Miradi ya Ukanda Mmoja na Njia Moja yabadilisha taswira ya Kenya

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
Na Kelly Ogome

Kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, mataifa ya Afrika Mashariki yameshuhudia mabadiliko makubwa katika uchumi na miundombinu. Haya ni kulingana na ripoti ya tathmini ya miradi ya Ukanda Mmoja,Njia Moja(BRI) iliyotolewa na Taasisi ya Sera ya Africa API.

Kenya ni miongoni mwa mataifa ya bara la Afrika ambayo yanaendelea kunawiri kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya BRI kulingina na ripoti hiyo ya API inayoangazia mafanikio ya BRI kati ya mwaka 2018 hadi 2021.

1638745528007.png


1638745538111.png


Ripoti hiyo iliyotolewa mwishoni mwa Novemba jijini Nairobi inaeleza kuwa mataifa 172 na mashirika ya kitaifa ulimwenguni yamesaini mikataba 200 ya makubaliano na China katika utekelezaji wa miradi ya BRI.

Kando na kupanua miundo mbinu na biashara, ripoti hiyo inaeleza kuwa nafasi za ajira kwa raia wa mataifa ya Afrika mashariki yanayotekeleza miradi ya BRI zimeongezeka. Kenya ni mojawapo ya nchi zinazotekeleza miradi ya BRI kikamilifu na haraka, na hili linadhihirika wazi kupitia ujenzi wa bandari ya Lamu, kukamilika kwa awamu ya kwanza ya reli ya kisasa SGR, barabara mbali mbali kote nchini bila kusahau mikakati ya kupiga jeki uchumi kupitia kuboreshwa kwa biashara kati ya Kenya na China.

Mkurugenzi wa taasisi ya sera ya Afrika Profesa Peter Kagwanja wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo alisema kuwa Afrika ni mshirika mkubwa wa kirafiki na kibishara wa China na uhusiano huu umepanua kiwango cha uwekezaji barani.“Mwaka 2003, kiasi cha uwekezaji vitegauchumi wa China nchini Kenya ilikuwa dola za kimarekani milioni 75, hivi sasa, kiwango hicho kimeongezeka na kufikia dola bilioni 2.7 kwa mwaka. Zaidi ya hayo, 45% ya misaada iliyotolewa na serikali ya China kwa mataifa ya kigeni kati ya mwaka 2013 na 2018 ilielekezwa barani Afrika. ”Alisema Profesa Kagwanja.

1638745557466.png


Kuanzia mwaka 2000 hadi 2019, mashirika kadhaa ya kifedha ya China yalisaini mikataba 1,141 yenye thamani ya dola bilioni 153 na serikali za mataifa ya Afrika kufadhili miradi ya maendeleo, thuluthi ya miradi hiyo ikiwa chini ya Ukanda Mmoja, Njia Moja. Jambo la kutia moyo ni kuwa mikopo hiyo ni nafuu ikilinganishwa na mikopo yenye masharti makali kutoka kwa mataifa ya magharibi ilisema ripoti hiyo.

Balozi wa China nchini Kenya Bw. Zhou Pingjian aliyehudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti hiyo alisema kuwa Kenya na China ni marafiki wa dhati na wa jadi na kwa misingi hiyo China itaendelea kushirikiana na marafiki zake katika kufanikisha miradi ya BRI. “Katika siku zijazo, China itaendelea kutekeleza miradi ya BRI na kushirikiana na marafiki kuafikia azma hii. Kenya ni rafiki wa China na China iko tayari kuisaidia Kenya kuboresha miundombinu yake” alisema Balozi Zhou.

Balozi Zhou alisema kuwa miundombinu hafifu ni mojawapo ya sababu ambazo zimefanya baadhi ya mataifa kusalia nyuma kimaendeleo, lakini tatizo hilo litasuluhishwa kupitia miradi ya BRI.

1638745578860.png


Katibu mkuu wa wizara ya viwanda na biashara ya Kenya Bw. Kirimi Kaberia alisema kuwa miradi ya Ukanda Mmoja na Njia Moja imeimarisha maendeleo ya kiuchumi kwa kufungua masoko mapya na kuunganisha miji ya bara la Afrika.

“BRI imefungua vituo vipya vya biashara barani Afrika. Chini ya mwongo mmoja, Kenya sasa ina bandari ya kimataifa katika mji wa Lamu, reli ya kisasa SGR inayounganisha pwani ya Kenya na jiji kuu la Nairobi bila kusahau ujenzi wa maelfu ya kilomita za barabara ambazo zinaunganisha miji na vijiji vya Kenya.” Alisema Bw. Kaberia.

Ripoti ya benki ya dunia ya mwaka wa 2019 inakadiria kuwa zaidi ya watu milioni 7.6 katika mataifa yanayoshiriki kwenye miradi ya BRI zikiwemo nchi zaidi ya 40 za Afrika wataondoka katika umaskini kupitia utekelezaji wa miradi ya Ukanda Mmoja, Njia moja.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom