SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Kijuujuu unaweza ukafikiri tatizo la huyo dokta na mkewe ni interest tofauti.Naomba nikupe undaniHapo tatizo si elimu ila walitofautiana interest", kila mtu ana interest yake hata wote mkiwa maprofesa. Na kwa ufahamu wangu interest haifundishwi darasani
wa hili tatizo lililokumba ndoa ya dokta.Hiki kisa cha dstv kilitokea mwaka 2006.
Dokta alimweleza mkewe kwamba tamthiliya za Mambo Hayo na Tausi zilishaisha zamani hazipo tena.Mkewe
hakuamini, aliona mume anamyima raha makusudi.Mke akanyamaza lakini rohoniakahifadhi cheche ya hasira iliyolipuka na kuvunja ndoa mwaka 2008 mume alipomnunulia simu.
Kwa sababu ya uelewa mdogo wa mambo, kila akimpigia mumewe simu akaambiwa na mitambo yenye sauti ya kike:"Namba unayopiga kwa sasa haipatikani kwa sasa, jaribu baadaye" mke anafikiri sauti ni ya hawara wa mumewe!
Mume akirudi nyumbani mke analianzisha, mume anamfahamisha juu ya hiyo sauti inakotoka, mke anang'ang'ania msimamo na uelewa wake.
Mwishowe waliachana oktoba 2013 baada ya vikao vyingi vya usuluhishi kushindikana.
Daktari yu mbioni anatafuta mke.