Million 142.96 Zatumika kutangaza Budget 2007/8

Bowbow

JF-Expert Member
Oct 20, 2007
541
31
Mil. 142.9/- zatumika kutangaza bajeti
MBUNGE VITI MAALUM



na Irene Mark, Dodoma



SERIKALI ilitumia jumla ya sh milioni 142.96 kugharamia safari za mawaziri na wasaidizi wao mwaka jana, wakati wa ziara za mikoa yote nchini kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutoa ufafanuzi kuhusu bajeti ya serikali ya mwaka 2007/08.
Akijibu swali bungeni jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge) Dk. Batilda Burian, alisema ziara hizo zilikuwa muhimu licha ya wabunge, ambao ni wawakilishi wa wananchi kuweza kuifanya kazi hiyo.

Akitetea uamuzi wa serikali kuwatumia mawaziri kuitekeleza kazi hiyo licha ya kuwepo kwa wabunge, Dk. Buriani alisema wabunge kama wawakilishi wa wananchi wanao wajibu wao na serikali nayo kwa upande wake inayo majukumu yake.

Aliliambia Bunge wakati akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Mhonga Said Ruhwanya (CHADEMA), kuwa fedha zilizotumika zilitokana na fedha zilizotengwa katika bajeti ya serikali chini ya mafungu ya safari za viongozi hao.

Katika swali lake, Ruhwanya alitaka kujua sababu zilizoifanya serikali kulitawanya Baraza la Mawaziri mikoani ili kuelezea utekeleazaji wa bajeti ya mwaka 2007/08 na fedha gani zilitumika katika ziara hiyo kuwalipa mawaziri, wasaidizi wao na watendaji wa serikali waliohusika katika ziara hizo.

Aidha, Ruhwanya alihoji sababu za serikali kutumia gharama nyingi kwa ajili ya kazi hiyo badala ya fedha hizo kuzielekeza kwenye utekelezaji wa ahadi zake ili wananchi waone mafanikio.

Lakini katika jibu lake, Dk. Burian alibainisha kuwa serikali iliamua kuwatuma mawaziri mikoani ili kuhimiza halmashauri na madiwani kuimarisha usimamizi wa fedha za serikali zilizotengwa katika maeneo yao ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

"Serikali imewataka wananchi watambue kuwa fedha za bajeti ni kodi zao, hivyo wasimamie matumizi yake ili zitumike vizuri kwa kazi zilizokusudiwa," alisema Dk. Burian na kuongeza kuwa kazi ya kutoa ufafanuzi huo isingeweza kuachwa kwa wabunge kwa kuzingatia kuwa hawana rasilimali za kutosha kuifanya kazi hiyo ipasavyo.

Jibu hilo lilimwamsha Benson Mpesya (Mbeya Mjini-CCM) aliyehoji iwapo serikali inalitambua hilo, kwa nini isiwaongeze wabunge uwezo ili waisaidie serikali katika kusimamia na kufuatilia matumizi ya fedha za bajeti.

Katika jibu la nyongeza, Dk. Burian alisema serikali itatekeleza hilo na kupitia sheria iliyopendekezwa na kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya jimbo, utakaowaongezea wabunge uwezo kirasilimali.
 
Well wanaweza kuquantify walichokipata/mafanikio baada ya ziara hizo??????????
 
Pia nahisi gharama halisi si hizi, hivi kweli mawaziri 60 + madereva 60 + wapambe (akina Akwilombe 60) kama wanapata average ya laki kwa siku kama posho kwa siku kumi ni Tshs milioni 180. Haya mafuta na gharama za maintenence ya mashangingi - Assume ni laki 5 kwa siku. Mashangingi 60 kwa siku kumi ni milioni 300. Jumla ndogo ni milioni 480. Haiingii vizuri akilini hii habari.

"WABUNGE WAOMBE BREAKDOWN YA HIYO 142.96M BANA"
 
Mawaziri watumia milioni 142.9 `kuuza` bajeti mikoani

2008-01-30 09:57:46
Na Gaudensia Mngumi, Dodoma


Zaidi ya Sh. milioni 142.9 zilitumika kugharimia safari za mawaziri waliotumwa kwenda mikoani kuelezea utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2007/2008.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Dk. Batlida Buraini alisema hayo Bungeni jana wakati akijibu swali la Mbunge wa CHADEMA (Viti Maalum), Bi. Mhonga Ruhwanya aliyetaka kujua kiasi gani cha fedha kilitumiwa na mawaziri hao.

Katika swali lake, Bi. Ruhwanya alitaka kujua gharama zilizotumika kuwalipa mawaziri na maofisa wengine waliokuwa kwenye misafara hiyo.

Alisema kuwa serikali ingewatumia wabunge waliopo mikoani kuzungumzia bajeti hiyo badala ya kuwatuma mawaziri, hali ambayo ingepunguza gharama.

Katika majibu yake, Dk. Buriani alisema kila wizara ilitumia fedha zilizoko katika bajeti ya kawaida na ilijumuishwa katika safari za kawaida za mawaziri na wasaidizi wao ikiwa ni sehemu ya kazi zao za kila siku za majukumu yaliyo chini ya wizara zao.

Alifafanua kuwa serikali iliamua kuwatuma mawaziri mikoani ili kuhimiza halmashauri na madiwani kuimarisha usimamizi wa fedha za umma zilizotengwa katika maeneo yao.

``Lengo lilikuwa ni kuwahimiza wananchi wasaidiane na serikali kusimamia fedha za umma na wakiona usimamizi na utekelezaji wa miradi ni hafifu watoe taarifa za matumizi ya fedha zao,`` alisema Waziri Buriani.

Aliwaambia wabunge kuwa bajeti ya mwaka jana ilikuwa Sh. trilioni 6.05 na katika hizo trilioni 3.14 ambazo ni nusu ya bajeti zililengwa kutumika kwenye maeneo ya kipaumbele ya sekta za afya, elimu, maji, miundombinu na kilimo.

``Kiasi hiki ni kikubwa kupelekwa kwenye halmashauri , kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya nchi yetu,`` alisema.

Akijibu swali la mbunge huyo juu ya kuwatumia wabunge badala ya mawaziri alisema, wabunge wana wajibu wa kuwaelimisha wananchi juu ya majukumu na masuala mbalimbali ya serikali lakini hawana rasilimali za kutosha za kutekeleza wajibu huu.

Lakini pia aliliambia Bunge kuwa mawaziri wana wajibu wa kufuatilia utekelezaji wa kazi na mipango ya serikali ili kuona kuwa mambo yaliyokubalika kitaifa yanatekelezwa.
``Hata siku moja hatutakaa kimya tukasema serikali isifanye kazi zake kwa kuwa kuna wabunge.

Tutawafuata wananchi mikoani na kusikiliza kero na kuwaletea maendeleo kwa kuwa ndiyo waliotupa kura na pia tutaendelea kuona kuwa shughuli za serikali zinatekelezwa,`` alisisitiza.

Alisema shughuli za mawaziri haziingiliani na za wabunge bali majukumu ya viongozi hao yanakwenda sambamba katika kuwahudumia wananchi.

Mbunge wa Mbeya Mjini (CCM), Bw. Benson Mpesya, akiuliza swali la nyongeza alihoji kwa nini serikali isiwapatie nyezo wabunge ili wafanye kazi kikamilifu ikiwemo ya usimamizi wa fedha za umma.

Alisema wabunge wataendelea kuwezeshwa ili wawahudumie wapiga kura na kwamba muswada wa sheria za mfuko wa maendeleo ya majimbo unaoandaliwa utawezesha upatikanaji wa rasilimali na uwezo katika kuhudumia wananchi.

SOURCE: Nipashe
 
Dk. Buriani alisema wabunge kama wawakilishi wa wananchi wanao wajibu wao na serikali nayo kwa upande wake inayo majukumu yake
Alipobanwa zaidi sikiliza hili jibu (in colour) linabadilika


Dk. Burian na kuongeza kuwa kazi ya kutoa ufafanuzi huo isingeweza kuachwa kwa wabunge kwa kuzingatia kuwa hawana rasilimali za kutosha
Hapa jibu sio jukumu la serikali tena bali wawakilishi hawana rasimali za kufanya hivyo.

Drama inaendelea
Dk. Burian alisema serikali itatekeleza hilo na kupitia sheria iliyopendekezwa na kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya jimbo, utakaowaongezea wabunge uwezo kirasilimali
Hii ni njia inayotumika siku zote kusilence mambo, yaani serikali inalishughulikia

Nadhani ni wakati sasa wabunge waombe time frame ya mipango yote inayosemekana ipo kwenye hatua ya kutaka kutekelezwa. Mfano Jana hiyo hiyo Waziri wa Afya alisema upo mpango wa kujenga Kitua Tiba ya Moyo (tofauti na THI)hakuna anaeuliza tena huo mpango uko kwenye hatua gani, utagharimu kiasi gani umepangwa kukamilika lini. Ndio maana Mawaziri wanatumia huu usemi "serikali iko kwenye mpango" kumaliza hoja
 
Well wanaweza kuquantify walichokipata/mafanikio baada ya ziara hizo??????????

Yep! unapoteza ng'ombe wa kulima wa shilingi laki moja, unauza shamba lote [na mimea ndani yake] kumtafuta; sasa ukimpata atalima wapi!

Only In Bongoland!
 
Bajeti ya serikali ya sasa ni ngumu sana, haieleweki hadi watu waelimishwe na mawaziri.

Kwamba "bajeti hii ni nzuri sana, utaondokana na umaskini muda si mrefu... and other blah blah."

Teh teh teh.
 
Kuna hii tahariri ya leo ya Tanzania Daima nimeona tushee namna huyu mama Buriani alivyojikanyanga jana kutetea utumbo wa matumizi mabaya ya walipa kodi walalahoi eti kisa kueleza uzuri wa bageti mbaya.

JANA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Dk. Batilda Burian, alitangaza bungeni kuwa serikali ilitumia sh milioni 142.96 kugharamia safari za mawaziri na wasaidizi wao mwaka jana, wakati wa ziara za mikoani, kwa kile kilichoelezwa kutoa ufafanuzi kuhusu bajeti ya serikali ya mwaka 2007/08.
Dk. Burian alieleza hayo alipokuwa akijibu swali bungeni na kueleza kuwa ziara hizo zilikuwa muhimu licha ya kuwapo wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi kuweza kuifanya kazi hiyo.

Alieleza kuwa wabunge kama wawakilishi wa wananchi wana wajibu wao na serikali nayo kwa upande wake inayo majukumu yake. Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhonga Said Ruhwanya (CHADEMA).

Kiasi hiki cha fedha kilichotumika kwa ziara hizi ni matumizi mabaya ya fedha kwa sababu fedha zilizotumika ni za walipa kodi wengi wao wakiwa walalahoi.

Pamoja na serikali kutumia kiasi hicho kikubwa cha fedha, hakuna mafanikio ya moja kwa moja yaliyoonekana kutokana na ziara hizo zilizowagharimu wananchi.

Fedha hizi zilizokwenda kuteketezwa katika ziara ambazo hazikuwa na manufaa yoyote kwa umma zingeweza kutumika kufanyiwa shughuli mbalimbali za maendeleo kama kuboresha sekta ya elimu na nyinginezo muhimu au kushughulikia kero mbalimbali za wananchi.

Hakika jambo hilo na mengineyo ambayo yamekuwa kero kwa wanannchi kwa kiasi kikubwa, yameshusha umaarufu wa serikali hiyo iliyokuja na falsafa ya Ari mpya, Nguvu mpya na Kasi mpya.

Kushuka kwa umaarufu wa serikali kulidhihirishwa na utafiti wa REDET uliofanywa mwisoni mwa mwaka jana.

Tangu awali wananchi walionekana kuzipinga ziara hizo za mawaziri, lakini kama kawaida yake serikali ililazimisha na kupuuza mawazo ya wananchi walio wengi.

Matokeo yake katika ziara hizo, baadhi ya mawaziri walizomewa na wananchi. Kuna ushahidi wa wazi kabisa, ingawa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikipinga kuwapo kwa vitendo hivyo.

Kama kweli ziara hizo zilikuwa na lengo la kueleza uzuri na ubaya wa bajeti, wananchi walikwishafahamu tangu ilipopitishwa bungeni Julai, mwaka jana, kwani baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo gharama za maisha zilipanda na hali ya maisha kuwa ya juu.

Hata kama kulikuwapo na ulazima wa kufanya ziara hizo, jukumu hilo wangeachiwa wabunge ambao wana nafasi nzuri ya kuwafikia wananchi na hapo ndipo unapoonekana umuhimu wa mgawanyiko wa madaraka.

Ufujaji wa aina hiyo wa fedha za walipa kodi kwa kiasi kikubwa unawaumiza wananchi na kuwafanya wasiwe na imani na serikali yao.

Haijawahi kutokea katika historia ya Tanzania serikali ikatuma mawaziri na manaibu wake kwenda mikoani kwa wananchi kuelezea uzuri wa bajeti. Kibaya zaidi, hakuna mafanikio yaliyoonekana kutokana na ziara hizo. Hili ni funzo kubwa kwa Serikali ya Awamu ya Nne.

Serikali ikitaka iendelee kuaminiwa na kuheshimiwa na wananchi, ni lazima itimize ahadi zake kwa vitendo na si maneno, kwani hayawasaidii kuleta maendeleo kwa wananchi waliokwishaanza kuonyesha kukata tamaa na serikali yao.
 
Hapa pia nafikiri inabidi tujue je hiyo hela iliyotumika kuinadi bajeti mbovu ilikuwa kwenye bajet au waliitumia tu kutokana na maamuzi yao tu kama viongozi?

Serikali ya Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya nafikiri inatumia hizi slogans kuupinga ukweli mpaka pale huo ukweli utakapowekwa hadharani ukiwa na vidhibiti ndo watakubali. They argue and talk alot....hii inasikitisha na hao hao wananchi wanaonadiwa bajet ndo kila siku wanaathirika na gharama za maisha kupanda ihali chanzo ni ufujaji wa hela za wananchi....
Does'nt make sense to me na nafikiri this time these guys will have to do alot kuirudisha hii serikali yao ya Upyamadarakani unless waende kumuomba Kibaki Techniques!
 
Milioni 142 kwa safari za mikoani kwa mwaka siyo nyingi hivyo na kama zinatumika vizuri sioni tatizo.Serikali lazima iwe na matumizi.Kama kuna ubaya hapo ni kwamba baraza letu la mawaziri ni kubwa sana.Mtatizo ni mawili.

1.Zinatumikaje kuleta maendeleo? Tunawezaje kupima "return on investment"?

2.Jamani huu ulimbwende wote za mawaziri wetu ni Tsh 142 tu kwa mwaka? Hiyo figure iko accurate kweli? Kama tunachukua 142.96 kwa mawaziri 60 (inategemea kama hizi namba ni kwa mawaziri kamili tu au manaibu pia) wastani ni kadiri Tsh 2.38 milion kwa mwaka, wanataka kutudanganya ukichanganya mafuta, marupurupu ya safari na gharama zooote za serikali (achilia mbali gharama za kweli ambazo zinajumuisha kirima kutoka kwa wananchi masikini) ni wastani wa Tsh 2.38 kwa mwaka kwa waziri?

Mimi siamini hizi tarakimu.
 
Milioni 142 kwa safari za mikoani kwa mwaka siyo nyingi hivyo na kama zinatumika vizuri sioni tatizo.Serikali lazima iwe na matumizi.Kama kuna ubaya hapo ni kwamba baraza letu la mawaziri ni kubwa sana.Mtatizo ni mawili
.

Suala kubwa mimi kwangu ni:-
1. Ina maana hii bajeti ilikuwa na kasoro kubwa kiasi cha kuweka mpango wa kuinadi au ni uelewa/upeo wa wananchi ndo ulionekana mdogo katika kuichambua bajeti?
2. Kweli 142m siyo nyingi kwa ziara za mawaziri kwa mwaka lakini je was the purpose met au na bajeti ya 2008/2009 pia tutahitaji kueleweshwa kama wanachi? (REWORK)
 
Pundit,
Ni single trip za kutetea budget na sii za mwaka mzima! Na mwaka mzima ni kubwa mara nyinyi!

Daaaaaayummmmmm!

No wonder nilikuwa naona figures hazi make sense!

In that case hayo ni matumizi mabaya ya fedha za umma.
 
Kama alivyosema Mwanahalisi hizi si pesa za mwaka mzima ni zile zilizotumika kwenye safari za mawaziri kwenye kilichoitwa kuelezea bageti. Waliita hivyo kuficha ukweli lakini nia hasa ilikuwa kurudisha imani ya wananchi baada ya wapinzani kumwaga radhi pale Mwembeyanga kwa kutoa list of shame.

Na hilo halikuwa kweli kwani walifanya hivyo mara tu baada kuhisi kwamba mambo si mambo kwao. Na waliohudhuria mikutano wanasema bageti haikuwa agenda kama wanavyodai ilikuwa in porojo tu ndio maana waliishia kuzomewa baadhi yao. Its fun hata hiyo approach waliyotumia kwani walikwenda kama kundi wakiwemo kina John Komba na TOT na Dito. Wangeweza kugawana ingepunguza idadi ya siku na gharama pia. Kingine ni kwamba waliishia mijini ambako vyombo vya habari,tv,magazeti n.k ni vingi so walikuwa wanaijuwa hiyo bageti, walipaswa kwenda vijijini ambako hawapati taarifa nyingi. In my opinion Wabunge kama ingekuwa ni budget wangeweza kulifanya hili vizuri zaidi kuliko hao mawaziri.
 
Hivi wabunge wetu wataendelea kukubali majibu ya kipuuzi kama haya mpaka lini? Hivi akina Akwilombe,Tambwe Hiza, Ditto na wengineo ndio wataalamu wa hiyo bageti yao fake? Si afadhali hizo milioni zingekutumika kusimamishia hizo kuta wanazoziita shule na kuwapunguzia walalahoi mzigo wa kuchangia ujenzi wa hizo kuta?
 
Kuna hii habari kuwa serikali ilitumia zaidi ya milioni mia moja kwa kuwatuma mawaziri mikoani kuelezea bajeti!

Give me a ........
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom