Mishahara ya walimu kukatwa madawati yakiharibika

shonkoso

JF-Expert Member
Mar 13, 2015
590
1,205
13669176_1307187512632485_7899101742728112322_n.jpg

Rais Magufuli pia aliwaagiza wakurugenzi hao kuwakata mishahara walimu ambao madawati katika shule yatavunjwa.

“Mkahakikishe shule zote katika halmashauri zenu zinakuwa na madawati na mtengeneze orodha, endapo madawati yataharibiwa au kuvunjwa yule mwalimu husika akatwe mshahara,” alisema.

Alisema kuna wakurugenzi wamekuwa wakiingia mikataba na wafanyabiashara wanaowafahamu huku wakitoa tenda kushinda zabuni.

Aliwataka wakurugenzi hao kupinga kodi za ajabu wanazolipishwa wananchi wa maisha ya chini.

“Kumekuwa na kodi na kero za ajabu ajabu, mkapinge hizo kodi ndogondogo; utakuta kina mama wauza mchicha wamepanga barabarani nao wanalipishwa kodi, wakati analima na kumwagilia hukumsaidia mbolea wala maji… ninawaomba mkazuie hizo kodi,” alisema.

Chanzo: Mtanzania
 
Kwa hiyo wanafunzi wa darasa ambalo hawampendi mwalimu wao kwa vile ni mkali kusimamia nidhamu wataharibu madawati ajikute analipa kwa mshahara mpaka akome na wao waendelee na upuuzi wao.
Hata mie ningepewa cheo hicho siwezi kutamka hilo agizo
 
udikteta wakati mwingine unaleta maendeleo kwa kasi.


pia umesahau hujenga chuki kubwa sana na matabaka miongoni mwa jamii kuna wale wa kujipendekeza unapo mfurahisha dikteta hachelew kukutunuku cheo kwani hao wanafunz wamezaliwa na hao walimu? Ustaarabu wa watoto huanzia ktk familia zao.
 
Back
Top Bottom