Milion 50 za Paul Makonda kushindaniwa na wasanii wawili, Banana Zoro vs Christian Bella

Mkuu wa mko wa Dar es salaam mh Paul Makonda amejitolea kuandaa mpambano mkali sana wa kugombea Tsh 50 millions baina ya wasanii wawili waotumbuiza muziki kupitia live band kati ya king of the best melody Christian bella dhidi ya mkongwe Banana Zoro!

Mkuu huyo wa mkoa ameyasema hayo katika hafla yake fupi ya kujipongeza baada ya ziara ya siku 10 ya kutatua kero za wana Dar es salaam, pia amesema yeye binafsi ni mpenzi wa muziki unaopigwa live.

My take: Wakazi wa Dar es salaam kero zao zimekwisha tatuliwa na mheshimiwa, ndio maana kaamua kuanzisha tamasha hili la watu wawili tu likimtaka mshindi mmoja (winner take all).
647f0046580df2f292d5846298afc18c.jpg
 
Mkuu wa mko wa Dar es salaam mh Paul Makonda amejitolea kuandaa mpambano mkali sana wa kugombea Tsh 50 millions baina ya wasanii wawili waotumbuiza muziki kupitia live band kati ya king of the best melody Christian bella dhidi ya mkongwe Banana Zoro!

Mkuu huyo wa mkoa ameyasema hayo katika hafla yake fupi ya kujipongeza baada ya ziara ya siku 10 ya kutatua kero za wana Dar es salaam, pia amesema yeye binafsi ni mpenzi wa muziki unaopigwa live.

My take: Wakazi wa Dar es salaam kero zao zimekwisha tatuliwa na mheshimiwa, ndio maana kaamua kuanzisha tamasha hili la watu wawili tu likimtaka mshindi mmoja (winner take all).
Hizo hela za mshindi atakaezitoa ni nani??
 
Bella anapendwa sana na mkulu bilanga...so msishangae mkulu akiwa mgen rasmi...coz alimiss fiesta nafikir hii amealikwa
 
Angeonyesha uzalendo kwa kum shindanisha banana na mzawa mwingine ili pesa izunguke humuhumu nchini
 
Hivi TAKUKURU hawana meno ya kumchunguza Mkuu wa Mkoa?

Ukimfatilia kwa mwezi mzima matumizi yake ni zaidi mara 100 ya mshahara wake kama mtumishi umma.

Hakuna utakatishaji unaendelea hapa?
 
Hadithi ya Mwendapole na Madereva

Hawa ni vijana waliojipatia umaarufu mkubwa katika nchi ya Kusadikika kila mmoja kwa sababu zake tofauti.

Madereva alianza kupanda chati baada ya kusikika hadharani akiwatukana viongozi (hata wa chama chake) na akafika kilele pale alipoonekana wazi akitaka kuvuruga mchakato wa KATI BAR mpya ili juwafurahisha wakuu wake. Anakumbukwa kwa vurugu za pale kwenye LULU ya BULUU aliposemekana alimpiga Mzee War Iobber kwa chupa ya maji na mdahalo kuvurugika.

Kwa upande wa MwendaPole yeye alijipatia umaarufu kwa sababu zote chanya, kwanza alisimamia kile alichoamini kuhusu mchakato wa KATI BAR kuwa KATI BAR ya wananchi ndiyo mwarobaini wa kudumu kwa taifa la Kusadika.

Kwa vyovyote vile...vijana hawa kwa wakati ule hawakuwa marafiki wala kuwa na fikra sawa, mmoja akitetea genge lililomtuma akawa mpiga zumari wa mfalme na mwingine akitaka KATI BAR inayowapa wananchi nguvu zaidi na kumbana mfalme.

Zoezi la Kati Bar likafa kifo cha kimya kimya, likafuatiwa na uchaguzi wa kumpata mfalme mpya lakini kabla yule wa zamani hajaondoka akamteuwa Madereva kuwa mkuu wa WE-LIAR, wengi wakasema ni fadhila kwa kazi nzuri ya upigaji wa zumari. Kuelekea uchaguzi wa mfalme mpya, Mwendapole akaamua kumpigania mfalme mpya kutoka msitu wa kijani, akidhani huyu mpya atakuwa na tofauti na aliyemtangulia. Watu wakasema sana kuwa Mwendapole anataka kupewa mfupa...akakanusha na kujiapia kuwa hataki na anamwomba Mungu amwepushe.

Ukafika wakati mfalme mpya anatoa fadhila kwa wapiganaji wake....Mwendapole akapewa mfupa...watu wakamkumbusha viapo vyake, jamaa akala ngumu. Madereva naye akabadili gia angania akawa dam dam na mfalme mpya akabaki mjini. Yakatokea mabadiliko, Madereva akapandishwa cheo akawa mkubwa wa Mjini na Mwendapole akatolewa kijijini akaletwa mjini sasa yupo chini ya Madereva.

Mambo yamebadilika sana, Mwendapole aliamini na anajua kuwa anauwezo mkubwa kuliko Madereva, na anajua kuwa mfalme mpya hasimamii kabisa misingi ya ile KATI BAR aliyokuwa anaipigania, amejikuta katika wakati mgumu....si wa kumeza wala kutema, amebaki kuwa MWANAFALSAFA akiandika maneno magumu ambayo wadadisi na wachunguzi wa kusadikika wanadai kuwa hali sasa si nzuri kwa Mwendapole.

Wananchi wanamtaka Mwendapole afanye maamuzi na siyo kulalamika kwa mafumbo, achague mmoja awe mpiga zumari wa mfalme au aendelee kutetea KATI BAR ya wananchi iliyomjengea heshima kubwa lakini ajue kuwa, akichagua uamuzi wa pili akubali kujitoa, kujikana na katu hatafanikiwa asipohama katika msitu wa Kijani.
Hiii stori ichapishwe isomwe na wanafunzi wa o-lever ni fasihi tosha
 
Nawasoma tuu, ila watumishi wa umma wakipewa pesa ama zawadi yoyote wanatakiwa kuikabidha kwa uongozi wa juu
 
Hivi TAKUKURU hawana meno ya kumchunguza Mkuu wa Mkoa?

Ukimfatilia kwa mwezi mzima matumizi yake ni zaidi mara 100 ya mshahara wake kama mtumishi umma.

Hakuna utakatishaji unaendelea hapa?
The best way to do a crime,,,is to do it in public...

nadhani anatumia hii theory.,,. izo amout anazotoa ni ambigous considering nchi nzma inalalmika ukata
 
Mwacheni ajipongeze kwa kazi ngumu ya kuijenga Dar es salaam mpya, kazi ameifanya kwa siku 10 tu. Na Dar mpya imepatikana, shida zimeisha,
 
Akimaliza kuwapambanisha hao , tunasubiri awapambanishe Diamond vs Alikiba , akimaliza hapo Clouds fm vs Efm then Mange kimambi vs Le mutuz maana ndo kazi anazoziweza
 
mkuu lugha ya wapi hii!?
andika ueleweke, nafikiri kiswahili au kingereza utaeleweka zaidi
23. Bali umejiinua juu ya Bwana wa mbingu; nao wamevileta vyombo vya nyumba yake mbele yako; na wewe, na wakuu wako, na wake zako, na masuria wako, mmevinywea; nawe umeisifu miungu ya fedha na ya dhahabu, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe; wasioona, wala kusikia, wala kujua neno lo lote; na Mungu yule, ambaye pumzi yako i mkononi mwake, na njia zako zote ni zake, hukumtukuza. 24. Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa. 25. Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI. 26. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. 27. TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. 28. PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi. 29. Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danieli mavazi ya rangi ya zambarau wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake, wakapiga mbiu kutangaza habari zake, ya kwamba yeye ni mtu wa tatu katika ufalme. 30. Usiku uo huo Belshaza, mfalme wa Wakaldayo akauawa. 31. Na Dario, Mmedi, akaupokea ufalme, naye umri wake alikuwa na miaka sitini na miwili

Daniel 5:23 - 31
 
Back
Top Bottom