Ujue mmea wa maajabu Comfrey

Tutor B

JF-Expert Member
Jun 11, 2011
9,025
6,554
MMEA WA AJABU – COMFREY

Comfrey ni mmea uishio miaka mingi. Una umuhimu kama mboga zenye afya kwa familia, pia malisho bora kwa wanyama wengi. Majani ya mmea huu huweza kutengenezwa mbolea kwa ajili ya bustani. Pia mmea huu hutumika kwa tiba mbalimbali kwa binadamu.

Comfrey ni mmea uliopatikana katika mapori ya milima ya Kaukasus-Urusi. Pengine ndio maana ukapewa jina la kitaalam, Russian Comfrey. Mmea huu ulipelekwa uingereza-ulaya katika karne zilizopita na kutoka Uingereza ulisambazwa Canada, Amerika, Australia, New Zealand na Afrika.

Waingereza ndio walioleta hapa Afrika ya Mashariki. Mmea huu unaweza kuoteshwa sehemu yoyote ile ili mradi kuwepo na msimu wa mvua katika kipindi cha mwaka mzima. Kwa kuwa teknolojia imekua, mmea huu unaweza pia kustawishwa kwenye mabanda maalum maarufu kama greenhouse. Hii ndiyo sababu Comfrey inaweza kupandwa katika kivuli cha upenu wa nyumba au miti.

Comfrey ni mmea ujengao Protini upesi zaidi kuliko mimea mingine iliyopo. Zaidi ya protin una viini muhimu vya vitamin na hasa kiasi cha juu zaidi cha vitamin B12 ambayo ni muhimu kwa ujenzi wa seli mwilini.

Kwa maana hii mmea huu unafaa sana kutumiwa na wenye matatizo ya Sickle Cell, Sickle Cell hushambulia chembechembe za damu. Pia kwa kiasi ni ugonjwa wa kurithi. Sehemu zenye ugonjwa wa Malaria kwa wingi ndio huathirika zaidi. Unatumia majani, na pia unaweza kuchanganya na mchicha, Chinese, Swiss Chard au mboga za maboga. Mchanganyiko huu ni muhimu sana katika kupambana na matatizo ya Sickle Cell. Unga wa majani uliokaushwa kwa kaushio la jua (Solar driers) ni muhimu kwa kuongeza protini ndani ya vyakula mbalimbali kama supu, mchuzi wa mboga (ugali), uji n.k

Pia majani mabichi au yaliyoanikwa unaweza kutumia kwa chai kwa kuongeza asali/ sukari, utaboresha afya yako kwa kinywaji hiki.

Magonjwa mengine yanayoponywa kwa kutumia Comfrey ni jeraha, michubuko na uvimbe wa miguu na mikono. Majani na mizizi ndivyo vinavyotumika kutengeneza dawa.

Comfrey ni malisho muhimu kuwakilisha samaki na wanyama. Ni malisho bora kwa wanyama wenye tumbo moja kama kuku n.k kwa sababu ina nyuzi kidogo zaidi kuliko mimea mingine. Inasaidia kujenga mifupa. Kwa ng’ombe wa maziwa hutoa maziwa mengi.

Comfrey kwa mbolea (hupata potashi kufunika udongo kwa majani ya Comfrey (Mulching) hasa kwa nyanya na viazi.

Ni vizuri zile sehemu ambazo unastawi wananchi wakachangamkia na kuupanda ili kupata faida zake.

Ukifanya jitihada za kututembelea bustanini kwetu – Posh Garden utaweza kujionea mimea tiba mbalimbali ikiwemo na comfrey.

Bustanini kwetu utajifunza mambo mengi ikiwemo kilimo cha azolla, watercress, na mengine mengi. Tupo jijini Mwanza, Tanzania – Simu / whatsapp +255655533543

comfrey.jpg
 
Hamjambo waungwana, nimeona nianzishe Uzi maalum kwa ajili ya kufundishana aina ya mimea na matumizi yake. Mimea mingi ilishafanyiwa utafiti na kuandikiwa kila kitu, lakini maandishi hayo yameandikwa kwa lugha ya Kiingereza hivyo wasiojua Kiingereza Ni VIGUMU Sana kujua kilichoandikwa.

Nitaanza na mimea michache ambayo ninayo bustanini kwangu - Posh Garden, hivyo kama na wewe unayo mimea unayojua matumizi yake - ungana nami kuelimishwa jamii. Nawasilisha

Kitaalamu, mimea Ina majina yanayotambulika kisayansi - botanic names, hivyo ili kuifuatilia mimea na matumizi yake Jambo la msingi Ni kujua botanic name ya mmea husika ndo uweze kusearch unavyoongelewa.
Nitaanza na mmea unaitwa phyllantus amarus

View attachment 1937069

Unaitwa phyllantus amarus, wenzetu ulaya wanauheshimu Sana huu mmea kwenye tiba, homa ya ini haifui dafu. Hapa bongo wamama wenye matatizo ya kutoshika mimba umewasaidia Sana. Tembelea Posh Garden ujifunze aina mbalimbali za mimea na faida zake. Tupo jijini Mwanza.

Nakuja na mmea mwingine unaitwa comfrey
View attachment 1937091

COMFREY NI NINI?
Huu ni mmea wa ajabu sana ambao matumizi yake ni mengi mno. Mmea huu uko Kama spinach, majani yake yanafanana na majani ya tumbaku. Hata Tanzania wengi wanaijua Kama sidifo, lakini jina lake la kitaalam ambalo linatumika ulimwenguni kote ni comfrey. Baadhi ya matumizi yake ni Kama ifuatavyo-

1. Hutumika Kama mbogamboga za majani na inao uwezo MKUBWA wa kuongeza UBORA wa Kinga za mwili kwa mwanadamu.

2. Paste yake hutumika kutibu vidonda vya aina yoyote.

3 l. Chai yake hutumika Kama mbolea ya maji (organic foliar fertilizer) ambayo mbali na kuwa mbolea pia hutumika Kama booster na husaidia kuua wadudu kwenye mimea MINGINE..

4. NI chakula kizuri Sana kwa mifugo Kama sungura, kuku, mbuzi, Ng'ombe NK.

Kwa mahitaji ya Miche ya comfrey, wasiliana nasi kwa SIMU au WhatsApp NAMBARI +255 655 533 543.

Tupo Posh Garden
Mtaa wa Mbugani,
Kata ya Kishili,
Wilaya ya Nyamagana,
Jijini Mwanza,
Nchini Tanzania.

Kinachofuata ni mmea maji unapitwa Azolla Pinnata.
View attachment 1937159

Azolla INALIPA
KARIBUNI kwa mbegu...
Kilo sh 15,000
Elimu bure.

SWALI: HIYO AZOLLA NDIO NINI?

AZOLLA!!!! AZOLLAA!!!
Azolla ni mkombozi wa mfugaji...

Azolla ni malisho bora, salama, yenye virutubisho vingi na kubwa zaidi yanakupunguzia gharama za malisho wewe mfugaji hadi nusu ya gharama au zaidi.

Kumbuka gharama kubwa ya ufugaji ni malisho...
Azolla inakusaidia katika hilo hivyo utaongeza faida.

Yaani azolla ni kama uchukue mashudu uchanganye na dagaa uweke mifupa uongeze na dcp bila kusahau chokaa na premix.

Azolla ni chakula kamili kwa mifugo aina zote. Yaani kuku, samaki, ng'ombe , bata, mbuzi...Yaani aina zote.

Faida za azolla.
1. Inapunguza gharama za malisho kwa zaidi ya nusu
2. Inaongeza ukuaji kwani ina virutubisho vingi zaidi.
3.Inaongeza uzalishaji mfano Maziwa au mayai yanaongezeka.
4.Mayai yanakuwa njano halafu organic( utauza sanaaa)

Azolla unaweza ukapanda kwenye bwawa la kujenga ama nailoni lakini hata kwenye beseni inafaa.

Uzuri wa azolla mbegu utanunua mara moja tu...

Karibu kwa mbegu...
Kilo moja ni sh 15,000 tu.

Tunapatikana Mwanza jijini ...
Kama uko mkoani unatumiwa kwa uaminifu mkubwa kabisa.

Ukihitaji maelezo zaidi kuhusu azolla nicheki watsup 0655533543 nakutumia audio usikilize.

Azolla kwa ufugaji unaolipa. Tuache kufuga kwa mazoea.
Mt. Baika (0655533543)

Tuendelee ama tusiendelee?
 
Comfrey plant
Mwonekano wa mche, spidi ya ukuaji, uwezo wa kujikinga na magonjwa na namna inavyozaliana ni sifa kuu za kuufanya mmea huu kuwa mkombozi kwa wakulima hasa kwenye suala la mbolea inayopanda Bei kila leo.

Uchaguzi Ni wako, kulima kwa mazoea au kubadili ili upate mazao Bora na mengi kwa gharama nafuu?

Tupigie upate mbolea, Miche na mafunzo. +255 655 533 543.
Tuko jijini Mwanza.


IMG_20210930_092807_HDR.jpg
 
Mmea unafanyaje? Toa maelezo ya kujitosheleza.
1. Ni mboga na inasemekana kuoandisha cd4 kwa haraka
2. Ni dawa ya kuunga mifupa na kuponya maumivu kwa haraka Sana
3. Inatumika kutakatisha ngozi
4. Ni chakula Cha mifugo
5. Inatumika kuandaa mbolea.
Hayo ndo ninayoyajua kuhusu mmea huo.
 
Back
Top Bottom