Nitabakia CCM ila mwaka huu naamua kufanya maamuzi magumu. Kura yangu nitaipeleka kwa mtu mwengine, mbunge mwengine, simupi mugombea yeyote wa CCM, yaani ni maamuzi ambayo ninataka kuona kama tukishindwa itakuwaje, hao watakao shika uongozi watatufanyia nini, kama ni moto au pepo.
Nione viongozi wetu watakiendeleza chama chetu CCM au watatimkia kusikojulikana na kutuwacha wanachama wao gizani.
Uchaguzi huu kura yangu chama changu cha CCM hakitaiona kuanzia Rais hadi balozi wa nyumba kumikumi,naihamisha na kuiwekeza chama kingine. Ni majaribio ambayo kama mwananchi nina haki na zaidi napenda nione tutakaposhindwa sisi CCM itakuwaje chama kitakufa? Maswali ni mengi kuliko majawabu.
Na zaidi kura ni siri yangu na Mungu wangu, kwenye sanduku hakuna mjumbe wala tarishi ni mimi na sanduku na anaeshuhudia ni Mungu, siogopi kitu kuipeleka kura yangu popote pale ila sio CCM, ili nipate kujua hawa viongozi wetu tutakaposhindwa wataendelea kuwa nasi, au wanatutumia tu kwa wao kushibisha matumbo yao na kutufanya sisi kama ngazi, nahitaji kulijua hili na ili kulijua kwa undani ni kwa mwaka huu kuikosesha kura chama changu.
Shime wana CCM, hamna haja ya kurudisha kadi wala kuhama chama, mwaka huu tu fanya maamuzi magumu kuikosesha CCM chama chetu kura, ili tukwapime hawa viongozi wetu.
Nione viongozi wetu watakiendeleza chama chetu CCM au watatimkia kusikojulikana na kutuwacha wanachama wao gizani.
Uchaguzi huu kura yangu chama changu cha CCM hakitaiona kuanzia Rais hadi balozi wa nyumba kumikumi,naihamisha na kuiwekeza chama kingine. Ni majaribio ambayo kama mwananchi nina haki na zaidi napenda nione tutakaposhindwa sisi CCM itakuwaje chama kitakufa? Maswali ni mengi kuliko majawabu.
Na zaidi kura ni siri yangu na Mungu wangu, kwenye sanduku hakuna mjumbe wala tarishi ni mimi na sanduku na anaeshuhudia ni Mungu, siogopi kitu kuipeleka kura yangu popote pale ila sio CCM, ili nipate kujua hawa viongozi wetu tutakaposhindwa wataendelea kuwa nasi, au wanatutumia tu kwa wao kushibisha matumbo yao na kutufanya sisi kama ngazi, nahitaji kulijua hili na ili kulijua kwa undani ni kwa mwaka huu kuikosesha kura chama changu.
Shime wana CCM, hamna haja ya kurudisha kadi wala kuhama chama, mwaka huu tu fanya maamuzi magumu kuikosesha CCM chama chetu kura, ili tukwapime hawa viongozi wetu.