Mishahara ya madaraja mapya inatakiwa ilipwe baada ya muda gani?

mahuwi

Member
Oct 18, 2011
22
1
Mh kawambwa, Waziri Ghasia na mkulo wizara zenu zinatuhumiwa kwakuchelewesha ama kutojali kuwalipa walimu wa chuo kikuu kilichokikubwa kuliko vyote huko dodoma. walimu hao walishapandishwa muda mrefu sana lakini mwajiri wao anadai alishawapa taarifa yakustahili walipwe pesa zao lakini mnadaiwa kutotoa ruhusa ama kupuuzia haki zao.

kama ni kweli mtawaomba radhi walimu hao na kuwalipa stahili zao lini? Na mnadhani kama hamhusiki walimu hawa wanafanya kazi nchi gani wakati wenzao walimaliza novemba 2010 na desemba wakalipwa mishahara yao?

Walipeni walimu stahili zao bwana acheni kuwanyanyasa kiasi hicho kwa stahili zao. wamefanya kazi tangu novemba 2010 ya daraja hilo jipya hadi leo hawajalipwa, nanyi mnafanya kazi kwa mkopo?
 
Ualimu ni wito..

Hii issue ni serious sana. Mawaziri kawambwa, Mkulo na Ghasia naomba muelewe hawa watu wamekuwa wakitoa lectures na seminars karibu mwaka sasa tangu wawe promoted na hawalipwi mshahara huo ina maanisha wanafanya kazi kwa kukopwa, je na nyie mnafanya kazi kwa mkopo? Na vipi nyaraka zenu zinazozuia taasisi za serikali kutorundika madeni na sasa watumishi wenu wamerundika deni tena kwa majibu kuwa ofisi zenu ndo hazitaki kuwalipa walimu hawa.

Mie nadhani Tz ni moja na universities za umma ziko chini yenu na hazina moja inakuwaje wengine wawe promoted mwezi huu na kulipwa mwezi unaofuata hali hawa wakifanya kazi na kungoja kwa mwaka sasa bila kulipwa. Primary school teachers hawachukui zaidi ya mwaka wanalipwa hawa lecturers wamemkosea nani wakamwombe msamaha walipwe?
 
Umeona eeh ualimu ni wito kweli kwahiyo rizikeni na hicho mnachopata huku mkiendelea kuwa wavumilivu

Watu wanhangaika kusoma wanaajiriwa, wanasaini mkataba unaoonesha uwepo wa kupanda madaraja na malipo yake stahili. Hapa hakuna wito vinginevyo wanasiasa kwakuwa wameajiriwa na wananchi wangekuwa wa kwanza kufanya kazi bila malipo. Kwa hili mawaziri mnaohusika chueni hatua za dhati japo zimechelewa mno kwa kuwa hawa watu wana mwaka sasa hawalipwi hela hiyo.
 
Back
Top Bottom