Mishahara ya wabunge, mawaziri na majaji juu!

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Feb 18, 2009
3,930
4,893
Mishahara ya wabunge,mawaziri na majaji imepandisha huku wa spika wa bunge ukipanda mara dufu.
Kwa kifupi tu;

Spika na Jaji mkuu Tshs 2,760,000/= mpaka 4,850,000/=
Naibu spika Tshs 2,080,000/= mpaka 2,172,000/=
Mbunge Tshs 1,840,000/= Mpaka 1,921,000/=
jaji wa mahaka kuu tshs 2,160,000/= mpaka 3,645,000/=
jaji Mahakam ya rufaa Tshs 2,310,000 mpaka 4,250,000/=

Wakuu ninchoomba kuelewesha inamaana kwa kuwa spika ni mbunge kwa hiyo anakula na mishahara mingine ya ubunge au?

Kwa hali hii kweli tutapona?
Source:Mwananchi news paper la leo
 
Hii serikali hata siielewi kabisa hivi hizi taarifa zinapomfikia mhangaikaji, mkulima inamtia majonzi na uchungu kiasi gani? We need a change.......
 
MSHAHARA WA SPIKA, JAJI MKUU WAONGEZWA MARADUFU

Waandishi Wetu

SERIKALI imewaongezea mishahara viongozi wa kisiasa, majaji, wakuu wa mikoa na wilaya kuanzia Julai mwaka huu, huku jaji mkuu na spika wakiongezewa maradufu.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa mshahara wa jaji mkuu na spika, ambao ni viongozi wa mihimili mikuu miwili ya nchi, umepanda kutoka Sh2,760,000 hadi Sh4,850,000 kuanzia mwezi Julai na ongezeko hilo ni sawa na asilimia 75.7

Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na vyanzo mbalimbali vya habari kutoka mihimili yote ya dola, mshahara wa naibu spika umepanda kwa Sh92,000, kutoka Sh2,080,000 hadi Sh2,172,000 na mbunge kutoka Sh1,840,000 hadi Sh1,921,000, ikiwa ni ongezeko la Sh81,000 kwa mwezi.

Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilillah aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki kuwa amesikia kuhusu nyongeza hiyo ya mishahara, lakini hana taarifa rasmi wala namna yoyote ya kuthibitisha, kwa kuwa mishahara hiyo haimuhusu.

"Viwango vya mishahara kwa viongozi wa serikali vinawekwa na serikali, mimi hainihusu hivyo siwezi kuthibitisha hilo. Nimesikia tu kama mlivyosikia ninyi," alisema Dk Kashilillah alipotakiwa na gazeti hili kuthibitisha ongezeko la mishahara ya wabunge.

Katika viwango hivyo vipya vya mishahara ambavyo Mwananchi imefanikiwa kuviona, jaji wa Mahakama Kuu ameongezewa mshahara kutoka Sh2,160,000 hadi Sh3,645,000, ikiwa ni ongezeko la Sh1,485,000 huku jaji wa Mahakama ya Rufaa ameongezewa Sh1,940,000 (kutoka Sh2,310,000 hadi Sh4,250,000).

Vyanzo vimeeleza kuwa mshahara wa waziri umepanda kwa Sh102,000 (kutoka Sh2,320,000 hadi Sh2,422,000) na mshahara wa naibu waziri umepanda kutoka Sh1,960,000 hadi Sh2,046,000, ikiwa ni ongezeko la Sh120,000.

Mkuu wa mkoa, ambaye anapata mshahara wa Sh2,172,000, sasa atalipwa Sh2,080,000 na mkuu wa wilaya amepandishiwa mshahara wake kutoka Sh1,840,000 hadi Sh1,921,000 kwa mwezi.

Vyanzo hivyo vya habari vimedokeza kuwa viwango hivyo vipya vya mishahara, havijumuishi posho za vikao, mafuta ya gari na fedha za kujikimu.

Habari zinaeleza kuwa jaji mkuu anapata posho ya madaraka ya Sh6 milioni kwa mwaka na jaji kiongozi anapata posho ya Sh3 milioni, kwa mujibu wa viwango hivyo vipya.

Majaji 70 wanapata posho ya simu na umeme inayofikia Sh 386,400,000 kwa mwaka na posho ya mavazi ya Sh35 milioni kila mmoja.

Habari zinadokeza kuwa majaji 70 wametengewa lita 100 za mafuta ya gari kwa juma, lita moja imekadiriwa kugharimu Sh1,500 hivyo kupewa Sh600,000 kwa wiki ambayo ni sawa na Sh504 milioni kwa mwaka.

Moja ya vyanzo vyetu vya habari kilidokeza kuwa nyongeza hiyo ni ya kawaida ambayo inaenda sambamba na nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma, ingawa mwaka huu kwake imeonekana kuwa kubwa zaidi.

"Hili ni kweli; mishahara yetu imeongezwa kuanzia Julai, lakini sisi tulidhani ni nyongeza ya kawaida inayoenda sambamba na nyongeza ya mishahara ya watumishi wengine wa umma, lakini ukweli mambo ni mazuri zaidi," alisema.

Akiwasilisha hotuba yake kwa mwaka 2000/2010, waziri wa Nchi, ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma, Hawa Ghasia alisema serikali inatarajia kutumia Sh1,774 trilioni kugharamia mishahara kwa watumishi wa umma,

Fedha hizo pia zitatumika kulipa mishahara kwa watumishi waliopo kazini, ajira mpya, upandishaji vyeo watumishi, kulipia madai ya malimbikizo na mapunjo ya mishahara ya watumishi wa umma nchini.

"Serikali itaendelea kuhakikisha watumishi wake wanapandishwa vyeo na kurekebishiwa mishahara yao ipasavyo," alisema Waziri Ghasia wakati akiwasilisha makadirio ya wizara ambayo wabunge waliyapitisha bila marekebisho.

Suala la mishahara hiyo mipya limekuwa siri kubwa hasa ikizingatiwa kuwa wakati wa bajeti ya serikali ya mwaka huu, waziri mwenye dhamana hakuweka bayana viwango vipya vya mishahara ya watumishi wa umma.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zilisema kuwa serikali hivi sasa iko katika mkakati muhimu wa kuboresha maslahi ya watumishi wa umma wenye taalumu ili kuzima wimbi la wasomi kukimbilia nyadhifa za kisiasa.

"Katika miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia madaktari na wanataaluma wengine wanaacha taaluma zao wanakimbilia ubunge kwa sababu anaona labda atateuliwa kuwa waziri na maslahi ni mazuri,¡"kilidokeza chanzo chetu cha habari.

Source: Mwananchi Date:8/25/2009
 
Hili ndilo changa la macho la Ari mpya kasi mpya na nguvu mpya kwa wadanganyika. Wengi walipe kodi wachache wafaidi matunda ya Uhuru. Unyonjaji wa mtandao wa SISIEM na maisha bora kwa wote. Silaha ya iliyobaki kwa wanyonge ni kuikataa SISIEM mwakani.
 
Ofisa wa serikali mwenye masters anaanza kazi na TGSD 3 ambayo gross is less than 450,000/= net around 300,000/= halafu eti uniambie asipokee rushwa na kula dili za juju kwa juu!!! Hata kama kuna allowance na vikao but haitoshi kwa maisha ya gharama ya leo!!!!
 
Inauma sana mwalimu wa sec. mwenye Diploma anakula take home 170,000/= kwa mwezi hapo ana mke na watoto na ndugu wanamtegemea.
 
Inauma sana mwalimu wa sec. mwenye Diploma anakula take home 170,000/= kwa mwezi hapo ana mke na watoto na ndugu wanamtegemea.

mkuu kumbe wakuu wa mikoa na wilaya nao wamo!!.

Mkuu wa mkoa, ambaye anapata mshahara wa Sh2,172,000, sasa atalipwa Sh2,080,000 na mkuu wa wilaya amepandishiwa mshahara wake kutoka Sh1,840,000 hadi Sh1,921,000 kwa mwezi.
source
 
Mkuu hizo za hao walafi bado posho na malupu lupu na vikao visivyo vya lazima nimesahau na safari.
 
Inauma sana mwalimu wa sec. mwenye Diploma anakula take home 170,000/= kwa mwezi hapo ana mke na watoto na ndugu wanamtegemea.
Tena saaaaana. 170,000/= hiyo hiyo ale yeye mke na watoto, usafiri hiyo hiyo. Kweli tutafika namna hii? Wenyewe sasa wanapata mshahara milioni 4 halafu wanapewa lita 100 za mafuta ya magari yao kwa wiki n.k. Sisi wa chini ambao hata laki moja tu hatuifahamu sijui tutafika wapi?

Ngoja nianze kulia kama dakika mbili hivi. uwi, uwi, eeeh, eeeeeeeeeeeh. uuuuuh.
 
Jiulize mzee ana miaka 75 analipwa Tshs169,000/= fidia ya nyumba ilobomoka.
Je,atajenga nini na hiyo hela?
Kwanini hiyo mishahara wasikatw hawa jamaa wakajengewa tujumba kama tule twa magomeni kota ama ilala kota??

Kweli kazi ipo,...
 
Mh!! Sijui kama tutafika......Hao wabunge wanaoenda kupamba ufisadi kweli walipwe mahela yote hayo? Kazi ipo.
 
Where is justice and fairness ktk kutumia national cake??

Kwanini wanasiasa tu wafaidi hii cake??

Kwani ni dhambi kuamua kuwa mwal. katika shule za umma Tanzania??

Halafu basi usiambiwe: mishahara ya wenzetu visiwani ndo iko chini..yaani balaa!!
 
Hesabu tatizo la kitaifa au wamepunguziwa mshahara?.

1. Kama wamepunguziwa mishahara basi ingekuwa safi tu!

2. Hivi vyeo vya wakuu wa Wilaya bora tu vifutwe..hizi kazi wakurugenzi kule wilayani wanatosha..na hii pesa waongezewe waalimu!
 
Kama hiyo ndio mishahara yao KWELI ni midogo sana. Hebu jaribu kuulizia mishahara ya wafuatao uone ninalojaribu kulieleza hapa;
1. Gavana wa BOT,CAG
2. Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,
3. Maafisa Watendaji Wakuu wa DAWASA, DAWASCO, EWURA, REA, SUMATRA, TCRA
4.Mkurugenzi wa TIC, PSRC
5. Uje pia kwenye Taasisi na asasi binafsi kama PSPF, LHRC, CTI uone watendaji wake wakuu wanalipwaje.
 
Nini Mwalimu,wazee walovunjiwa nyumba na mabomu mbagala wamepewa hundi za Tshs30,000/=kama malipo ya fidia ya uharibifu ulotokea.

Je,huu ni uungwana????

Duuh inaumaaaaaa! yaani unaweza fikiri tunaongozwa na mapunguani vile. Duuh kweli Serikari its a strange creature u can never think of what will strangely do next............
 
Back
Top Bottom