Mimi ni mtumiaji wa Vodacom. Nakatwa salio langu Tsh.100 ya huduma ya Mdundo bila ya ridhaa yangu

Gushleviv

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
3,437
5,146
Habari zenu Wakuu,

Mimi ni mtumiaji wa Vodacom. Hivi karibuni nimekuwa nikikutana na hali ya salio langu kukatwa kiasi cha Tsh.100 kila baada ya mida flani bila ya ridhaa yangu.

Nikiwapigia Vodacom wananiambia kuwa nakatwa salio sababu nimejisajili kwenye huduma ya "Mdundo". Na zaidi sasa naletewa hadi msg kuomesha kwamba nimejisajili na hiyo huduma.

Naomba kueleweshwa kama kuna yoyote mwenye uelewa juu ya hili suala.

Kwa mtazamo wangu hadi sasa naona kama ni wizi kumsajili mtu kwenye huduma bila ya ridhaa yake na bila kutoa elimu juu ya huduma hiyo.

Isije kuwa ujinga wa wengi unatumika kama fursa kwa wezi wachache.

Iwapo nitagundua kuwa nimeibiwa basi nitawafikisha mahakamani.

Asanteni.
 
Kampuni ninapofanyia kazi huwa nawekewa Airtime kila tarehe Moja. Sasa Juzi niliwekewa nikaja kuikuta imepungua kwa 60% wakati Sijapiga simu wala sikuweka hiyo simcard hewani! Nilivyowapigia customer service wakaishia kunipa pole na kuahidi kurejesha hela yangu lakini Hadi Leo siku ya Tatu kimya
 
Kampuni ninapofanyia kazi huwa nawekewa Airtime kila tarehe Moja. Sasa Juzi niliwekewa nikaja kuikuta imepungua kwa 60% wakati Sijapiga simu wala sikuweka hiyo simcard hewani! Nilivyowapigia customer service wakaishia kunipa pole na kuahidi kurejesha hela yangu lakini Hadi Leo siku ya Tatu kimya
Pole sana Mkuu, hawa jamaa ni wezi mno. Tusipochukua hatua tutaibiwa mno
 
Pia Mara nyingi natumiwa SMS za "umefanikiwa kujiunga na huduma...." Wakati sikujiunga. Inamaana wananiunga wenyewe bila ridhaa yangu
Dah, ni makosa makubwa sana. Mbaya zaidi hawa Customer care attendants nao kama hawaelewi kitu zaidi ya kupewa maagizo namna ya kujibu wateja. Ila huu ni wizi kabisaa. Nimejaribu kuingia leo kwenye website ya mdundo nakuta tayari nipo subscribed!
 
Ni mitandao yote mkuu. Halotel kila siku tunagomambana. Unakatwa salio, ukiuliza unaambiwa ulijiunga na huduma flani na wanakaza shingo kabisa eti hiyo huduma wao hawana uwezo wa kumuunga mteja.
Unabaki unashangaa. Anyways ndo nchi zetu hizi, kampuni inafanya uhuni Kama huo and nothing happens!
 
Ni mitandao yote mkuu. Halotel kila siku tunagomambana. Unakatwa salio, ukiuliza unaambiwa ulijiunga na huduma flani na wanakaza shingo kabisa eti hiyo huduma wao hawana uwezo wa kumuunga mteja.
Unabaki unashangaa. Anyways ndo nchi zetu hizi, kampuni inafanya uhuni Kama huo and nothing happens!
Mkuu nikueleweshe kidogo, hizo huduma mara nyingi kama siyo mara zote huwa hazitolewi na Mno(kampuni za simu kama Voda, Tigo na zinginezo). Kampuni binasi huwa zinaingia mkataba na hizo kampuni za simu ili kutoa hizo huduma, sasa hizo kampuni ndiyo huwa zinawaunga watu bila mtu husika kujua. Ukilalamika sana ndipo kampuni husika ya simu wanawapigia hiyo kampuni kuwa wakutoe kwenye hiyo huduma ila kifupi kampuni hizo za simu hazihusiki kutoa hiyo huduma japo wewe una haki ya kulalamika kwa kampuni ya simu kwani hujui nyuma ya pazia kuna kampuni gani inayofanya hayo. Asante
 
Pole sana.

Jamaa yangu alikua customer care alinambia ni utaratibu wa kuibia watu wanaiba sababu wanajua hamna hatua watachukuliwa.

Ukieka tu hela hizo huduma zinakata salio lako.
 
Habari zenu Wakuu,

Mimi ni mtumiaji wa Vodacom. Hivi karibuni nimekuwa nikikutana na hali ya salio langu kukatwa kiasi cha Tsh.100 kila baada ya mida flani bila ya ridhaa yangu.

Nikiwapigia Vodacom wananiambia kuwa nakatwa salio sababu nimejisajili kwenye huduma ya "Mdundo". Na zaidi sasa naletewa hadi msg kuomesha kwamba nimejisajili na hiyo huduma.

Naomba kueleweshwa kama kuna yoyote mwenye uelewa juu ya hili suala.

Kwa mtazamo wangu hadi sasa naona kama ni wizi kumsajili mtu kwenye huduma bila ya ridhaa yake na bila kutoa elimu juu ya huduma hiyo.

Isije kuwa ujinga wa wengi unatumika kama fursa kwa wezi wachache.

Iwapo nitagundua kuwa nimeibiwa basi nitawafikisha mahakamani.

Asanteni.

Pole sana mkuu. Huo ni wizi 100%.

Hakuna aliye juu ya sheria. Hiyo kampuni ni kuiburuza mahakamani.

Mimi sio mwanasheria lakini I hope Tanzania kuna kitu kinaitwa Class Action Lawsuit. Kampuni inayowaibia watu kwa njia hii inabidi ifundishwe adabu na ustaarabu.

Cha kufanya ni kutafuta wale wote wanaoingizwa kwenye huduma kama hizo bila consent yao ili waungane pamoja kufungua kesi mahakamani. Cha maana ni kuhifadhi ushahidi wote.

Binafsi Tigo walishawahi kuniunga kwenye huduma fulani mara mbili lakini wakanipa option ya kujitoa. Ila sikuishia hapo, niliwafuata ofisini kwao nikawaambia kabisa wakirudia tena nawafungulia kesi. Toka siku hiyo sijaona tena huo upumbavu wao.

Somebody has to say something. Somebody has to do something. Tusiishi kwa mazoea. Tusiishi nchini mwetu kwa unyonge.
 
Pole sana mkuu. Huo ni wizi 100%.

Hakuna aliye juu ya sheria. Hiyo kampuni ni kuiburuza mahakamani.

Mimi sio mwanasheria lakini I hope Tanzania kuna kitu kinaitwa Class Action Lawsuit. Kampuni inayowaibia watu kwa njia hii inabidi ifundishwe adabu na ustaarabu.

Cha kufanya ni kutafuta wale wote wanaoingizwa kwenye huduma kama hizo bila consent yao ili waungane pamoja kufungua kesi mahakamani. Cha maana ni kuhifadhi ushahidi wote.

Binafsi Tigo walishawahi kuniunga kwenye huduma fulani mara mbili lakini wakanipa option ya kujitoa. Ila sikuishia hapo, niliwafuata ofisini kwao nikawaambia kabisa wakirudia tena nawafungulia kesi. Toka siku hiyo sijaona tena huo upumbavu wao.

Somebody has to say something. Somebody has to do something. Tusiishi kwa mazoea. Tusiishi nchini mwetu kwa unyonge.
Kweli kabisa Mkuu, I gotta do something.
 
Naamini mtu akiweka tangazo hapo kwa wale waliounganishwa kwenye service bila consent zao, wengi watajitokeza. Baada ya hapo ni kuweka action plan to end this madness and daylight robbery once for all.
 
Kuna hii nyingi inaniuzi kutoka Vodacom ,kukata salio ukikosea menu Yani kwamfano ulikusudia kuandika *149*03# sasa wewe ukajichanganya ukaandika *148*03# au menu yeyote tofauti na menu yao .

Wanakata shilling 100 kwahiyo hapo unakuta zoezi la kujiunga kifurushi unachokihitaji linashindikana ,inabidi utafute vocha nyingine.

Hii kitu kwangu naona haijakaa poa kabisa
 
Kuna hii nyingi inaniuzi kutoka Vodacom ,kukata salio ukikosea menu Yani kwamfano ulikusudia kuandika *149*03# sasa wewe ukajichanganya ukaandika *148*03# au menu yeyote tofauti na menu yao .

Wanakata shilling 100 kwahiyo hapo unakuta zoezi la kujiunga kifurushi unachokihitaji linashindikana ,inabidi utafute vocha nyingine.

Hii kitu kwangu naona haijakaa poa kabisa
E bwana we!
 
Shida Nini huu mtandao kwa sasa ukiweka Salio ukija kuangalia baada ya siku mbili mbele unakuta limepungua
 
Back
Top Bottom