napenda movie
JF-Expert Member
- Apr 24, 2015
- 521
- 457
Kuna kauli nimekua naisikia toka nikiwa mtoto mdogo sana na nadhani inatumika maeneo mengi sana hapa duniani kama sio dunia mzima.
Je, ni kwa sababu gani binadamu niliekamilika kiakili kimwili pia mkaniita mlemavu halafu mkaandaa hadi vitengo vinavyojidai eti vinalinda haki zetu ili tuishi na sisi kama binadamu. Kwani mimi sio binadamu, au kuwa na ngozi nyeupe tu hicho ndo kitu kinachowafanya mniite mie mlemavu.
Kwangu mimi nakataa na kauli kama hii sitaki kabisa kuisikia kwenye masikio yangu basi kwetu hapa Africa, yaani bara lenye wakazi wengi wenye ngozi nyeusi.
Mmekua na kupungukiwa kidogo kwenye kauli zenu sisi watu wenye ualbino mnatuita walemavu; sasa mimi binafisi nikijitizama nimekamilika kila idara na sina hata kiungo kilichopungua kwenye mwili wangu lakini mnaniita mlemavu. Mimi hii kauli sitaki kabisa kuisikia kwenye masikio yangu na mimi kuwa na ngozi nyeupe na macho yenye rangi tofauti na macho yako kisiwe kigezo cha kuniita mimi mlemavu.
Kama magonjwa, je ni nani hasa asiyeugua? Kwangu mimi hilo naona ni kama tusi.
licha ya kuwa na tetesi nyingi kwenye mitaa mara wanatuua au kukata viungo vyetu na kuvihusisha kwenye mambo ya kishirikina. Ni sawa lakini hao wenye ngozi nyeusi wao kwa wao huwa hawauani kwa sababu hizo hizo lakini kwetu sisi kwa nini tuitwe walemavu?
Mimi hii kauli sitakaki kabisa kuisikia
au kwani ualbino ni ugonjwa, laa hata kama ingeikuwa ugonjwa, unanifanya mimi mniite mlemavu?
Hii kauli mimi sitaki kabisa kuiskia.
@sahanpass1
#fikilia_sana
#mr_tiger
#presdent_laurent_sahan
#away_dous
#verspot
Je, ni kwa sababu gani binadamu niliekamilika kiakili kimwili pia mkaniita mlemavu halafu mkaandaa hadi vitengo vinavyojidai eti vinalinda haki zetu ili tuishi na sisi kama binadamu. Kwani mimi sio binadamu, au kuwa na ngozi nyeupe tu hicho ndo kitu kinachowafanya mniite mie mlemavu.
Kwangu mimi nakataa na kauli kama hii sitaki kabisa kuisikia kwenye masikio yangu basi kwetu hapa Africa, yaani bara lenye wakazi wengi wenye ngozi nyeusi.
Mmekua na kupungukiwa kidogo kwenye kauli zenu sisi watu wenye ualbino mnatuita walemavu; sasa mimi binafisi nikijitizama nimekamilika kila idara na sina hata kiungo kilichopungua kwenye mwili wangu lakini mnaniita mlemavu. Mimi hii kauli sitaki kabisa kuisikia kwenye masikio yangu na mimi kuwa na ngozi nyeupe na macho yenye rangi tofauti na macho yako kisiwe kigezo cha kuniita mimi mlemavu.
Kama magonjwa, je ni nani hasa asiyeugua? Kwangu mimi hilo naona ni kama tusi.
licha ya kuwa na tetesi nyingi kwenye mitaa mara wanatuua au kukata viungo vyetu na kuvihusisha kwenye mambo ya kishirikina. Ni sawa lakini hao wenye ngozi nyeusi wao kwa wao huwa hawauani kwa sababu hizo hizo lakini kwetu sisi kwa nini tuitwe walemavu?
Mimi hii kauli sitakaki kabisa kuisikia
au kwani ualbino ni ugonjwa, laa hata kama ingeikuwa ugonjwa, unanifanya mimi mniite mlemavu?
Hii kauli mimi sitaki kabisa kuiskia.
@sahanpass1
#fikilia_sana
#mr_tiger
#presdent_laurent_sahan
#away_dous
#verspot