Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,273
- 17,096
Binamu yangu kaowa majuzi tu...shida ni kuwa baba mkwe kutwa simu haziishi kwa mwananwe kujuwa nini kinaendelea...binamu alipofuatilia kulikoni mkewe kamwambia Baba yake anamhimiza asirukwe ukuta na mumewe...sasa jamaa kachanganyikiwa na mikwara ya mkwewe kwa kuwa alimfuta kumuuliza naye akamjibu ni kweli na kidhubutu kufanyia hivyo huyo mwanawe basi atamnyoosha kimjini..ndoa iko kapuni kwa muda...naomba tuungane kujadili hili :angry: