Miongoni mwa mambo yanayomkera mwanamke!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,393
Naomba niwaambie jambo moja. Miongoni mwa mambo ambayo humkera mwanamke ni kukutana na mwanaume mwongo na anayejikweza. Mwanamke na hata mwanaume hupenda kitu au mtu asilia na sio mtu feki.

Ukweli ni kwamba kwa kutojiamini kutokana na kuambiwa kwamba wao ni bora kuliko wanawake, na kufundishwa kwamba ili waonekane wa maana ni lazima waoneshe mafanikio na ndipo watakapokubaliwa na wanawake, wanaume wengi wamekuwa wakijikweza na kusema uongo ili kuwapata wanawake.

Ni kweli huwapata wanawake hao, lakini cha kushangaza huwapata wanawake hao sio kwa sababu ya uongo na kujikweza kwao, bali ni kwa sababu wanakuwa wamevutiwa nao. Na kwa sababu ya ujinga mwanaume atadhani amempata mwanamke kwa sababu ya uongo na kujikweza kwake!

Kwani hamjawahi kuona wanawake kwa maelfu wanakimbia ndoa za wenye fedha na walio Maarufu? Cécilia Ciganer-Albéniz, Mke wa Rais wa Ufaransa Nicolas Salkozy ni mfano wa jambo hili.Kama ingekuwa anachoangalia mwanamke ni mali na umaarufu, naamini kusingekuwa na talaka nyingi.

Kwa asilimia nyingi, mwanaume ndiye anayejikanyaga kwa mwanamke, ndiye anayejikweza ili mwanamke ampandishe thamani.
 
haijambo ,atleast ukweli umesemwa,, you make my day,, huu ni ukweli thabit,,
 
ahh makontena yangu bandarini hayajatoka

yule atak kunilipa m8 zangu....
ahh yule mpumbavu tu bila mimi asingepaweza mjin apa...


ahhhh mavx yangu...ile hammer sjui vip...
 
ngoja, kwanza umechelewa kuileta hii mada pili pata mbili baridi pale kwa n ani tena.....ntarudi kulipa bill baadae. thumbs Up!!!!
 
Unapomtokea mwanamke lazima ujiweke juu sab... wanawake wengi wanapenda kuwa na mahusiano na watu maarufu, wenye pesa, nk..
 
Tatizo nyie wanawake bila kudanganywa hampatikani.......... Mnapenda kuongopewa ndio mkubali....... Kwani SEDUCTION maana ake nini? Hahahahahaaaaa! Uzuri mwisho wa siku si utaujua ukweli na ndo sasa utaamua muachane au muendeleeeee!
 
Yaani leo mmetuamulia hakuna shaka lakini upepo nao hugeuka na mambo huwa yanabadilika
 
mmmh!! na kinyume chake pia............Kuna wengine hawapatikani hadi wadanganywe!!!
 
nimepata mbinu...kuna dada m1 ni HR wa NMB, naenda kumtokea leo. ntajishusha sijikwezi tuone. ni research tu ila akikubali naendeleza libeneke
 
ahh makontena yangu bandarini hayajatoka

yule atak kunilipa m8 zangu....
ahh yule mpumbavu tu bila mimi asingepaweza mjin apa...


ahhhh mavx yangu...ile hammer sjui vip...
Bila kuambiwa hivyo hamuelewi somo....
Hiyo njia inatumika sana kwa sababu inaonekana wanaume wanafanikiwa sana kuwapata wale wanaovutiwa nao..
Kuna mmoja nilimsikia katika daladala anaongea na binti kwa simu..........oooh naelekea eapoti hivi sasa naenda Uholanzi, kupitia J'berg, Dubai. baada ya wiki tatu unitafute nitakuwa nimerudi. Jamaa mwenyewe kapanda daladala ya Ubungo Kibamba, anaelekea kibamba usiku...
 
Yaani wanaume wa dot com eti mimi naongea lugha zote duniani kiswahili tu ndo kinanipiga chenga loh?

kiingereza kihispania kifaransa. kichaga tunasahau kabsa.. hivi bebii siulikuwa unatafuta mchumba.
 
ahh makontena yangu bandarini hayajatoka

yule atak kunilipa m8 zangu....
ahh yule mpumbavu tu bila mimi asingepaweza mjin apa...


ahhhh mavx yangu...ile hammer sjui vip...
Sasa Rose mtu wangu kwa nini unapata shida na wavimba macho, hebu njoo huku kwangu nikupe raha. Naagiza Rolls Royce yangu ije kukuchukua sasa hivi.
 
Tatizo nyie wanawake bila kudanganywa hampatikani.......... Mnapenda kuongopewa ndio mkubali....... Kwani SEDUCTION maana ake nini? Hahahahahaaaaa! Uzuri mwisho wa siku si utaujua ukweli na ndo sasa utaamua muachane au muendeleeeee!
Mkuu ndiyo maana nikamuuliza mleta mada kama ni me au ke.
 
Back
Top Bottom