projectman
JF-Expert Member
- Sep 8, 2015
- 349
- 484
Kama nilivyoelezea kichwa cha habari hapo juu!
Tumesikia watumishi hewa na tuhuma mbalimbali! watu wakitumbuliwa majipu kwa ufisadi,wizi na dhuluma mbalimbali dhidi ya ubadhirifu wa fedha za serikali.
Hawa wanaopatikana na majipu ya wizi wa mali za umma mbona hatuoni hatua za kimahakama na sheria zikiwashitaki watuhumiwa hawa ili wawajibike au kufungwa kama sheria inavyosema?
Je, hawa ni wakina nani na kila mmoja alihusika na nani na waliiba shilingi ngapi?
Au ndio business as usual! kuchezeana akili.
Kwani mahakama na magereza ni kwa wakina nani?
Kwa kweli kwa hili suala bado tunahitaji kulijua zaidi suala hili maana haiwezekani mwizi wa kuku anafungwa miaka kazaa lakini mwizi wa bilioni moja au mbili na zaidi anaachiwa huru! hivi kuna kuku wangapi katika bilioni 1.
Tunataka kuona watuhumiwa wanajazana huko mahakamani na gerezani kama sheria inavyosema.
Naomba kuwasilisha.
Tumesikia watumishi hewa na tuhuma mbalimbali! watu wakitumbuliwa majipu kwa ufisadi,wizi na dhuluma mbalimbali dhidi ya ubadhirifu wa fedha za serikali.
Hawa wanaopatikana na majipu ya wizi wa mali za umma mbona hatuoni hatua za kimahakama na sheria zikiwashitaki watuhumiwa hawa ili wawajibike au kufungwa kama sheria inavyosema?
Je, hawa ni wakina nani na kila mmoja alihusika na nani na waliiba shilingi ngapi?
Au ndio business as usual! kuchezeana akili.
Kwani mahakama na magereza ni kwa wakina nani?
Kwa kweli kwa hili suala bado tunahitaji kulijua zaidi suala hili maana haiwezekani mwizi wa kuku anafungwa miaka kazaa lakini mwizi wa bilioni moja au mbili na zaidi anaachiwa huru! hivi kuna kuku wangapi katika bilioni 1.
Tunataka kuona watuhumiwa wanajazana huko mahakamani na gerezani kama sheria inavyosema.
Naomba kuwasilisha.