Kamukhm
JF-Expert Member
- Aug 30, 2015
- 2,799
- 4,195
Mipango Kabambe Master plan, ni dira ya maendeleo ya mji/taasisi, ambayo huandaliwa kwa kuzingatia Ushirikishwaji wa wadau na ushauri wa kitaalamu wa taaluma zote.
Huu mpango unaeleza kwa ujumla mahitaji ya msingi ya mji, namna bora ya kuyafikia mahitaji haya, na majukumu ya kila mmoja katika kutimiza mahitaji haya ili kuleta tija kwa umma wote iwe kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia.
Hii mipango inaandaliwa kwa fedha nyingi sana. Na TAMISEMI wanalipa wakandarasi kuandaa hii mipango, ambayo ukiisoma hakuna mji masikini. Miji yote ni vibrant na inter connected vizuri kuleta maendeleo jumuishi.
Kwa mujibu wa document hizi, biashara zimeshamiri, afya zimeboreka, kuna matumizi mazuri na uwekezaji unaleta tija kubwa katika matumizi ya fedha za serikali.
Kwanini yote haya hayatokei!? Kwa mujibu wa mpango!?
1) Mipango inaandaliwa kama dili tu au requirement za kupata fedha na sio vipaumbele vya halmashauri na serikali kwa ujumla.
2) Siasa imechukua usukani toka kwa wataalamu, matokeo yake miji inaendeshwa kwa matamko ya watu wasio wataalamu na ushauri usioongozwa na tafiti
3) wananchi wamedekezwa,. Na hawapendi kufuata sheria na taratibu. Kwa eneo hili nazungumzia kuheshimu mpango kwa kuutekeleza kama inavyotakiwa. Moja ya maeneo wananchi wanakochangia ni kupitia uvamizi wa maeneo Tengefu na kulia lia kwa wanasiasa.
Nini kifanyike
Kama nilivyosema kupitia Kichwa cha Uzi huu.
Kwa kuwa mpango Kabambe (Master plan) ni mawazo ya wananchi tena yaliyoongozwa na utaalamu, basi yafuatayo yafanyike.
1) Mafanikio ya wakurugenzi yapimwe kwa kiwango cha utekelezaji wa master plans na sio makusanyo kama ilivyo sasa.
2) Sera/ilani za wagombea zijengwe juu ya namna ya kutekeleza master plan (mpango kabambe). Hayati Mzee Benjamin Mkapa alisisitiza juu ya kuwa na "Continuity" nadhani hii ndio itakuwa Mwarobaini.
3) Halmashauri na Serikali kwa ujumla ijenge utamaduni wa kusimama na sheria (kuboresha utawala wa kisheria) bila hivyo matamko yanaweza kutumika vibaya na watu kwa manufaa binafsi ikiwemo kupata umaarufu katika siasa.
4) Mipango ya halmashauri iibuliwe kutoka katika mahitaji orodheshwa ndani ya Master plan. Sio kuibuka ni miradi ambayo haitakuwa na uhusiano wenye tija na miradi.iliyopo tayari, inayoendelea au itakayokuja.
#Mungu Atujalie mafanikio tele katika kazi zetu. Na Alibariki Serikali yetu na Viongozi wake. Amin.#
Huu mpango unaeleza kwa ujumla mahitaji ya msingi ya mji, namna bora ya kuyafikia mahitaji haya, na majukumu ya kila mmoja katika kutimiza mahitaji haya ili kuleta tija kwa umma wote iwe kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia.
Hii mipango inaandaliwa kwa fedha nyingi sana. Na TAMISEMI wanalipa wakandarasi kuandaa hii mipango, ambayo ukiisoma hakuna mji masikini. Miji yote ni vibrant na inter connected vizuri kuleta maendeleo jumuishi.
Kwa mujibu wa document hizi, biashara zimeshamiri, afya zimeboreka, kuna matumizi mazuri na uwekezaji unaleta tija kubwa katika matumizi ya fedha za serikali.
Kwanini yote haya hayatokei!? Kwa mujibu wa mpango!?
1) Mipango inaandaliwa kama dili tu au requirement za kupata fedha na sio vipaumbele vya halmashauri na serikali kwa ujumla.
2) Siasa imechukua usukani toka kwa wataalamu, matokeo yake miji inaendeshwa kwa matamko ya watu wasio wataalamu na ushauri usioongozwa na tafiti
3) wananchi wamedekezwa,. Na hawapendi kufuata sheria na taratibu. Kwa eneo hili nazungumzia kuheshimu mpango kwa kuutekeleza kama inavyotakiwa. Moja ya maeneo wananchi wanakochangia ni kupitia uvamizi wa maeneo Tengefu na kulia lia kwa wanasiasa.
Nini kifanyike
Kama nilivyosema kupitia Kichwa cha Uzi huu.
Kwa kuwa mpango Kabambe (Master plan) ni mawazo ya wananchi tena yaliyoongozwa na utaalamu, basi yafuatayo yafanyike.
1) Mafanikio ya wakurugenzi yapimwe kwa kiwango cha utekelezaji wa master plans na sio makusanyo kama ilivyo sasa.
2) Sera/ilani za wagombea zijengwe juu ya namna ya kutekeleza master plan (mpango kabambe). Hayati Mzee Benjamin Mkapa alisisitiza juu ya kuwa na "Continuity" nadhani hii ndio itakuwa Mwarobaini.
3) Halmashauri na Serikali kwa ujumla ijenge utamaduni wa kusimama na sheria (kuboresha utawala wa kisheria) bila hivyo matamko yanaweza kutumika vibaya na watu kwa manufaa binafsi ikiwemo kupata umaarufu katika siasa.
4) Mipango ya halmashauri iibuliwe kutoka katika mahitaji orodheshwa ndani ya Master plan. Sio kuibuka ni miradi ambayo haitakuwa na uhusiano wenye tija na miradi.iliyopo tayari, inayoendelea au itakayokuja.
#Mungu Atujalie mafanikio tele katika kazi zetu. Na Alibariki Serikali yetu na Viongozi wake. Amin.#