Mishahara ya madaktari kwa baadhi ya nchi za Afrika

Kiwango cha uchumi una maanisha nini? Tz ni tajiri kuliko zambia, namibia na nchi nchi nyingine sema tu tumeshindwa kutumia rasilimali zetu. Rwanda ni kanchi masikini ila madaktari wao wanapata zaidi ya milioni 5 za Tz. Utaniambia ni wachache, kumbuka pia wao wana rasilimali chache. Kama swala ni uchache na wingi wa watu basi USA wangekuwa masikini. Wao marais wao hawapo angani kila siku kula kodi za umma, hawalipani vikao nk ndio maana wanamudu kulipa vizuri
Liquidity ndo inalipa mishahara, sio 'potential' ya rasilimali..ambazo hata hivyo tumeshindwa kuzipa thamani.unless utuambie turudi kwene ujima wa barter trade..
 
jamani jamani tuache unafiki tujifunze kuangalia facts. hebu ona relation ya mshahara wa mbunge na daktari katika nchi tuitazo role model wetu
CANADA--- mbunge analipwa 20millionTsh na daktari average 18millioniTsh

UINGEREZA---mbunge analipwa 10millioniTsh na daktari wakawaida aliyeajiliwa 8.8 millioniTsh

TANZANIA----mbunge analipwa 10millioniTSh na daktari analipwa 0.95millioniTsh
ukiangalia mshahara wa dokta na mbunge nchi hizo unakaribiana na wabunge lakini bongo ni mara kumi zaidi. kweli wabunge wahuko wanapewa nyumba na magari je watanzania hawapewi?. pesa zipo ila hatujui vipaumbele(tunatakiwa tujifunze hili).bila kusahau mbona mshahara wa mbunge wa tanzania unafanana na wa uingereza madokta kuomba theluthi ya hiyo ndio iwe nongwa.
 
Huu ni mshahara wa daktari anayeanza kwa kiwango cha shillingi za kitanzania

Zambia-millioni 1.9

Namibia-millioni 5.7

Africa kusini-millioni 6.2

botswana-millioni 4.023

kenya- walikuwa wanadai milioni 3.299
wazambia wamemuingiza sata kawapa hizo mwaka huu ni nyongeza ya 100%

Pamoja na hiyo mishahara kwa Shs za Tanzania, pia ungeweka wastani wa kipato kwa kila mwananchi kwa mweizi (Income per capita) kwa kila nchi ili tupate uwiano vizuri.
 
Mambo mengi hapa kwetu yanawezekane ila tumekaririshwa kuwa 'nchi yetu ni maskini,nchi yetu ni maskini' huo ndo wimbo tunaoimbiwa na watawala wetu....., na umetukolea kweli!

Nakuunga mkono kwa hili. Umaskini wa nchi yetu ni nini? Mbona haohao wanaosema nchi yetu maskini wanatuibia kila kona? Jumlisha fedha zote zilizoibiwa au kufujwa tokea 1995 adi sasa utashangaa. Bado watu wanakaririshwa kuamini nchi yetu maskini! Iko siku wataachia ngazi na tutawataka waishi maisha ya kilala hoi waone adha inayowapata wanachi.
 
serikali inapaswa kulimaliza hili suala la mgomo wa madakitari kama wameshindwa waachie ngazi waache vitisho vya ajabu.
 
Unauhakika na hayo unayoyasema au unadanganya watu ukijua watu hawafuatilii mishahara ya nchi nyingine hakuna nchi katika africa inayotoa viwango hivyo ulivyovitaja mkuu mbona unachangia kuwauwa watanzania wapigakura masikini. Acha hayo kwa africa nchi inayoongoza kwa madaktari kupata mshahara wa juu ni africa ya kusini na kwa daktari anayeanza anapokesa kiasi cha fedha sawa na 1.8 million za kitanzania
lakini lazima utambue kuwa haikuwa haraka hivyo kama hawa madaktari wanasiasa wanavyotaka iwe haraka hivyo hayo mambo yanawezekana ila taratibu mkuu tusipende kushabikia mambo ambayo yanatesa watanzania wenzetu
 
aibuuuuuu! mmesoma lakini hamjaelimika kama mmeelimika basi ni wabinafsi kupindukia tufe tukifanya kazi kwa ajili yenu! eti nyie ni muhimu sana, kawadanganya nani? mama lishe asipolipa kodi hata hiyo laki tisa mnayoidharau mtaipata wapi?
USHAURI WA BURE: Sisi sote tunategemeana. Mkulima mnayetaka afe kwa migomo yenu asipolima mtakula nini? au mnafikiri mtakula hela ? mnakera kweli kweli.
 
Mh Dr JK ana umri wa baba yangu. Ila nasema anapenda majungu majungu, huwa ni dhaifu wa kutafuta ukweli. Ni mwepesi kudanganywa
 
[h=2][/h]
Unauhakika na hayo unayoyasema au unadanganya watu ukijua watu hawafuatilii mishahara ya nchi nyingine hakuna nchi katika africa inayotoa viwango hivyo ulivyovitaja mkuu mbona unachangia kuwauwa watanzania wapigakura masikini. Acha hayo kwa africa nchi inayoongoza kwa madaktari kupata mshahara wa juu ni africa ya kusini na kwa daktari anayeanza anapokesa kiasi cha fedha sawa na 1.8 million za kitanzania
lakini lazima utambue kuwa haikuwa haraka hivyo kama hawa madaktari wanasiasa wanavyotaka iwe haraka hivyo hayo mambo yanawezekana ila taratibu mkuu tusipende kushabikia mambo ambayo yanatesa watanzania wenzetu​
 
Unauhakika na hayo unayoyasema au unadanganya watu ukijua watu hawafuatilii mishahara ya nchi nyingine hakuna nchi katika africa inayotoa viwango hivyo ulivyovitaja mkuu mbona unachangia kuwauwa watanzania wapigakura masikini. Acha hayo kwa africa nchi inayoongoza kwa madaktari kupata mshahara wa juu ni africa ya kusini na kwa daktari anayeanza anapokesa kiasi cha fedha sawa na 1.8 million za kitanzania
lakini lazima utambue kuwa haikuwa haraka hivyo kama hawa madaktari wanasiasa wanavyotaka iwe haraka hivyo hayo mambo yanawezekana ila taratibu mkuu tusipende kushabikia mambo ambayo yanatesa watanzania wenzetu
Nadhani wewe upo nyuma ya wakati sana! Na safari hii ya 2015 mtakoma mliozoea kura rushwa. Ni mabadiliko tu, kama siyo CDM ni CUF, wajinga nyie! Na mtafungwa wote na kufilisiwa!
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom