Mimba kwa wanafunzi zaongezeka Misungwi, kipindi hiki cha COVID 19

Nyanswe Nsame

Senior Member
Jul 9, 2019
158
175
Mimba kwa wanafunzi zaongezeka Misungwi, kipindi hiki cha COVID 19

VITENDO vya ukatili vimetajwa kuongezeka katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza katika kipindi hiki cha maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na kirusi cha Corona (COVID 19).

Imeelezwa kwamba, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu, wilaya ya Misungwi ina kesi mbalimbali za ukatili zipatazo 66 ikiwemo kuwapa mimba wanafunzi na kutorosha wanafunzi.

Kauli hiyo imetolewa mbele ya mkuu wa wilaya ya Misungwi, Juma Sweda na Afisa wa Dawati la Jinsia la Polisi Wilaya ya Misungwi, Anna Sarimo wakati wa kukabidhi vifaa kinga vya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu vilivyotolewa na shirika lisilo la kiserikali la KIVULINI.

Alisema kati ya hizo kesi, kesi tano zilifikishwa Mahakamani na tayari hukumu ilishatolewa na watuhumiwa wamefungwa jela miaka 30.

Sarimo alisema, licha ya kupambana kufikisha kesi hizo mahakamani, bado kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo jamii kushindwa kutoa taarifa kwa wakati.

"Unakuta binti kapata tayari mimba na anatarajia kujifungua, ndipo mzazi analeta taarifa polisi sasa hali hii inasababisha sisi tushindwe kuwapata watuhumiwa kwa haraka kwa sababu unakuta mtuhumiwa kakimbia.

"Pia changamoto nyingine ni jamii yetu kuwa na mfumo dume unawakandamiza sana wanawake na watoto hi inasababisha familia nyingi zinatelekezwa, na ukiangalia muhimili mkubwa kwa familia ni mama na hii inachangia mama ashindwe kutunza watoto wake," alisema Sarimo.

Sarimo alisema ,changamoto nyingine zinazowakabili kitengo cha dawati la jinsia la Polisi ni usafiri, kwani hali hiyo imekuwa ikisababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ya kutoa elimu kwa jamii hususani maeneo ya vijijini jambo ambalo linasababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea Haki za wanawake na watoto la KIVULINI, Yassin Ally alisema katika wilaya ya Misungwi, wametoa vifaa kinga mbalimbali ikiwemo mashine ya kupima kiwango cha joto mwilini nne,vitakasa mikono (sanitizer) na matenki matatu ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 1000 kila moja.

Vifaa vingine ambavyo vimetolewa na kivulini katika kitengo cha dawati la jinsia Polisi Misungwi, mashine ya kudurufu, viti na compyuta mpakato.

Yassin alisema lengo, ni kuhamasisha ya Jami, kupitia kampeni yao ya CORONA IKO MLANGONI KWAKO ili waweze kuchukua jitihada binafsi za kujikinga na COVID 19.

Alisema ugonjwa huo, ni hatari na haibagui mtu, kwani Corona ipo kwenye nyumba za inada na haichagui Daktari ama mwanasiasa, wakati corona haibagui lakini bado kuna watu wanaleta mzaha kwenye mitandao ya kijamii hivyo nashauri watu wachukue tahadhari.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema, Juma Sweda alisema bado wilaya hiyo inaendelea kuchukua hatua za kupambana na COVID 19 kwa kuwaelemisha wananchi.

Alisema bado kuna watu wanaoendelea kufanya mzaha na utani na ugonjwa huo, kufuatia kuwepo kwa watu wanaoendelea kucheza bao na karata muda wa kazi hatua ambayo inachangia kuenea kwa ugonjwa huo.

Sweda alisema watu hao (wacheza bao na karata) wanashindwa kufanya shughuli za uzalishaji ili kusaidia kuliingizia taifa pato na badala yake wanacheza bao kwenye vijiwe vya kahawa.

Kutokana na hali hiyo, Sweda amewaagiza watendaji wa kata na makatibu tarafa, sambamba na kutoa elimu kwa wananchi namna ya kujikinga nanCOVID 19, pia wawahimize wananchi kufanya kazi.

Mwisho
 
Mimba kwa wanafunzi zaongezeka Misungwi, kipindi hiki cha COVID 19

VITENDO vya ukatili vimetajwa kuongezeka katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza katika kipindi hiki cha maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na kirusi cha Corona (COVID 19).

Imeelezwa kwamba, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu, wilaya ya Misungwi ina kesi mbalimbali za ukatili zipatazo 66 ikiwemo kuwapa mimba wanafunzi na kutorosha wanafunzi.

Kauli hiyo imetolewa mbele ya mkuu wa wilaya ya Misungwi, Juma Sweda na Afisa wa Dawati la Jinsia la Polisi Wilaya ya Misungwi, Anna Sarimo wakati wa kukabidhi vifaa kinga vya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu vilivyotolewa na shirika lisilo la kiserikali la KIVULINI.

Alisema kati ya hizo kesi, kesi tano zilifikishwa Mahakamani na tayari hukumu ilishatolewa na watuhumiwa wamefungwa jela miaka 30.

Sarimo alisema, licha ya kupambana kufikisha kesi hizo mahakamani, bado kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo jamii kushindwa kutoa taarifa kwa wakati.

"Unakuta binti kapata tayari mimba na anatarajia kujifungua, ndipo mzazi analeta taarifa polisi sasa hali hii inasababisha sisi tushindwe kuwapata watuhumiwa kwa haraka kwa sababu unakuta mtuhumiwa kakimbia.

"Pia changamoto nyingine ni jamii yetu kuwa na mfumo dume unawakandamiza sana wanawake na watoto hi inasababisha familia nyingi zinatelekezwa, na ukiangalia muhimili mkubwa kwa familia ni mama na hii inachangia mama ashindwe kutunza watoto wake," alisema Sarimo.

Sarimo alisema ,changamoto nyingine zinazowakabili kitengo cha dawati la jinsia la Polisi ni usafiri, kwani hali hiyo imekuwa ikisababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ya kutoa elimu kwa jamii hususani maeneo ya vijijini jambo ambalo linasababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea Haki za wanawake na watoto la KIVULINI, Yassin Ally alisema katika wilaya ya Misungwi, wametoa vifaa kinga mbalimbali ikiwemo mashine ya kupima kiwango cha joto mwilini nne,vitakasa mikono (sanitizer) na matenki matatu ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 1000 kila moja.

Vifaa vingine ambavyo vimetolewa na kivulini katika kitengo cha dawati la jinsia Polisi Misungwi, mashine ya kudurufu, viti na compyuta mpakato.

Yassin alisema lengo, ni kuhamasisha ya Jami, kupitia kampeni yao ya CORONA IKO MLANGONI KWAKO ili waweze kuchukua jitihada binafsi za kujikinga na COVID 19.

Alisema ugonjwa huo, ni hatari na haibagui mtu, kwani Corona ipo kwenye nyumba za inada na haichagui Daktari ama mwanasiasa, wakati corona haibagui lakini bado kuna watu wanaleta mzaha kwenye mitandao ya kijamii hivyo nashauri watu wachukue tahadhari.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema, Juma Sweda alisema bado wilaya hiyo inaendelea kuchukua hatua za kupambana na COVID 19 kwa kuwaelemisha wananchi.

Alisema bado kuna watu wanaoendelea kufanya mzaha na utani na ugonjwa huo, kufuatia kuwepo kwa watu wanaoendelea kucheza bao na karata muda wa kazi hatua ambayo inachangia kuenea kwa ugonjwa huo.

Sweda alisema watu hao (wacheza bao na karata) wanashindwa kufanya shughuli za uzalishaji ili kusaidia kuliingizia taifa pato na badala yake wanacheza bao kwenye vijiwe vya kahawa.

Kutokana na hali hiyo, Sweda amewaagiza watendaji wa kata na makatibu tarafa, sambamba na kutoa elimu kwa wananchi namna ya kujikinga nanCOVID 19, pia wawahimize wananchi kufanya kazi.

Mwisho

Hao mabinti watakuwa WEUPE. Wasukuma bwana!
 
Wazazi wasikwepe majukumu yao ya kuwaelimisha watoto wao wa kike na wa kiume juu ya madhara yatokanayo na vitendo vya ngono katika umri mdogo. Wazazi wengi wa kiafrika mjini na vijijini tunakumbatia sana mila potofu kwa kuona aibu kuwaelimisha watoto wetu wadogo hasa kwenye haya mambo ya ngono zembe. Kutegemea taasisi za serikali (hasa shule na walimu) ndiyo watufundishie na kutulelea watoto wetu wakati sisi tuliowaleta hao watoto hapa duniani tumerelax na hatuchukui hatua zozote za maana za kuwalea na kuwaelimisha/kuwakanya watoto wetu madhara yake ndiyo hayo. Kwa akili za sisi watanzania tutuanza kuilaumu serikali kwa jambo kama hili. HEBU TUBADILIKE JAMANI.
 
Mimba kwa wanafunzi zaongezeka Misungwi, kipindi hiki cha COVID 19

VITENDO vya ukatili vimetajwa kuongezeka katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza katika kipindi hiki cha maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na kirusi cha Corona (COVID 19).

Imeelezwa kwamba, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu, wilaya ya Misungwi ina kesi mbalimbali za ukatili zipatazo 66 ikiwemo kuwapa mimba wanafunzi na kutorosha wanafunzi.

Kauli hiyo imetolewa mbele ya mkuu wa wilaya ya Misungwi, Juma Sweda na Afisa wa Dawati la Jinsia la Polisi Wilaya ya Misungwi, Anna Sarimo wakati wa kukabidhi vifaa kinga vya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu vilivyotolewa na shirika lisilo la kiserikali la KIVULINI.

Alisema kati ya hizo kesi, kesi tano zilifikishwa Mahakamani na tayari hukumu ilishatolewa na watuhumiwa wamefungwa jela miaka 30.

Sarimo alisema, licha ya kupambana kufikisha kesi hizo mahakamani, bado kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo jamii kushindwa kutoa taarifa kwa wakati.

"Unakuta binti kapata tayari mimba na anatarajia kujifungua, ndipo mzazi analeta taarifa polisi sasa hali hii inasababisha sisi tushindwe kuwapata watuhumiwa kwa haraka kwa sababu unakuta mtuhumiwa kakimbia.

"Pia changamoto nyingine ni jamii yetu kuwa na mfumo dume unawakandamiza sana wanawake na watoto hi inasababisha familia nyingi zinatelekezwa, na ukiangalia muhimili mkubwa kwa familia ni mama na hii inachangia mama ashindwe kutunza watoto wake," alisema Sarimo.

Sarimo alisema ,changamoto nyingine zinazowakabili kitengo cha dawati la jinsia la Polisi ni usafiri, kwani hali hiyo imekuwa ikisababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ya kutoa elimu kwa jamii hususani maeneo ya vijijini jambo ambalo linasababisha washindwe kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea Haki za wanawake na watoto la KIVULINI, Yassin Ally alisema katika wilaya ya Misungwi, wametoa vifaa kinga mbalimbali ikiwemo mashine ya kupima kiwango cha joto mwilini nne,vitakasa mikono (sanitizer) na matenki matatu ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 1000 kila moja.

Vifaa vingine ambavyo vimetolewa na kivulini katika kitengo cha dawati la jinsia Polisi Misungwi, mashine ya kudurufu, viti na compyuta mpakato.

Yassin alisema lengo, ni kuhamasisha ya Jami, kupitia kampeni yao ya CORONA IKO MLANGONI KWAKO ili waweze kuchukua jitihada binafsi za kujikinga na COVID 19.

Alisema ugonjwa huo, ni hatari na haibagui mtu, kwani Corona ipo kwenye nyumba za inada na haichagui Daktari ama mwanasiasa, wakati corona haibagui lakini bado kuna watu wanaleta mzaha kwenye mitandao ya kijamii hivyo nashauri watu wachukue tahadhari.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema, Juma Sweda alisema bado wilaya hiyo inaendelea kuchukua hatua za kupambana na COVID 19 kwa kuwaelemisha wananchi.

Alisema bado kuna watu wanaoendelea kufanya mzaha na utani na ugonjwa huo, kufuatia kuwepo kwa watu wanaoendelea kucheza bao na karata muda wa kazi hatua ambayo inachangia kuenea kwa ugonjwa huo.

Sweda alisema watu hao (wacheza bao na karata) wanashindwa kufanya shughuli za uzalishaji ili kusaidia kuliingizia taifa pato na badala yake wanacheza bao kwenye vijiwe vya kahawa.

Kutokana na hali hiyo, Sweda amewaagiza watendaji wa kata na makatibu tarafa, sambamba na kutoa elimu kwa wananchi namna ya kujikinga nanCOVID 19, pia wawahimize wananchi kufanya kazi.

Mwisho
Ili kuwa na uhakika wa hili bandiko nilitarajia kuona hilo ongezeko la mimba miongoni ,wa wanafunzi. Mfano katika kipindi cha January - March idadi ya wanafunzi waliopata ujauzito imepandz kwa aidha asilimia hizi kufikia hizi ukilinganisha labda na kipinda kama hiki mwaka 2019 au mwezi September hadi December mwaka jana. Hapo utakuwa umeonyesha kiasi cha ongezeko.
Pia umetaja idadi ya kesi ila haijafafanua ni kesi za mimba au za unyanyasaji kijinsia. Hebu fafanua zaidi.
 
Back
Top Bottom