Ubungoubungo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2008
- 2,502
- 739
Jamani, mipaka ya ziwa victoria watu wanataka kuifuta, ili kusiwe na mipaka kabisa. ziwa victoria linahitajika sana kwa uchumi wa kenya pamoja na kwamba wanamiliki asilimia 6% tu ya ziwa, ila wana viwanda vingi na wanazalisha samaki wengi viwandani kuliko uganda na tz. Samaki kwenye kaeneo kao wameisha, wanachukulia kisiwa cha migingo na mgogoro wake kutaka kufuta mipaka ili waje wavue samaki huku kwetu pia ambako sisi wenye ziwa kubwa tulilinda mazalia ya samaki wetu kwa kukamata na kuchoma nyavu nyingi za kokora pamoja na kuwapeleka jela wanachi wetu.
Hivi tz tuko tayari? wengi wanasema, ati, hii sisi wananchi hata tukipita makelele, hata ile ya ardhi ya EAC, haituhusu, kwasababu wanaoamua ni viongozi wetu na sio sisi, hivi Tz ya aina hii bado ipo? mbona hapa tz siku hizi maamuzi yanakuwa ya wananchi? tuwe macho, viongozi wetu wasituburute tukajikuta wameingia mikataba ya ajabuajabu, wakahatarisha maliasili zetu kwa kuwagawia majirani zetu wanaotutukanaga kuwa sisi hatuna akili hatujasoma na hatujui biashara kazi yetu ni kukaa kwenye mkeka kupiga soga na kula kipunga.
kama kuungana kwenye jumuiya ya afrika mashariki ni muhimu, basi, tunataka MIPAKA YETU YOOOTE ILINDWE, ARDHI YETU ILINDWE, MALIASILI ZETU ZILINDWE ZOOOOTE, tena kikamilifu. la sivyo, watu watakuja wajiuzuru hapa. Mungu ibariki Tanzania.
Hivi tz tuko tayari? wengi wanasema, ati, hii sisi wananchi hata tukipita makelele, hata ile ya ardhi ya EAC, haituhusu, kwasababu wanaoamua ni viongozi wetu na sio sisi, hivi Tz ya aina hii bado ipo? mbona hapa tz siku hizi maamuzi yanakuwa ya wananchi? tuwe macho, viongozi wetu wasituburute tukajikuta wameingia mikataba ya ajabuajabu, wakahatarisha maliasili zetu kwa kuwagawia majirani zetu wanaotutukanaga kuwa sisi hatuna akili hatujasoma na hatujui biashara kazi yetu ni kukaa kwenye mkeka kupiga soga na kula kipunga.
kama kuungana kwenye jumuiya ya afrika mashariki ni muhimu, basi, tunataka MIPAKA YETU YOOOTE ILINDWE, ARDHI YETU ILINDWE, MALIASILI ZETU ZILINDWE ZOOOOTE, tena kikamilifu. la sivyo, watu watakuja wajiuzuru hapa. Mungu ibariki Tanzania.