Minister of Energy & Mineral Resources, William Mganga Ngeleja SLEEPING in 2011 EITI Meeting

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,906
22,036
Nilihisi mapepo yako bungeni Dodoma tu kumbe hadi Ufaransa? Kazi ipo

TUMEZOEA KUMWONA MH KOMBA AKISINZIA NA KUKOROMA DODOMA SASA HUYU SIJUI TUMWITE JINA LA MNYAMA GANI


03_11_8cu1nz.jpg


Jamani,

Hiyo ni Kamera tu alikaa upande akachukua wakati mheshimiwa ameinama. Au wakati anapiga kope (eye twinkling). Thread inataka kuleta uchochezi usio na maana. Swala la kujadili ni hili lifuatalo:

Raisi Kikwete akifuatana na Membe (MB) na Ngeleja (MB) walienda Ufaransa kuhudhuria mkutano ulioandaliwa na EITI (Extractive Industries Transparency International) yaani mtandao wa kimataifa unaotetea uwazi kwenye mapato yatokanayo na rasimali chimbwa yaani Madini, vito, gasi na mafuta. Mzee Bomani ndiyo anayosimamia chapter ya Tanzania.

EITI Tanzania kama itasajiliwa kisheria watatakiwa kila mwaka kutangaza (to publish) na kuanisha mapato yote yanayotokana rasilimali chimbwa inayopata nchi. Sasa hivi tuko kwenye mchakato wa Tanzania kuwa mwanachama wa EITI kama tutatimiza masharti ya kuwa wazi kwenye mikataba na mapato.

Mwaka jana bunge lilipitisha sheria ya madini iliyopingwa sana na upande wa upinzani kwa sababu ya vipengele vya usili katika mikataba na sector hii. Lakini kwa sababu wabunge wa chama chetu ni wengi ikapitishwa. sheria inatoa hata adhabu kwa yule atakaye divulge siri zinazohusiana na mikataba hii. Hivyo basi kabla ya JK kwenda Ufaransa alitakiwa kwanza kuyafanyia mambo haya ya msingi kwanza ili watanzania wawe huru kua access mikataba hii na kujua hasa nini kimewekwa humu. Ngoja niwamegee kidogo tu mapato tuliyopata kutokana na rasilimali chimbwa so far:

Aina ya mapato kwa nchi Shilingi za kitanzania Revenue collected on behalf of the government (hizi ni PAYE na NSSF) 66,129,144,000.00 Total Taxes (yaani Corporate tax, withholding tax, SDL (Skill development levy), import duty, fuel levy ni zero yaani hawalipi na sector specific taxes yaani (loyalties - Mrahaba wa aslimia tatu kama matusi vile?, License na permit fees, mineral concessions, kaprofiti wanakopata TPDC, Local government levy - Zile dollar laki mbili wanazolipwa kule Tarime, Geita na Kahama na devidends inayopata serikali kwenye makampuni kwa sasa hivi ni sifuri) 62,293,938,000.00 Jumla kuu 128,423,082,000.00 Asilimia ya mapato kutoka na kodi ya wafanyakazi wa rasilimali chimbwa 51% Mchango wa kodi za makampuni moja kwa moja 49%

*data hizi ni kwa mwaka 2008: nazo zimepatikana kwa taabu kweli
*Kile wanachodai makampuni wamelipa kwa serikali na kile serikali inachokiri kulipwa vinatofautiana. Sijui wamekunywa? Mtajaza wenyewe, sie tunasonga mbele. Naomba kuwasilisha wana JF.
* Yaani kodi ya wafanyakazi wa migodini na kwenye gas eti ndiyo tegemeo kubwa la mapato ya serikari.
Kwenda ufaransa ni aibu tupu, sijui wanafukuzia masurufu ya safari tu hawa!
 
Huyo kazoea kukesha club za usiku, 84 Dodoma kama sebuleni kwake vile sasa hapo jana yake sijui alikeshea club gani huko ufaransa
 
mmmmhhhhhhhhhhh!!!!!!!!!! tena kakaa jirani na Mkwere
 
Loh, ndio hii safari yao ya juzi tu ama?
Ila ndo wanavyotuwakilisha hapo walipo.
 
Maskini weeeeee! yaani huyo ndio waziri anayetuwakilisha watanzania, lol! sasa hapo akisikia watu wanapiga makofi na lenyewe litashtuka usingizini na kupiga makofi bila hata kujua nini kilisemwa, embu mwangalie na Rais wake, anajifanya yuko busy kusoma desa kumbe hamna lolote, sijui hawaelewi lugha inayozungumzwa hapo? Wenzao wako makini kusikiliza hoja wao wapo wapo tu!

Kwakweli CHADEMA endelezeni kazi nzuri mliyoianza, hawa hawastahili kutufikisha 2015, ni mzigo mzito kuendelea kuwa na viongozi wa namna hii.
 
Sorry, naomba nitoke nje kidogo. Of course hata huyo asiyesinzia naye amelala tu si unaona kabisa anaangalia picha tu. Well, nitaomba kusaidiwa in case hii obsrvation yangu si sahihi.

Kwa haraka haraka simwoni rais mwingine zaidi ya our cheap president. Hivi kwanini hakumwacha huyo anayelala hapo aende peke yake? Hiki kikao si cha marais I'm sure waandaji hawakumtarajia ndio maana unaona wamemrundika hapo maskini. Its high time rais wetu awe na aibu kidogo mbona alishasafiri sana alipokuwa minister hachoki tu? Mbali ya hasara tunayopata lakini pia tunonekana hamnazo sisi wote inakuwaje rais anakuwa na muda mwingi hivi wa kuzurura?

Hii nchi inaoboa sana.
 
Mbona hata hapo mkwere anazunga tu na kijitabu wala hasomi kitu wanatalii hao, angalia wenzao wanavyoangalia mbele na kusikiliza kinachosemwa wenyewe haka mkwele anatizama kacheki kako kwenye kitabu hicho na kuwaza mbona jamaa wamenipunja hawa?
 
hakuna rais hapo wenzie wametuma mawaziri yeye anapenda kwend akwenda ulaya basi ndo tabu tupu ....
 
Ngeleja: ''Dah nji yangu ipo gizani, ,huyu nae anadesa playboy magazine, Chadema nao wametukalia kooni, aagh ngoja nlale manake kusikiliza hii lugha ''bonyzwiii'' haipandi kabisa yani'' krooooooo,krooooooo!!!!!
 
.....Ngeleja hajalala, ila 'ANATAFAKARI' kwa makini kile kinachozungumzwa pale!
 
03_11_8cu1nz.jpg


Mkao huu unaonyesha wazi kabisa ni conference ya kawaida ambayo hata wahudhuriaji wake si mawarais au mawaziri bali executives wa taasisi, na sitoshangaa kuwa they are not even senior executives. Ingekuwa ni marais ingekuwa Summit na mkao wake usingekuwa wa namna hii kama vile watu wanavunja kamati ya harusi.

Nimejaribu kumwangalia Ngeleja strait kati ya ngeleja na jamaa aliye kushoto kwake kuna mzungu kama vile anamwangalia JK, sijui jamaa anawaza nini, kumwona rais wa nchi kubwa kama TZ eti anahudhuria kikongamano cha junior officers kama hicho. Jk is not even there, hicho kitabu anachosoma ........ni kama hakihusiani na mkutano huo maana hakuna mwingine aliyeshikilia kitabu kama hicho.

Ngeleja seems to be bored, alichokikuta sicho alichotegemea. Imagine waziri unaambiwa utakutana na maprofessor badala yake unakutana na wahudumu wa ofisi. Ndicho anachowaza poor Ngeleja, wala hajasinzia hapo. anajisikia aibu mno maana inaonekana hakuna hata waziri mwingine yeyote kutoka nchi zingine, ni yeye tu. Poor him
 
Si unaona hata mjumbe aliyekaa nyuma ya aliyeko kushoto kwa Ngeleja anavyomshangaaaa?...ni sawa na kuanzisha mradi wa kufunga MIKOKOTENI speed Govern
 
hivi hicho kitabu kimeandikwa kwa kiswahili ..??maana najua kama ni kingereza basi hapo mkwere haelewi kitu?
 
Back
Top Bottom