Misemo na Methali za Kiswahili

Mr. Miela

JF-Expert Member
Aug 2, 2007
1,226
2,055
Wajameni;

kuna mtu anaweza kunipa link itakayonisaidia kupata Misemo ya kiswahili katika mtandao?
 
Hapa kuna methali za kiswahili

Kuna kazi kibao za Kiswahili kwenye wikipedia and its sisters.


Ebwana methali nyingine nilidhani nafahamu maana zake. Hii inatoka wikiquote,
Usimwamshe aliyelala, ukimwamsha utalala wewe.
Don't trust a fool with your private matters, if you do, you will be the fool!​


.
 
Hapa kuna methali za kiswahili

Kuna kazi kibao za Kiswahili kwenye wikipedia and its sisters.


Ebwana methali nyingine nilidhani nafahamu maana zake. Hii inatoka wikiquote,
Usimwamshe aliyelala, ukimwamsha utalala wewe.
Don't trust a fool with your private matters, if you do, you will be the fool!​
.
Mchelea mwana kulia....?
 
...kwamba mzazi asipomuadabisha mwanae, atakuja kulia yeye?

Mmepatia vema nyote wawili:

Kila msemo wa kiswahili una maana sana! Nawapa kwa kifupi ili mmalizie na wengine mjaribu kupambanua kwa undani zaidi.

Wale mnaoendekeza wanenu gharama yake kwenu ni kubwa. Methali hiyo inaendana kabisa na "Samaki mkunje angali mbichi"... Sambamba naweza kusema inaendana kabisa na "Maji yakimwagika hayazoleki!"

Kuna huu pia:-

Mficha uchi.............
 
Mmepatia vema nyote wawili:

Kila msemo wa kiswahili una maana sana! Nawapa kwa kifupi ili mmalizie na wengine mjaribu kupambanua kwa undani zaidi.

Wale mnaoendekeza wanenu gharama yake kwenu ni kubwa. Methali hiyo inaendana kabisa na "Samaki mkunje angali mbichi"... Sambamba naweza kusema inaendana kabisa na "Maji yakimwagika hayazoleki!"

Kuna huu pia:-

Mficha uchi.............

.... hazai!
 
wantala chikokoto, chaulezi chinyunyunyu..................

Gang, samahani hivi hayo yako katika Kiswahili au ni lugha nyingine tu asilia?!
Naomba tafsri yake tafadhali iwe Kiswahili au lugha nyingineyo yoyote.. thanks.
 



...kwamba mzazi asipomuadabisha mwanae, atakuja kulia yeye?

... msemo huu una apply kwa vijibwa pia... kwamba usipo kaadabisha kajibwa, kitakuhangaisha kikikua na kuwa jibwa!! :D


where u bn fool?! missed ya.
 
Mficha uchi.............
....hazaizai ovyo.

Unajua, Invisible, huu msemo, ni wanaume wamejitungia wapate kujisadia kwa kupumbaza wanawake.

Ukiwa nje ya ndoa na ukawa unaficha basi hutazaliana zaliana nje ya ndoa, kitu ambacho ni kizuri kwa mficha.

Ukiwa ndani ya ndoa na ukawa unaficha ina maana hutaki kuzaa tokea hapo. Kitu ambacho ni nia ya mficha.

Kama nakosea, hebu nisaidie kama ujumbe "mficha uchi hazai" una mantiki au ujumbe kwa manufaa ya mficha.
 
Mficha uchi.............



Unadhani mtunzi alilenga kumaanisha kama inavyoelezwa hapa chini?

Literal Meaning: We should let our friends know our troubles so they can help us, even if that involves revealing something shameful.
 
Mimi huwa nazimia sana methali hii:

Mgaagaa na upwa (mpwa?)............

Hivi hii misemo inaungukia kwenye kitabu cha methali pia?
- Dunia tambara bovu
- Utakiona cha mtema kuni
 
Mficha uchi....
Hii methali inaendana na methali hii:
Mficha maradhi kifo kitamuumbuwa au Mzaa mzaa mwishowe utumbuka usaha.

"Samaki mkunje angali mbichi..."
Hakisha kauka hakunjiki

Mgaagaa na upwa...
Hali wali mkavu

Dunia tambara bovu
Dunia ni sawa na nguo chakavu, inataka taadhari sana jinsi ya kuishi na kusabiiana na watu. Bila ya taadhari inaweza kukufika maafa au kupata hasara... ni sawa na mtu aliye vaa nguo iliyo chakaa... wakati wowote inaweza kumchanikia.

Utakiona cha mtema kuni
Hii methali inatokana na hadithi au simulizi ya mkata kuni (Mtema kuni... Hiki ni kiswahili cha zamani). Kwa ufupi inasimuliwa kwamba mkata kuni alikwenda porini kwa nia ya kutema kuni (kukata kuni) kutokana na sababu anazo zijuwa yeye au kwa kuzidiwa na mawazo alipofika porini akapitiwa na usingizi (kama bado nakumbuka vizuri) ndio kwanza ulikuwa muda wa Mawio yaani jua linachomoza). Alipokurupuka... kuangaza huku na huku shoka halioni, na hali anakumbuka vizuri kulichukuwa...

Yeye hakahisi labda limedondoka mahali... akaanza kulitafuta kuanzia Mawio mpaka Machweo (Kuzama kwa jua Wakati wa Magharibi) Mwisowe akajikuta amechoka na shoka halionekani. Akaamua kukaa chini ya mti ili apumzishe akili na kutafakari upya wapi alipolidondosha shoka lake. Wakati anajiandaa kukaa chini kuangalia begani kwake analiona shoka lake... kumbe alikuwa amesahau kuwa shoka lilikuwa amelining'iniza begani kwake...

Hapo ndipo palipo patikana huo msemo wa "Utakiona cha mtema kuni... Kutafuta shoka wakati lipo begani."

Hii kidogo inataka kufanana ule msemo wa "Utakiona kilicho vunja shoka mpini ukabaki... msemo huu umetokana na simulizi za Sir H. Rider Haggard kwenye moja ya simulizi zake zinazo elezea visa vya mwindaji Tembo hodari Bwana Allan Quatermain (Makumazan or Macumazahn)... Na msaidizi wake Msolopaganzi (Umslopogaas) na shoka lake Nkosi kazi (Inkosi-kaas)... Bwana Henry Curtis, na rafikie Kapiteni Good, (Bwana Mzuri).
Kwenye liwaya hii ndipo pia lilipo patikana jina Gagula... Kibibi kilichokuwa kichwawi (Kigagula)

Vitabu hivi ni miongoni mwa vitabu ambavyo vinaonyesha au kusimulia ujasiri wa hali ya juu sana... Pia kwenye ile riwaya ya Machimbo ya Mfalme Suleiman na nchi ya Wakukuana... Na vile vingine ambavyo havikuwahi kutafsiriwa kwa kiswahili kama vile SHE & Ayesha (Tibet)

Wale walio wahi kusoma watamkumbuka sana Bwana Msolopaganzi (Umslopogaas) na majigambo yake a.k.a Mikwara mizito aliyokuwa akiwatishia maadui zake... Nakumbua mwisho wa riwaya Umsolopaganzi alipomaliza kazi ya kulinda ngazi kuu... Alikuwa amepata majeraha mengi mwilini... akajua kuwa mwisho wa uhai wake umekaribia ndipo alipoamua kufa na shoka lake (Bibi msemi).... lilizungusha shoka lake kiasi ya kuonekana kama mwali wa moto... kisha kwa pigo moja... pigo lililo takatifu... Pigo lililo nyooka... akalishusha shoka lake kwa kasi ya ajabu na kulipasuwa jiwe lile na huku shoka lake likitawanyika vipande vipande na kubakia akiwa ameshikilia mpini wa shoka ukiwa mzima.... Mzee wa kizuru akaanguka chini akakata roho...

Soma baadhi ya vipande toka Riwaya ya Allan Quatermain

...Umslopogaas... Straight up the hall he went, leaving
behind him a track of blood on the marble pavement, till at last
he reached the sacred stone, which stood in the centre of it,
and here his strength seemed to fail him, for he stopped and
leaned upon his axe. Then suddenly he lifted up his voice and
cried aloud...

'I die, I die... but it was a kingly fray. Where are they who
came up the great stair? I see them not. Art thou there, Macumazahn,
or art thou gone before to wait for me in the dark whither I
go? The blood blinds me... the place turns round... I hear the
voice of waters.'

Next, as though a new thought had struck him, he lifted the red
axe and kissed the blade.

'Farewell, Inkosi-kaas,' he cried. 'Nay, nay, we will go together;
we cannot part, thou and I. We have lived too long one with
another, thou and I.

'One more stroke, only one! A good stroke! a straight stroke!
a strong stroke!' and, drawing himself to his full height, with
a wild heart-shaking shout, he with both hands began to whirl
the axe round his head till it looked like a circle of flaming steel.
Then, suddenly, with awful force he brought it down straight
on to the crown of the mass of sacred stone. A shower of sparks
flew up, and such was the almost superhuman strength of the blow,
that the massive marble split with a rending sound into a score
of pieces, whilst of Inkosi-kaas there remained but some fragments
of steel and a fibrous rope of shattered horn that had been the
handle
. Down with a crash on to the pavement fell the fragments
of the holy stone, and down with a crash on to them, still grasping
the knob of Inkosi-kaas, fell the brave old Zulu... dead.

And thus the hero died.

A gasp of wonder and astonishment rose from all those who witnessed
the extraordinary sight, and then somebody cried, '_The prophecy!
the prophecy!_ He has shattered the sacred stone!' and at once
a murmuring arose.
Soma majigambo (Mikwara ya mzee wa Kizuru)

'...Ah, Macumazahn,' he said, 'I suppose it is because I am getting
old, but I don't think that I shall ever learn to understand
the ways of you white people. Look there now, I pray thee, they
are a pretty pair of doves, but what is all the fuss about, Macumazahn?
He wants a wife, and she wants a husband, then why does he not
pay his cows down... like a man and have done with
it? It would save a deal of trouble, and we should have had
our night's sleep. But there they go, talk, talk, talk, and
kiss, kiss, kiss, like mad things. Eugh!'

'Thou shalt stand against me man to man, be not afraid,' replied
Umslopogaas, still in the same ominous voice. 'Thou shalt stand
face to face with Umslopogaas, of the blood of Chaka, of the
people of the Amazulu, a captain in the regiment of the Nkomabakosi,
as many have done before, and bow thyself to Inkosi-kaas, as
many have done before. Ay, laugh on, laugh on! tomorrow night
shall the jackals laugh as they crunch thy ribs.'

'What, comest thou too?' laughed out the old warrior. 'Welcome
....a welcome to thee, brave heart! Ow! for the man who can die
like a man; ow! for the death grip and the ringing of steel.
Ow! we are ready. We wet our beaks like eagles, our spears
flash in the sun; we shake our assegais, and are hungry to fight.
Who comes to give greeting to the Chieftainess (Inkosi-kaas)?
Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the
Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas,
of the tribe of the Maquilisini, of the people of Amazulu, a
captain of the regiment of the Nkomabakosi: I, Umslopogaas, the
son of Indabazimbi, the son of Arpi the son of Mosilikaatze,
I of the royal blood of T'Chaka, I of the King's House, I the
Ringed Man, I the Induna, I call to them as a buck calls, I challenge
them, I await them. Ow! it is thou, it is thou!'
Umbopa...
'Koos' (chief), he began, 'Koos-y-Pagete! Koos-y-umcool! (Chief
from of old ...mighty chief) Koos! Baba! Macumazahn,
old hunter, slayer of elephants, eater up of lions, clever one!
watchful one! brave one! quick one! whose shot never misses,
who strikes straight home, who grasps a hand and holds it to
the death (i.e. is a true friend) Koos! Baba! Wise is the voice
of our people that says, "Mountain never meets with mountain,
but at daybreak or at even man shall meet again with man."
Behold!
a messenger came up from Natal, "Macumazahn is dead!" cried he.
"The land knows Macumazahn no more." That is years ago. And
now, behold, now in this strange place of stinks I find Macumazahn,
my friend. There is no room for doubt. The brush of the old
jackal has gone a little grey; but is not his eye as keen, and
are not his teeth as sharp? Ha! ha! Macumazahn, mindest thou
how thou didst plant the ball in the eye of the charging buffalo
...mindest thou...
 
Last edited:
Back
Top Bottom