Siri Sirini
JF-Expert Member
- Mar 12, 2012
- 547
- 198
Kuna gazeti nimesoma yani nimeishia kucheka tu, lakini ni vinatokea kwenye jamii yetu, ni kuhusu watu waendavyo misibani, mana watu wanaenda kuonyeshana nguo, magari ya kifahari, mitindo ya nywele na jinsi ya kupaka vipodozi.
Palipo nichekesha
wengine mavazi wanayokuja nayo msibani hayana heshima, akidondosha kitu mtihani kuokota, achilia mbali viatu alivyovaa kama ngongoti anayesubiliwa kupigiwa makofi na watoto wanaomtizama, mradi atizamwe msiba mzima. Vipodozi vinavyopakwa usoni hata wengine kulia hawawezi, nyuso zimewakakamaa, mikope mirefu kama mijinamizi, huo wanja kama amefukuzwa kwenye fumanizi, mwingine hata mtandio wa kujitanda hana, mradi aonyeshe style yake ya nywele, ukija kwa wakaka, kutwa kaning'iniza funguo ya gari mkononi, suti kali hata kama kuna jua kali gani, cm ipo sikioni mda wote, mradi muione.
Jamani wapi tunaelekea? Tunawaiga wenzentu? Maana wao hata kulia cdhani kama wanalia, na kuvaa vimini kawaida yao,
dah! Nimechoka, ni hayo tu wana cc
Palipo nichekesha
wengine mavazi wanayokuja nayo msibani hayana heshima, akidondosha kitu mtihani kuokota, achilia mbali viatu alivyovaa kama ngongoti anayesubiliwa kupigiwa makofi na watoto wanaomtizama, mradi atizamwe msiba mzima. Vipodozi vinavyopakwa usoni hata wengine kulia hawawezi, nyuso zimewakakamaa, mikope mirefu kama mijinamizi, huo wanja kama amefukuzwa kwenye fumanizi, mwingine hata mtandio wa kujitanda hana, mradi aonyeshe style yake ya nywele, ukija kwa wakaka, kutwa kaning'iniza funguo ya gari mkononi, suti kali hata kama kuna jua kali gani, cm ipo sikioni mda wote, mradi muione.
Jamani wapi tunaelekea? Tunawaiga wenzentu? Maana wao hata kulia cdhani kama wanalia, na kuvaa vimini kawaida yao,
dah! Nimechoka, ni hayo tu wana cc