Misingi ya Chadema na Cuf imevifanya iwe rahisi kubomoka!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,598
141,415
Ukiondoa CCM na Nccr mageuzi ambavyo vimejengwa katika msingi wa umoja wa kitaifa, vyama vingine vyote vimejengwa katika misingi ya maeneo nk...nk. Na hii ilisababishwa na ukweli kwamba vyama kama Chadema na Cuf baada tu ya kuanzishwa vilikuwa vinajitahidi kuimarika haraka ili vishiriki uchaguzi wa 1995. Matokeo yake wakajikuta wanawekeza nguvu kubwa kwenye maeneo wanayojulikana na hasa ya nyumbani na hata baada ya uchaguzi wakashindwa kujiongeza hivyo vyama vikaonekana ni vya maeneo. Utakumbuka hata UDP kilikuwa cha usukumani, TLP uchagani/wahaya, NRA iliegemea udini pamoja na ukweli kwamba vyama hivi vilikuwa na nguvu katika maeneo fulani lakini vilibomolewa kirahisi sana. Na hata ACT wazalendo wanabomoka haraka kwa sababu hiyo hiyo. Ni wakati sasa viongozi wa vyama hivi vikubwa vya upinzani wakajiadjust kwa haraka ili viwe vya kitaifa kweli vinginevyo vitafutika kwenye ramani. Si kwamba wabunge wananunuliwa NO bali wanakwenda sehemu wanayohisi watakuwa salama. Wabunge kama Cecil Mwambe wa ndanda au Easter Bulaya wa Bunda hawa hawahitaji kununuliwa bali kuambiwa tu " karibuni tena nyumbani " basi kwa moyo mkunjufu wanarejea kwani walitoka CCM baada ya hila tu za watu binafsi na hii ya sasa ni CCM mpya. Cuf na Chadema bado hamjachelewa na taifa bado linahitaji upinzani, lakini ule makini na wenye tija vinginevyo pale mjengoni mtabakia na wabunge kutoka Pemba, Moshi - Arusha, na yule wa Ujiji. Nawasilisha!
 
Ukiondoa CCM na Nccr mageuzi ambavyo vimejengwa katika msingi wa umoja wa kitaifa, vyama vingine vyote vimejengwa katika misingi ya maeneo nk...nk. Na hii ilisababishwa na ukweli kwamba vyama kama Chadema na Cuf baada tu ya kuanzishwa vilikuwa vinajitahidi kuimarika haraka ili vishiriki uchaguzi wa 1995. Matokeo yake wakajikuta wanawekeza nguvu kubwa kwenye maeneo wanayojulikana na hasa ya nyumbani na hata baada ya uchaguzi wakashindwa kujiongeza hivyo vyama vikaonekana ni vya maeneo. Utakumbuka hata UDP kilikuwa cha usukumani, TLP uchagani/wahaya, NRA iliegemea udini pamoja na ukweli kwamba vyama hivi vilikuwa na nguvu katika maeneo fulani lakini vilibomolewa kirahisi sana. Na hata ACT wazalendo wanabomoka haraka kwa sababu hiyo hiyo. Ni wakati sasa viongozi wa vyama hivi vikubwa vya upinzani wakajiadjust kwa haraka ili viwe vya kitaifa kweli vinginevyo vitafutika kwenye ramani. Si kwamba wabunge wananunuliwa NO bali wanakwenda sehemu wanayohisi watakuwa salama. Wabunge kama Cecil Mwambe wa ndanda au Easter Bulaya wa Bunda hawa hawahitaji kununuliwa bali kuambiwa tu " karibuni tena nyumbani " basi kwa moyo mkunjufu wanarejea kwani walitoka CCM baada ya hila tu za watu binafsi na hii ya sasa ni CCM mpya. Cuf na Chadema bado hamjachelewa na taifa bado linahitaji upinzani, lakini ule makini na wenye tija vinginevyo pale mjengoni mtabakia na wabunge kutoka Pemba, Moshi - Arusha, na yule wa Ujiji. Nawasilisha!
Mkuu uko sahihi chadema na cuf ni vyama vya wafanyabiashara wa kichaga na kipemba.Baada ya kuona wachaga na wapemba wameshika biashara Tanzania wakajiunga kwenye kitu kinaitwa UKAWA ili washike nchi waipore mikononi mwa wakulima na wafanyakazi .Cuf chama cha wafanyabiashara wa kipemba na chadema chama cha wafanya biashara wa kichaga.ni vya ukanda na wafanyabiashara
 
Mkuu uko sahihi chadema na cut ni vyama vya wafanyabiashara wa kichaga na kipemba.Baada ya kuona wachaga na wapemba wameshika biashara Tanzania wakajiunga kwenye kitu kinaitwa UKAWA ili washike nchi waipore mikononi mwa wakulima na wafanyakazi .Cuf chama cha wafanyabiashara wa kipemba na chadema chama cha wafanya biashara wa kichaga.ni vya ukanda na wafanyabiashara
Porojo za kwenye kijiwe cha kusubiri bk 7. Zinawasaidia kuhama na kivuli.
 
Acha upuuzi, CCM mnategemea dola. Over
Wafanyabiashara wa kipemba wa Zanzibar waliunda CUF na wafanyabiashara wa Tanzania bara wa kichaga waliunda chadema. Over.Baadaye wakaungana kuunda UKAWA
 
Kama misingi yake sio imara ruhusuni tume huru,kama hamtanyolewa nywele bila maji
 
Kama misingi yake sio imara ruhusuni tume huru,kama hamtanyolewa nywele bila maji
Tume huru IPO ndio maana wapinzani akina Mbowe,Godless Lema,Msigwa ,Sugu.Na mameya akina Mwita nk walishinda
 
Maelezo marefu yasiyo na chembe ya ukweli zaidi ya propaganda mfu. Ukweli ni huu, mwenyekiti wa sasa wa ccm hana uwezo wa siasa za ushindani kwani anapenda kusifiwa na kunyenyekewa. Ukiangalia sifa hizo hawezi kuzipata ndani ya Cdm wala cuf asilia labda cuf academia ya lipumba. Sasa kwa kutumia nafasi yake amiri jeshi mkuu, anatumia njia za kikatili, kuhonga na kuzuia vyama hivyo kushindwa kufanya siasa.

Katika mazingira haya ni wapinzani wachache wanaweza kuhimili. Nani atamudu kufanya siasa ya upinzani ambapo ukipinga ama kukosoa bila woga unaweza kupigwa risasi na hatua zisichukuliwe. Ili kuwaonyesha tumewapuuza tutahimiza wanaounga mkono upinzani wa kweli wasigombee au kupiga kura ili ccm mbaki mnashindana wenyewe kikabila na kikanda. Hatuwezi kuendekeza siasa za kipuuzi.
 
Huyu YEHODAYA na wadau fulani wa CHADEMA wakati fulani huwa wanaweka comment za kuudhi inabidi ucheke tu.

Unajiuliza huyu jamaa huwa anawaza vitu gani kichwani? Atanaka awatibue tu makada wanywa maji ya bendera ma-bavicha na ma-uvccm.
 
Tume huru IPO ndio maana wapinzani akina Mbowe,Godless Lema,Msigwa ,Sugu.Na mameya akina Mwita nk walishinda

Walishinda kabla hizi siasa za kipuuzi za kupigana risasi na kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano yake haijaingizwa nchini. Hatutopiga kura tena kuanzia sasa, mtabaki wanaccm wenyewe mkishindana kikabila na kikanda.
 
Walishinda kabla hizi siasa za kipuuzi za kupigana risasi na kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano yake haijaingizwa nchini. Hatutopiga kura tena kuanzia sasa, mtabaki wanaccm wenyewe mkishindana kikabila na kikanda.
Mmmmmmmmmm
 
Walishinda kabla hizi siasa za kipuuzi za kupigana risasi na kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano yake haijaingizwa nchini. Hatutopiga kura tena kuanzia sasa, mtabaki wanaccm wenyewe mkishindana kikabila na kikanda.
Kikwete kawa mwema ghafla washenzil nyie si mlimporomoshea matusi kuwa ni dhaifu anacheka Cheka tu na ni Vasco da gama kazi yake kusafiri tu kila siku kwa kuwa kuwa huwa anakula miguu ya kuku ndio maana hatuliii kutwa safari? Kikwete alivyowaambia mtanikumbuka mitandaoni mkajibu kuwa kwenda zako akukumbuke nani ishia mumesahau? CCM ilisikia kilio chenu ikawapa MTU asiyecheka wala kusafiri mnabweka nini mbwa nyie
 
Kikwete kawa mwema ghafla washenzibl nyie si mlimporomoshea matusi kuwa ni dhaifu anacheka Cheka tu na na ni Vasco da gama kazi yake kusafiri tu kila siku kuwa huwa anakula miguu ya kuku ndio maana hatuliii kutwa safari? Kikwete alivyowaambia mtanikumbuka mitandaoni mkajibu kuwa kwenda zako akukumbuke nani ishia mumesahau? CCM ilisikia kilio chenu ikawapa MTU asiyecheka wala kusafiri mnabweka nini mbwa nyie

Wapi nimemsifia JK kuwa alukuwa mwema na kuna sehemu yoyote nimeonyesha kumkumbuka? JK alikuwa akisafiri sana safari zenye tija na zisizo na tija. Je kuna aliyekosea kwa kuhoji safari zenye tija na zisizo na tija? Kikwete sio wa kwanza kusema tutamkumbuka kwani kila aliyemaliza muda wake aliyatumia maneno hayo.

Acha hoja za mkumbo, mimi nina mtazamo wangu na nikiamua kumchambua Magufuli v/s Kikwete wote nitakupa mazuri na mabaya yao. Haya mambo ya hoja za mkumbo kwamba wote waliomkosoaJK ndio haohao wanaomkosoa Magufuli na kumsifu JK hapo unachemsha.

Kwangu JK alikuwa rais aliyesimamia nchi kizembe lakini alijali demokrasia kwa kiasi chake. Magufuli ni rais asiyejali demokrasia lakini anayeweza kusimamia baadhi ya mambo kwa umadhubuti. Sasa usinijie na lugha za mkumbuko huku umepanick wote na mazuri na mapungufu yao. Sasa kunijia na hoja muflisi kwamba udhaifu wa JK kuwa ni ubora wa Magufuli ni kuniona sijui kipi ni kipi dogo.
 
John kuna ukweli kidogo kwenye maandishi yako, ingawa kimsingi tatizo hilo lipo lakini si kwa viwango sawa katika baadhi ya vyama.

Upinzani unapaswa kujitathmini na kujijenga upya maana mazingira na mbinu za vita pia zimebadilika. Kiutendaji visiwe vyama vya maofisini au nyakati za uchaguzi tu bali wajikite vijijini na wawe na sera endelevu, wajitahidi sana kwenye kujenge uwezo na mtandao kuanzia CHINI sio juu, wawe na mbinu za kutenda ili wajulikane na kuaminiwa na wengi huko vijijini.
 
Back
Top Bottom