"Mimi nitakuwa wa mwisho kupiga kura kumwondoa Mhe. waziri Mkuu"

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
"Mawaziri waliotuhumiwa wapo, wapime na waamue jinsi gani watamwokoa Waziri Mkuu, Mimi nitakuwa wa mwisho kupiga kura kumwondoa Mhe. waziri Mkuu, ni mapema mno kumhukumu Mhe. Waziri Mkuu wakati waoahusika wapo" - Mhe. Mtutula Abdallah Mtutula Mbunge wa CCM Tunduru (CCM) akizungumza leo asubuhi tarehe 20.04.2012 katika kipindi cha Jambo TBC1.

Maoni yangu:

Msitarajie lolote kutoka kwa wabunge wa CCM, wengi wanahisi chama ndicho kimewaweka pale na sio wananchi wa majimboni mwao. Wengi ni wanafiki kama akina Aggrey Mwanri na William Lukuvi..hawataki kukiri kuwa wao ndio chanzo cha mabadikili..wanakilalamikia chama chao kwa kulifiksha Taifa hapa lakini hawako tayari kunyosheana vidole na kuwajibishana wao wenyewe . wanamnunuu Mwalimuu kuhusu falsafa yake ya maendeleo ya "watu, siasa safi, ardhi na uongozi bora" lakini hawatekelezi hii kwa vitendo hasa inapofikia kupima maana ya 'uongozi bora".
 
Mawaziri waliotuhumiwa wapo, wapime na waamue jinsi gani watamwokoa Waziri Mkuu, Mimi nitakuwa wa mwisho kupiga kura kumwondoa Mhe. waziri Mkuu, ni mapema mno kumhukumu Mhe. Waziri Mkuu wakati waoahusika wapo- Mhe. Mtutula Abdallah Mtutula Mbunge wa CCM Tunduru (CCM) akizunguzmza na Jambo TBC laeo tarehe 20.04.2012- .
Huyo Mtutula hana vision kabisa. Nasikia ni mchawi wa kutisha huyo mbunge je ni kweli?
 
Huyo ni mbunge asiyesoma alama za nyakati ndio maana yeye muda wote analinda status quo tu ya serikali hii. Nguvu ya umma itammaliza huyu kupe.
 
step ya kwanza ni kumpa zitto kura 70.step ya pili ni vonoco kwa waziri mkuu.sasa yeye anashindwa kumpa kura yake zito?
 
suala la uwajibikaji linaanzia kwa yule anayetuhumiwa kujiondoa mwenyewe katika uongozi, thereafter akishindwa kujiondoa mwenyewe basi mkubwa wake ana mamlaka ya kumsimamisha kwa manufaa ya umma.

Lakini jambo linapokuwa linagusa maslahi ya nchi kwa mapana zaidi basi hata huyo mkubwa anatakiwa naye kuwajibika hata kama hajahusika katika matumizi mabaya ya mali ya umma.

My take: uwajibikaji kwa nchi zetu za Afrika bado ni suala gumu na viongozi wetu hawalitilii maanani kwa manufaa ya taifa
 
Kwakuwa yeye Pinda ni kiongozi wa mawaziri bungeni, kwakuwa wasaidizi wake hao wamedhihirika kufanya ubadhirifu, kwakuwa wabunge wawawezi kuwawajibisha, kwa kuwa nae amesikia na kuthibitisha ubadhirifu huo, kwa kuwa nae ni mtoto wa maskini na "anauchungu" na nchi hii, basi namwomba atangaze kujiuzulu ili baraza la mawaziri liundwe upya na kama rais atamteua tena, akiwa na mawaziri wapya basi tumpime upya kama atatufaa tumrudishe.

Lakini akiendeleza kiburi cha wenzake, watatokomea wote!
 
Ni vizuri amekuwa mkweli mapema....
Zitto kachora mstari katikati, mwisho wa siku tutaona nani ni nani.
Huyo wa kwanza kajibainisha mapemaaa.
Wengine!
 
Kufanya vibaya kwa mawaziri ni kukosa usimamizi mzuri wa kiongozi wao ambaye ni pinda. Hivyo pinda hana jinsi ya kukwepa kuwajibika kama kiongozi wao.

Kuna njia mbili za yeye kuwajibika: 1) kama msimamizi wa shughuli za serikali bungeni kumshauri jk (kama mteuzi wa mawaziri) awafukuze kazi mawaziri wanaoipeleka nchi pabaya; 2) yeye mwenyewe (pinda) aanze kuondoka ili "automatically" na mawaziri wengine watalazimika kuachia nyadhifa zao kwa mujibu wa katiba na baraza jipya la mawaziri litaundwa.

Kwa kifupi pinda hana namna ya kukwepa kuwajibika katika madudu yanayofanywa na mawaziri wa jk.
 
Kufanya vibaya kwa mawaziri ni kukosa usimamizi mzuri wa kiongozi wao ambaye ni pinda. Hivyo pinda hana jinsi ya kukwepa kuwajibika kama kiongozi wao. Kuna njia mbili za yeye kuwajibika: 1) kama msimamizi wa shughuli za serikali bungeni kumshauri jk (kama mteuzi wa mawaziri) awafukuze kazi mawaziri wanaoipeleka nchi pabaya; 2) yeye mwenyewe (pinda) aanze kuondoka ili "automatically" na mawaziri wengine watalazimika kuachia nyadhifa zao kwa mujibu wa katiba na baraza jipya la mawaziri litaundwa. Kwa kifupi pinda hana namna ya kukwepa kuwajibika katika madudu yanayofanywa na mawaziri wa jk.
Umenena kweli Mkuu. Pinda anatakiwa kujiuzuru yeye ili automatically na hao viwavi wengine waondolewe. Pinda ame-prove failure ktk kuwasimamia mawaziri, bora ya Mh. Lowassa.
 
Huyo Mtutula hana vision kabisa. Nasikia ni mchawi wa kutisha huyo mbunge je ni kweli?
Shida ya viongozi waliozoea kulindana huwa hawaoni zaidi ya Waziri Mkuu...hawaoni ni jinsi gani ameshindwa kuwajibika na kuiwajibisha serikali yake na mawaziri wabadhirifu. Kama yeye si mbadhirifu ameshindwa nini kuwachukulia hatua hao wezi?
 
Shida ya viongozi waliozoea kulindana huwa hawaoni zaidi ya Waziri Mkuu...hawaoni ni jinsi gani ameshindwa kuwajibika na kuiwajibisha serikali yake na mawaziri wabadhirifu. Kama yeye si mbadhirifu ameshindwa nini kuwachukulia hatua hao wezi?
Pinda ni kansa ndani ya serikali yetu, anatakiwa kuwajibishwa ili kuinusuru nchi yetu dhidi ya hawa viwavi. Ni lege lege mno!
 
Pinda anatakiwa asome alama za nyakati ameshindwa kusimamia wajibu wake kama WM ni vema sasa kama atajiuzuru kwa manufaa ya umma, asisubiri kupigiwa kura.

Tatizo viongozi wetu wa kiafrika ni kupe wa madaraka.
 
Pinda ni kansa ndani ya serikali yetu, anatakiwa kuwajibishwa ili kuinusuru nchi yetu dhidi ya hawa viwavi. Ni lege lege mno!
Kansa ni JK bana. Hawa wote wameambukizwa tu. Awajibishwe ila kichwa cha nyoka bado kipo hai.
 
Wakati umefika kwa wana Tunduru kuona kuwa Mtutura hafai. Kwa hali ilivyofikia haiingii akilini kwa Mbunge makini kuongea vile ili kuendeleza ulaji.

Anyway sishangai kwa wanamagamba wengi wapo hivyo, na naamini watakuwa tayari kupinga kumwajibisha Waziri Mkuu na kuendelea na unafiki wao!

Ndugu zangu wa Tunduru najua bado hamuelewi zaidi ya CCM amkeni mufanye mabadiliko.
 
jamani hebu tusubiri tuone mpaka kufikia leo jioni zitto atakua kashapata sign ngapi.
 
Back
Top Bottom