Minister belittles link with JK's son

Huyu jamaa ni mwongo mkubwa kabisa.....

moja Masha kalidanganya Taifa kuwa kila mwaka wanaajiri wanafunzi watano wanaofanya vizuri hapo kwenye hiyo firm yao, huo ni uongo kabisa, mimi nilikuwa mmoja wa watu niliyekwenda hapo na Ridiwani, mbona mlimchukuwa Ridhiwani peke yake????

.... sasa iweje kuwa eti Ridhiwani aliajiriwa kabla hata ya baba yake kuonyesha dallili za kuwa President???
Mkuu unauhakika na hilo Jina ulilolitaja hapo juu??? si-dhani kama huyo jamaa aliwahi kuajiriwa na Masha Advocates.kama KWELI ulikwenda kudondosha CV hapo mahala,basi hebu tupe Jina sahihi!!
 
Mwisho, usijisifie sana wewe, umeongoza kampuni toka 1991, kwa ufisadi na mmekuwa wezi mkishirikiana na Kikwete kuujumu uchumi na kupeana nafasi kwa kujuana, hivyo sio kwamba wewe unachapa kazi, lo, jamaa analipa fadhila

Mkuu Babah,

Heshima mbele, hii haijakaa sawa, mengine sina uhakika,

1. Masha, alishwahi kuwa Secretary wa Shirika la Oxygen, na baadye akawa director wake, kama kweli ni fisadi basi tungesikia toka akiwa huko ufisadi wake.

2. Amekuwa waziri mdogo wa Nishati, nafikiri hapo ndipo tungemsikia kwenye Richimonduli, lakini Mwakyembe hakumgusa kabisaa meaning kuwa yuko safi.

3. Toka awe waziri kamili wa ndani, hata mwezi hajamaliza, sasa hizi tuhuma zako mkuu mbona nzito sana na hazilingani na Masha kabisaa mkuu.

4. Huko IMMA, ninakubaliana naye kuwa huwa wanaajiri wanafunzi mbali mbali, ninawafahamu wengi waliowahi kuajiriwa hapo ambao baba zao wala sio wakubwa wa nchi.

Ninaomba niseme hivi, Masha ni kijana mdogo sana mwenye shule ya kutosha, na pia ameonyesha uwezo wa kuongoza na ni kichwa pia, maana kijana ana Masters ya sheria ya Georgetown DC, na anayo Bar ya sheria ya New York ambayo hata mtoto wa JFK ilimshinda aliirudia mara tatu lakini huyu kijana Masha aliifanya mara moja tu, hivyo angeweza kubaki huko na kuwa Lawyer mkali na kuishi maisha mazuri kuliko anayoishi sasa, lakini akaamua kurudi nyumbani kulijenga taifa lake,

I mean sina uhakika na base ya mashambulizi yako kwake, lakini nina wasi wasi kuwa humtendei haki kabisa mkuu, I know the kid bro inasikitisha sana kuona kijana mchapa kazi na muadilifu kama huyu, akishambuliwa namna hiii, huku ripoti ya Mwakyembe ikiwashika mpaka katibu wa Nishati, lakini yeye waziri mdogo akiachiwa bila ya kuguswa kabisaa, ninasema mara nyingi kuwa viongozi wazuri na wadilifu tunawafahamu, na mafisadi pia tunawajua, tusiowajua habari zao ziwekwe kwa uwazi na ukweli,

Unless, kuna habari zingine zaidi za ubaya wa Masha, kwa kweli mkuu hizi charges zina walakini mkuu, kulingana na hukumu nzito ulizomhukumu hapo juu, kwamba ati ni mwizi au amepewa kazi kwa kujuana, kwenye hayo naomba kutofautiana na wewe mkuu, Masha ni mbunge wa Nyamagana, uwezo wa uongozi anao maana amekuwa kiongozi akiwa na umri mdogo sana, na hata sasa bado ni kijana mdogo sana, na anaonyesha kuwa atatusadia sana kitaifa na mawazo yake ya kimaendeleo na hasa sera za ki-capitalism, ambazo anaoneakan kuzi-master sana, kwa hiyo mkuu tumpe tu nafasi atuongoze na akosolewe pale akikosea.

Ahsante Mkuu.
 
Baba H mkuu samahani kidogo tuanze na majina, kwanza ni Lawrence siyo Rawrence, pili ni Ridhiwani siyo Ridiwani hapo tu naweza kuhisi sababu ya wewe kutoajiriwa kwenye hiyo kampuni!

Sasa kwenye suala la madai ya ufisadi dhidi ya Masha, sidhani kama kuna ushahidi wowote wa hilo, the close you may come up with itakuwa ni conflict of interest alipokuwa Naibu Waziri wa Madini na Nishati wakati huo huo kampuni yake ikiwa mawakili wa AFGEM na akiwa na hisa huko, unless kuna mengine nisiyoyafahamu.
 
BabaH i want you to be in my campaign. Wamarekani weusi wana sema "damn boy".

I love that analysis, you brake down to the bones. Jakaya anataka kutuchezesha kizungu mkuti, anachukua so called new faces kutoka kwenye kapu lake la mafisaidi wadogo wadogo.

Ridhwani alikuwa kwenye deal la Richmond, nawasiliana na vijana wangu wanajua kabisia ni part gani alihusika, after i get all the facts I will put them here in JF so we can Xray them togather.

BabaH, get some more facts, then we gonna craete 100 reasons why Ridhiwani is not clean.
 
FMES,
Ni kweli kuwa Masha hakuguswa na kamati ya Mwakyembe na so far hakuna ushahidi wowote unaomhusisha na ufisadi hadi sasa. Hata hivyo, kampuni ambayo yeye ni mmoja wa wamiliki wake IMMA kuelezwa kuwa ndiyo iliyohusika na kufanikisha usajili wa kampuni ya kifisadi ya Deep Green, na ukweli kuwa miongoni mwa wamiliki wa Deep Green ni partiners wawili wa Masha kunaleta wingu la mashaka.
 
jamani tumpe mda huyu mtu..bado mapema mno..kashfa kama hizi zinamvunja mtu moyo wakuendelea ku chapa kazi na kibaya zaidi kama ni za uongo
 
Jamamni, mbona mambo yako wazi sana? Mnamlaumu babah kwa kutokuelewa tu. Labda kwa sasbabu ametumia lugha chafu. Tafuteni gazeti la Mwanahalisi la juzi jumatano. Wala hutakuwa na haja ya kuhoji, ukweli always hujitenga! Kuna element za ufisadi hata kwa mtu asiyekwenda shule.
 
haya naona mapya sana na hadi naona nami niingie niseme jambo ambalo nafikiri nalifahamu na ningependa wana jf tuchangie mawazo.ninazungumzia kuhusika kwa huyu ridhiwani maana ni muendelezo ambao leo tunao.

kwanza niwape pole watanzania kwa haya wanayoyaona ya ufisaidi ambao magazeti na vijiwe vyetu vimeamua kuweka wazi huku tukisubiri report za ukweli toka kwa wale tuwaitao wasema ukweli. mie sijui kama ni waandishi wa magazeti, kamati za bunge au mwanangu mwakyembe.

jambo langu , ni kwanza nimuweke sawa huyu aliyepost thread hii. inaonyesha kwa upande wake hajafurahishwa na ridhiwani kupata kazi hapo immma na yeye kuachwa. lakini nataka nijue je kwani ni lazima kuajiriwa wewe na yeye aachwe na pengine nani mwenye maamuzi ya kuajiri katika sekta binafsi?

la pili ambalo nataka mnisaidie kimawazo, inakuwaje tunazungumza ufisaid kwa kuhisi. mie nataka nijue , ni wakati gani mtu anaweza itwa fisadi na ni vipi iwe fisadi bila kuwa na vigezo na kama vigezo vipo ni kwa vipi ridhiwani anahusiana navyo.

mie nachukia sana uharamia lakini pia ninasimama katika misingi ya haki, ambayo siku zote inasisitiza kuwa ..........hukumu mtu baada ya kuridhika na ushaidi wa kutosha uliotolewa kwamba amefanya kosa fulani.....! inakuwaje leo hii tunasema fisadi na ushahidi hatuna.kama munao ni upi ambo unamuunganisha kijana huyu ,naomba tuuweke wazi.

(nazungumzia kipande hapo juu).....mfano ndg johnson lukaza tulipomuhusisha na ufisadi , nafikiri ni kwa sababu yeye ndiye mmiliki wa kampuni ya proin na kwamba anahusika moja kwa moja na shughuli zote za kila siku za kampuni yake na kiasi kama kile cha fedha kinapoingia ni nlazima hajue.leo hii inakuwaje kwa kijana huyu.

jengine ambalo linanitatiza ni kuhusiana na haki za msingi ambazo mtu anakuwa nazo katika jamhuri hii ya tanzania. ninaanza kuona kwamba tunaweza kuwa na mambo ambayo sio ya kawaida. ukiukwaji wa wazi wa ibara za katiba yetu ya jamhuri ya muungano unaanza.yawezekana vipi mtu asiwe na haki ya kufanya kazi kama inavyopingwa na ibara ya 11 ya katiba yetu?

mh. waziri ameeleza kwamba huyu bwana aliingia kama intern na baadae wakamuajiri. sasa nini tatizo wakati unaambiwa kwamba ni sera ya kampuni kuajiri huku kipaumbele kikitolewa kwa wale intern .nashindwa elewa kwamba watu wana lalamika kuwa kaajiriwa pale...nyie mlitaka nini?

ni vigumu kuwaelewa au kuwaeleza lakini wengi mnajua tunao uhuru wa kutoa mawazo lakini sio kuhukumu moja kwa moja au kutoa tafsiri ya jambo.ukweli ni kwamba ridhiwani anafanya kazi immma kama muajiriwa na immma ni kampuni ambayo inawaajiriwa wengi zaidi ya 20 na maboss zao ni wako wanne. hakuna shaka katika ili kwamba anafanya kazi lakini sidhani kama kufanya kazi pale kunaweza mfanya naye fisadi. kama hii ni maana basi tuangalie BOT,Wizara ya maliasili na utalii, wizara ya miundo mbinu,n.k.waajiriwa wote pale ni mafisadi.

hivi huyu kijana anatakiwa afanye nini?maana akifanya jambo lolote mtasema. hadi lini.basi tumsaidieni mawazo nini afanye?

kweli inasikitisha ndg zangu maana sasa itabidi watu tuanze angalia kampuni ambazo hazina historia ya ufisadi bila kuangalia namna kazi inavyo fanyika. vigumu kutambua lakini inawezekana kabisa.

mwisho nisingependa kwenda kwenye sheria maana mie sio mwanasheria ila nataka sema kitu kimoja. ninavyojua mimi,moja ya kazi ya wanasheria ni kusajiri kampuni na pia kulipwa gharama fulani za kazi baada ya usajiri. mh. waziri amezungumza wazi na kwamba sidhani kama kuna tatizo.kama lipo nafikiri tumtafute yule mwengine alisemwa kuwa ni msimamizi au muongeaji wa kampuni, atayasema. vipi kuhusu kuhusika kwao.

ninavyofikiri au kushauri mimi haipendezi kufanya personal attack kwa mtu.ukweli wa mambo utajulikana.

lakini pia tusisahau kuna usemi wa wahenga unasema......chokochoko uzaa jambo.tusikilize nini kinakuja.

nakaribisha mawazo .aksante sana.
 
kwa elimu yake na sifa nilizowahi kuzisikia kutoka kwa watu wanaodai kumjua, sikutegemea yeye kama waziri kuitisha press conference na moja ya ajenda ni kuijibia maswali kampuni binafsi ambayo alidai ilishajing'atua kwenye shughuli za uendeshaji wa kila siku pindi alipoingia siasa. kaeleza yote mpaka hatua za kulitia adabu hilo gazeti, mbaya zaidi, mwisho anasema yeye sio mtendaji wa hiyo firm kwahiyo anawaachia watendaji. hv hii firm haina PR? hivi alikua anaongea kama masha au waziri, au vyote kwa wakati tofauti.
otherwise nampa salute kwa kuwa mbali na richmond, ufisadi mwingine siujui ingawa ana hisa tanzaniteone ambayo inatandika risasi wana apollo kila uchao.
 
mh. waziri ameeleza kwamba huyu bwana aliingia kama intern na baadae wakamuajiri. sasa nini tatizo wakati unaambiwa kwamba ni sera ya kampuni kuajiri huku kipaumbele kikitolewa kwa wale intern .nashindwa elewa kwamba watu wana lalamika kuwa kaajiriwa pale...nyie mlitaka nini?

ni vigumu kuwaelewa au kuwaeleza lakini wengi mnajua tunao uhuru wa kutoa mawazo lakini sio kuhukumu moja kwa moja au kutoa tafsiri ya jambo.ukweli ni kwamba ridhiwani anafanya kazi immma kama muajiriwa na immma ni kampuni ambayo inawaajiriwa wengi zaidi ya 20 na maboss zao ni wako wanne. hakuna shaka katika ili kwamba anafanya kazi lakini sidhani kama kufanya kazi pale kunaweza mfanya naye fisadi. kama hii ni maana basi tuangalie BOT,Wizara ya maliasili na utalii, wizara ya miundo mbinu,n.k.waajiriwa wote pale ni mafisadi.

hivi huyu kijana anatakiwa afanye nini?maana akifanya jambo lolote mtasema. hadi lini.basi tumsaidieni mawazo nini afanye?

kweli inasikitisha ndg zangu maana sasa itabidi watu tuanze angalia kampuni ambazo hazina historia ya ufisadi bila kuangalia namna kazi inavyo fanyika. vigumu kutambua lakini inawezekana kabisa.

mwisho nisingependa kwenda kwenye sheria maana mie sio mwanasheria ila nataka sema kitu kimoja. ninavyojua mimi,moja ya kazi ya wanasheria ni kusajiri kampuni na pia kulipwa gharama fulani za kazi baada ya usajiri. mh. waziri amezungumza wazi na kwamba sidhani kama kuna tatizo.kama lipo nafikiri tumtafute yule mwengine alisemwa kuwa ni msimamizi au muongeaji wa kampuni, atayasema. vipi kuhusu kuhusika kwao.

ninavyofikiri au kushauri mimi haipendezi kufanya personal attack kwa mtu.ukweli wa mambo utajulikana.

lakini pia tusisahau kuna usemi wa wahenga unasema......chokochoko uzaa jambo.tusikilize nini kinakuja.

nakaribisha mawazo .aksante sana.

I like your analysis, it seems your educated enough to derive that conclusion. Twende hoja kwa hoja.
Kwanza kuna kitu kinaitwa "Conflict of Interest" kwenye bishara au serikalini. Mgongano wa maslai ni swala nyeti sana, sasa kama baba yangu ni Mkuu wa Nchi, na Mwanae anafanya kwenye firm ambao ina wateja kadhaa nchini. Jee swali niliweke kwako jee ni wateja wa aina gani wapo chini ya Firm hiyo? Jee wateja hao wana deal na serikali au watu binafsi? Na kama wana deal na serikali how will you assure me that Ridhiwani will not campaign for them after clocking out? Hizi ni assumption ambazo zinazabishwa na swala zima la mgongano wa maslahi.

Pili baba yako anapokuwa raisi then your public figure, WE(wananchi) have a right to X-ray every movement your making. Why? Because My tax, Your tax and everybody Tax finance his life from kindergaten to Law School. We have every right on earth to even ask where did you get the money to take your fiance for a date.

It is public figure stupidy, you either hate it or like it. Mimi binafsi nilishaomba data za huyu kijana ili nimu X-ray alisoma wapi, kwa nini kulikuwa na uvumi wa yeye kuhusika Richmond, Jee ni kwelie Mh. Jakaya alimuondoa kwenye deal ya Richmond baada ya kutoka US kwenye summit.

Public figure ina faida na hasara zake, faida ni kuenjoy easy ride on everything, hasara ni kuanikwa pindi utakaapoacha fingure print.

So, Kuajiriwa kwake kwenye kampuni inayodeal na makampuni yanafanya biashara na serikali kwa njia yoyote ile ni mgongano wa maslai, na ilo ni MWIKO kwa kampuni yenye "ETHIC CODE"...
 
kwa elimu yake na sifa nilizowahi kuzisikia kutoka kwa watu wanaodai kumjua, sikutegemea yeye kama waziri kuitisha press conference na moja ya ajenda ni kuijibia maswali kampuni binafsi ambayo alidai ilishajing'atua kwenye shughuli za uendeshaji wa kila siku pindi alipoingia siasa. kaeleza yote mpaka hatua za kulitia adabu hilo gazeti, mbaya zaidi, mwisho anasema yeye sio mtendaji wa hiyo firm kwahiyo anawaachia watendaji. hv hii firm haina PR? hivi alikua anaongea kama masha au waziri, au vyote kwa wakati tofauti.
otherwise nampa salute kwa kuwa mbali na richmond, ufisadi mwingine siujui ingawa ana hisa tanzaniteone ambayo inatandika risasi wana apollo kila uchao.

Vkitina kuna kitu kwenye third world nation kinaitwa "dictatorship mind oriented", ndio maana alisema atalishughulikia gazeti, sio meet me at the court, NOOO nitalishughulikia. Did you read that? Ina maana kwa kutumia nguvu ya aina yoyote i will make sure that am going to protect mtoto wa bosi mpaka siku ya kiama.

Swala la Richmond bado nalifanyia kazi, i will conclude kama Ridhiwani alihusika au laaa. Maana kama aliusika meet me on Raia Mwema au Mwananchi.
 
Mkuu unauhakika na hilo Jina ulilolitaja hapo juu??? si-dhani kama huyo jamaa aliwahi kuajiriwa na Masha Advocates.kama KWELI ulikwenda kudondosha CV hapo mahala,basi hebu tupe Jina sahihi!!

Kampuni inaitwa IMMA ADVOCATES, hata Fatuma Karme (yule wakili aliyemtukana Hakimu Mkazi Kisutu ni mwajiriwa wake).

(Just to keep the records straight)
 
Baba H,

Ndugu yangu angalia usahihi wa maneno ---- kuna neno hapa --- mnaajiri ---- lakini kwenye post yako naona umeandika---- mnaajili.

hebu edit basi mambo yawe mswano.

end
 
Watanzania bwana! Yaani miaka 38 ni umri mdogo? Hivi umri wa kuishi kwa TZ
si ni miaka kama 45? Sasa iweje watu waone 38 ni kijana mdogo?

Najua marais kibao ambao walichaguliwa kuwa marais wakiwa na miaka chini ya 35, sasa sisi mtu kuwa waziri mpaka awe na miaka 50?

Masha kafanya kazi tokea 1991, ana uzoefu wa kazi miaka 17, bado ni kijana mdogo huyo?

Wamshambulie kwa mambo mengine lakini sio suala la umri.

Mimi nilikuwa najifikiria kwa TZ ni mkubwa, kumbe nikipewa ulaji kuna watu
wataona nimepataje kwa umri huu? Miaka zaidi ya kumi kazini, bado watu wanaona mtu huna uzoefu wa kutosha.

Acheni kutuletea mambo ya waziri Majivuno wa Kusadika "Weusi wa nywele za mshitakiwa, waonyesha kwa kiasi gani hana busara"
 
Nafikiri mashambulizi dhidi ya baba-H yanakosa base, hii inawezekana kwa kuwa wachangiaji wengi wanacomment maelezo yake na sio maneno ya Masha kwenye mkutano na waandishi wa habari.

Pamoja na sifa nyingi za Masha, binafsi nimepatwa na mshtuko kusoma kwenye gazeti kuwa ameitisha press conference, na moja ya ajenda kuu ni kusema kuwa Ridhiwani hakuajiriwa IMMA kwa kuwa ni mtoto wa Rais. Hakuna mtu mwenye wasiwasi kwanini Ridhiwani aliajiriwa. Wasiwasi wa watu ni kuhusishwa kwa Ridhiwani na kashfa ya Deepgreen ambayo Masha hakuizungmzia kwenye hiyo press conference. Ngoja nimpe Masha benefit of doubt, lakini nilichokiona kutoka kwa Masha baadaya ya hiyo press conference ni kuwa jamaa ni MSANII kama MAWAZIRI wengine tofauti yake yeye na wengine MASHA NI MSANIII ALIYEENDA SHULE.
 
Mkuu Babah,

Heshima mbele, hii haijakaa sawa, mengine sina uhakika,

1. Masha, alishwahi kuwa Secretary wa Shirika la Oxygen, na baadye akawa director wake, kama kweli ni fisadi basi tungesikia toka akiwa huko ufisadi wake.

2. Amekuwa waziri mdogo wa Nishati, nafikiri hapo ndipo tungemsikia kwenye Richimonduli, lakini Mwakyembe hakumgusa kabisaa meaning kuwa yuko safi.

3. Toka awe waziri kamili wa ndani, hata mwezi hajamaliza, sasa hizi tuhuma zako mkuu mbona nzito sana na hazilingani na Masha kabisaa mkuu.

4. Huko IMMA, ninakubaliana naye kuwa huwa wanaajiri wanafunzi mbali mbali, ninawafahamu wengi waliowahi kuajiriwa hapo ambao baba zao wala sio wakubwa wa nchi.

Ninaomba niseme hivi, Masha ni kijana mdogo sana mwenye shule ya kutosha, na pia ameonyesha uwezo wa kuongoza na ni kichwa pia, maana kijana ana Masters ya sheria ya Georgetown DC, na anayo Bar ya sheria ya New York ambayo hata mtoto wa JFK ilimshinda aliirudia mara tatu lakini huyu kijana Masha aliifanya mara moja tu, hivyo angeweza kubaki huko na kuwa Lawyer mkali na kuishi maisha mazuri kuliko anayoishi sasa, lakini akaamua kurudi nyumbani kulijenga taifa lake,

I mean sina uhakika na base ya mashambulizi yako kwake, lakini nina wasi wasi kuwa humtendei haki kabisa mkuu, I know the kid bro inasikitisha sana kuona kijana mchapa kazi na muadilifu kama huyu, akishambuliwa namna hiii, huku ripoti ya Mwakyembe ikiwashika mpaka katibu wa Nishati, lakini yeye waziri mdogo akiachiwa bila ya kuguswa kabisaa, ninasema mara nyingi kuwa viongozi wazuri na wadilifu tunawafahamu, na mafisadi pia tunawajua, tusiowajua habari zao ziwekwe kwa uwazi na ukweli,

Unless, kuna habari zingine zaidi za ubaya wa Masha, kwa kweli mkuu hizi charges zina walakini mkuu, kulingana na hukumu nzito ulizomhukumu hapo juu, kwamba ati ni mwizi au amepewa kazi kwa kujuana, kwenye hayo naomba kutofautiana na wewe mkuu, Masha ni mbunge wa Nyamagana, uwezo wa uongozi anao maana amekuwa kiongozi akiwa na umri mdogo sana, na hata sasa bado ni kijana mdogo sana, na anaonyesha kuwa atatusadia sana kitaifa na mawazo yake ya kimaendeleo na hasa sera za ki-capitalism, ambazo anaoneakan kuzi-master sana, kwa hiyo mkuu tumpe tu nafasi atuongoze na akosolewe pale akikosea.

Ahsante Mkuu.


Katika historia yangu kwenye JF Es huwa hatetei kitu bila ya maslahi.Nampenda Es maana akiwa na maslahi yuko tayari kukusafisha hata kama anapoteza heshima yake . Nimefuatilia hili la Masha kuanzia kwa Ridhwan ES you are firm .Wakati wengine wanakata issue hii lazima wengine waingie tena pembeni kujua , kitu gani unacho simamia namna hii kwa nguvu zako zote .Maana uko kama wazungu wanakupa msaada wakijua wanataka nini.Nakupenda kwa hil lakini najiuliza pia kwa hili .
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom