watu wengi juu ya mambo haya ya maendeleo.
Nimefurahi kupata nafasi ya kueleza jambo kuhusu uchumi kwasababu binafsi nimejikita katika shughuli za kiuchumi kwa muda mrefu hivyo basi ninaweza kuwa na jambo la kusema kwa wadau wa maendeleo na wanajamii Forums.
Kimsingi maendeleo ya kiuchumi huanza na mtazamo aliokuwa nao mtu kichwani mwake, uwezo wa kuona, kuvumbua au kutengeneza fursa, uthubutu na nidhamu.
Kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja ndio msingi haswa wa kukua kwa uchumi wa Taifa zima. Tukianza kuangalia ni namna gani sasa mtu anaweza kukuza uchumi wake basi tutaangalia mambo yafuatayo:-
- MTAZAMO
- TENGENEZA FURSA
MFANO: Saluni ya kike unaweza ukaanza kwa kusuka kibarazani tu nje ya nyumba unayoishi, Shule ya malezi ya watoto chini ya umri wa miaka mitano pia unaweza ukaanzisha chini ya mti, kwenye kibaraza cha nyumba au Frame kubwa. Hiyo ni mifano tu ambayo inaonesha kwamba unaweza ukawa hauna mtaji lakini bado ukaanza biashara hata kwa kuunga unga kabisa na inawezekana.
- UTHUBUTU
- NIDHAMU
MFANO HALISI
Mimi ni mwalimu lakini pia ninamiliki biashara ndogo ndogo za vyakula yaani mabanda ya chipsi pamoja na mama ntilie, Sabasaba na Mawenzi mkoani Morogoro.
Niliiona fursa ya biashara za vyakula katika maeneo hayo ambapo ndipo ninapoishi, licha ya kwamba wapo wengine lakini na mimi nikaja na ubunifu wangu ambao kwa kuzingatia mambo niliyoeleza hapo juu leo hii kwa mwezi ninafunga kiasi ambacho pengine nikisema hapa kila mtu atasema nadanganya.
Na bado nina malengo ya kuendelea kufungua biashara nyingi katika maeneo mengi zaidi ili niendelee kukuza uchumi wangu binafsi na taifa kwa ujumla. Nina mpango wa kuanza kulima mpunga, mahindi na kilimo cha mboga mboga ili vyote viwe vinatumika katika mabanda yangu.
Hakuna lisilowezekana, changamoto ni nyingi sana ikiwemo kukosa mitaji na elimu na ujuzi juu ya shughuli za kiuchumi kama ufugaji lakini penye nia pana njia, unaweza kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kama vile Vocha, Soda na Bia, n.k kisha ukakusanya pesa zako na kuanza kidogo kidogo kwasababu wafanya biashara wengi tunaanza hivyo.
Niishukuru JamiiForums kwa kutoa fursa hii, licha ya kwamba kuna kitita kinashindaniwa lakini naamini kwa sehemu kubwa sana kuna elimu itasambaa na kuwafikia watu wengi juu ya mambo haya ya maendeleo.
Upvote
1