Mikutano ya Siasa Ingekuwa Huru, Rais Magufuli Angekuwa Hoi Kisiasa

Tuwe wakweli Mungu anatuona.Mikutano imeruhusiwa lakini Mbunge afanye mkutano jimboni kwake.Wabunge wa upinzani wangapi wametumia fursa hii?Tuache kuongea uongo

Mm nilidhani na naamini Kukishinda chama tawala ni lazima watatue kero za wananchi na kuisimamia serikali ipasavyo ktk majimbo yao
Mkuu siasa ni kama club za mpira zinavojiendesha kwa kusajili wachezaji wapya na wazuri sasa ukisema mtu afanye kwenye jimbo lake watapaje member wapya manake jimbo lake wamemwelewa ndo maana wakampa kura jimbo LA upinzani watalichukuaje kama siyo kwenda kupiga siasa kwenye jimbo husika think twice
 
Kila alifanyalo au kusema lingekuwa na majibu kisiasa na ni majukwaani kila mtu anasikia.

Hivi sasa wanasiasa wa upinzani hawana pa kuzungumzia lakini ni kama vile kauli za Mhe Rais, matendo yake na hali halisi ya maisha na kiuchumi yanajichanganya na kujijibu na nyota yake kufanya ififie.

Jee wanasiasa hao nayo wangekuwa huru kujibu kama katiba inavyo waruhusu hali ya bwana mkubwa kisiasa ingekuwaje?

Au alilijua hilo ndio maana kaamua kuweka zuio?
'Ingekuwa' , 'Angekuwa'. maana TOO LATE . Fikiria jambo lenye tija sasa Na baadae. Sio ndoto zilizopita.
 
sidhani kama hii ni excuse bana. there're several ways of skinning a cat.....

kitu gani kinawafanya washindwe kutumia social media (youtube, facebook, whatsapp, instagram, twitter, etc)? wakitoa nondo zao kupitia means hizo magazeti yata-pick na wananchi watakutana nazo kwenye magazeti.

au, wameshindwa hata kuitisha fortnightly media conferences?

au, wameshindwa hata ku-capitalize on ruksa waliyopewa wabunge wao ya mikutano majimboni?

ama, hata kutoa matamko ya uamsho kupitia vikao vya ndani ambavyo tunajua vimeruhusiwa?

last but not least...kwa nini wasianzishe propaganda machinery kama radio au tv? why not???

disgusted!
Mkuu nia ovu ni nia ovu tu wao shida sio mikutano wao wanataka kuuzima upinzani tanzania so hta kma wataanzisha tv sijui redio watafanyiwa zengwe maana nia yao ni kuua upinzania sio mikutano tu mfano gazeti la mawio huwa linaweka zidi ya watawala leo hii likwapi?? Mwanahalisi nalo limepewa onyo..... kwa mazingira haya kweli wapinzani wanawwza simamisha media house bila kusuguana na watawala??
We huoni jf ikikosoa serikali kwenye baadhi ya mada wameanza kuifanyia visa ulitegemea ndo redio au tv itasaidia??? Pia sijui youtube hizo sio watanzania wote wana access na internet hasa vijijini watapataje hizo taarifa za upinzani wakati hta wengine simu hawana kabisa?? Coz research ya zantel mara ya mwisho mwaka juzi ilisena zaidi ya watanzania 40% hawatumii simu so hyo bado challenge kubwa.
Pia mikutano ya wabunge haitosaidia kwasababu ya majimbo ambayo ccm inayo ni mengi kuliko upinzani sasa mkoa kama rukwa ambapo hatuna jikbo hta moja je upunzani utajisimamisha vipi??? Ina maana hayo majimbo tulionayo ndo hayo hayo mpala mwisho?? Hayatoongezeka??
Mkuu muhim hapa ni kupiga kelele aruhusu mikutano na aheshimu katiba maana inataka ivo hizi nyingine kwa sasa hazitekelezeki chini ya utawala huu
 
Hivi kwanini hamkushinda uchaguzi?
Mfumo mbovu wa uchaguzi yaani so huru na haki
vyombo vya dola kutumika na chama kimoja muda wote wa uchaguzi
Tume kutumika na chama kimoja na hata watawala waliposhindwa bado wakafuta uchaguzi bila aibu
Diplomasia kupita kiasi ya upinzani yaani kuogopa kuingia barabarani na kudai haki zao kma alivyofanya odinga 2007
Pia katiba mbovu isoruhusu kupinga matokeo ya urais mahakamani
 
Mkuu ukweli ni kuwa Lowassa tulimpigania kwenye kampeni kwa sababu ya chama ila kwa 2020 ni lazima Chadema iandae mtu anayeonekana kweli anaweza siasa na siyo kurudia ya 2015.. Nashangaa kuona eti mwezi mzima, miezi inaisha katibu mkuu wa chama kama Chadema hasikiki kwenye media! Hiyo ni aibu kubwa na hasa ukiona mambo yanayoendelea nchini!
Mkuu kwa mfumo huu wamagufuli na ubabae wake seriously tunahitaji kiongozi radical sana awe pale juu type ya besigye au odinga ila tukiweka mwanadiplomasia tena be it mbowe lowassa mashinji au safari sijui baregu chadema itapoa sana na hta uchaguzi wa 2020 mavuno yatakuwa machache. Muhim tusifanye makosa kwrnye uchaguzi wa ndani tuoate viongozi radical wanaoweza kupambana na udikteta yaani jino owa jino sio wanadiplomasia tena
 
Lakini hii haiwezi kuwazuia wana siasa kumjibu bali pia kina watu kama Mashinji sijui ni uvivu? Angeenda hata kwenye media kama alivyokuwa anafanya Slaa ingetosha.

Ukweli utuweke huru kuwa kina Mashinji wameshindwa kutumia mwanya huo kuitangaza Chadema.

Siasa za CCM na Magufuli kwa sasa ni nyepesi mno na kina Mashinji wangeweza kiubuka kama wangetumia nafasi vizuri.

Kumbuka kuwa alivyokuwa anafanya Slaa iliwafanya hadi wanasiasa wengine kuingia majukwaani kwa lazima na hilo ndilo linalonifanya nimkubali Slaa hata akiamua kurudi Chadema nimpiganie!!

Chadema ya sasa ambayo kimsingi inatakiwa kuwa chini ya Mashinji imepwaya na imewafanya wengine kuweka majeshi kambini. Natamani kila mwana Chadema aelewe hilo na siyo kutoa kisingizio cha tumezuiwa!

Haiwezekani leo eti kwenye mikutano mzungumzaji mkuu awe Lowassa huku kina Mashinji wakimzindikiza! Hiyo ni aibu kubwa kwa Chadema!!
Mie naona ukatibu mkuu angepewaga at least dk marcua albanie... au maybe mashinji angekuwepo bado ila mambo ya kutolea ufafanuzi wa kisiasa angedelegate kwa mnyika naona hii kazi angeiweza yeye mashinji abakie kwenye paper work tu. Ila kwa chama kilipofikia tunahitaji jitu kma the late mawazo msigwa au lissu watu wa ''TIMBWILI TIMBWILI'' i hope chama kingesimama hta kma wametubana hawa watawala
 
Hata mie kwa sasa naona Tundu Lissu ndio mwiba mbaya sana kwa Ccm na Magu. Kwanza ni mtu mwenye broad knowledge ya mambo mengi ikiwapo historia ya nchi hii na kumuacha mbali Magu.
Ana uelewa wa mambo ya kinataifa mbali sana kwa Magu na wenzake ndani ya Ccm jambo ambalo ni muhimu sana.
La msingi sasa ni kumuandaa kwa muda uliobaki ajijue kuwa sasa ni presidential material na kumpunguza kidogo yale makali ya kisheria. Hakika Lissu anaweza kujisimamia kampeni kama bondia aingiapo ulingoni ha hapo hamtegemei Kocha tena Bali kusukuma masumbwi tuu.
Tuanze sasa kampeni hii [HASHTAG]#LISSU4PRESIDENCY[/HASHTAG]
Mkuu kweli umeona mbali we need a radical leader ikiwezekana wampe uenyekiti mwakani mbowe apumzike sasa naona kama ccm watapelekwa mpela mpela sana na wataonja upinzani halisi ambao kwa sasa wamefanikiwa kuuzima kwa kiasi kikubwa maana umejaa wanadiplomasia....
 
Kila alifanyalo au kusema lingekuwa na majibu kisiasa na ni majukwaani kila mtu anasikia.

Hivi sasa wanasiasa wa upinzani hawana pa kuzungumzia lakini ni kama vile kauli za Mhe Rais, matendo yake na hali halisi ya maisha na kiuchumi yanajichanganya na kujijibu na nyota yake kufanya ififie.

Jee wanasiasa hao nayo wangekuwa huru kujibu kama katiba inavyo waruhusu hali ya bwana mkubwa kisiasa ingekuwaje?

Au alilijua hilo ndio maana kaamua kuweka zuio?
Jamaa anawarahisishia kazi sana wapinzani. Anajimaliza mwenyewe....wapinzani wangekuwa wanamsaidia kujimaliza sijui kama angefika 2020 hajautema mzigo.
 
Ujinga wa Kiafrika tu watu wanataka bla bla kila siku. Mbona hatusikii Hilary Clinton saa hizi anafanya mikutano ya hadhara kujenga Democratic Party?? Kanyagia tu tutazoea.
Mkuu usilinganishe tz na USA clinton kwa wazungu mambo ya ONLINE yametapaka nchi nzima so wanatumia blogs,websites,videoo feeds,youtube channels,social networks na vitu kama hivyo kwa hyo unakuta wananchi wako chumbani tu ila wanapokea nondo zote sasa huku tanzania mikutano imewekwa ili kuwafikia wanamchi ambao hawawezi kumufu hta kununua gazeti so usilinganishe tz na us.
Vile vile sheria yao ya vyama umeisoma?? Mfumo wao wa utawala unaujua?? Hvi unafkiri ni bei rahisi kufanya mikutano majimbo 50 yanye watu si chini ya milion 300 ?? Utalinganisha na tanzania ambapo watu milion 50 pekeee??
Sheria ya vyama vya siasa inakubali maandamano na mikutano ya kisiasa sasa kma aliyajua hya si angeifuta hyo sheria bungeni kuliko kujiamulia mwenyewe tu utafkiri nchi inaendeshwa na mawazo ya mtu mmoja....its not fair at all
 
Mie naona ukatibu mkuu angepewaga at least dk marcua albanie... au maybe mashinji angekuwepo bado ila mambo ya kutolea ufafanuzi wa kisiasa angedelegate kwa mnyika naona hii kazi angeiweza yeye mashinji abakie kwenye paper work tu. Ila kwa chama kilipofikia tunahitaji jitu kma the late mawazo msigwa au lissu watu wa ''TIMBWILI TIMBWILI'' i hope chama kingesimama hta kma wametubana hawa watawala
Mkuu mbona unachanganya mada?
 
..kama ukawa wana nia ya dhati ya kubadili katiba basi hawana budi kuwa na wabunge wengi zaidi ktk bunge letu.

..actually katiba yetu inaelekeza kwamba Waziri Mkuu atateuliwa kutoka ktk chama chenye wabunge wengi zaidi bungeni. Now, i dont think that is a bad position to be.

..vilevile katiba yetu inaelekeza kwamba ili mswada upite bungeni ni lazima ukubalike na 2/3 ya wabunge. Kwa hiyo ukawa wanaweza kuwa more effective kama wakiwa na wabunge zaidi ya asilimia kuanzia 35.

..kwa hiyo ukawa wawekeze pia kwenye kupata wabunge na madiwani wengi zaidi.
Well said mkuu umefkiria vizuri sana na hili wazo liwafikie viongozi wa upinzani wanaopita humu. Hongera sana mkuu kwa kuliona hii
 
..ikiwa ata deliver on his campaign promises atakuwa salama.

..lakini asipo deliver hizi kauli zake zenye ukakasi zitamletea matatizo makubwa kwenye campaign za 2020.

..ila ukawa wasifanye makosa waliyofanya 2015. Lowassa was not inspiring at all. Yaani ilikuwa inatia huruma.

Cc MTAZAMO
What do you mean Lowasa was not inspiring? Are you joking?
 
kiukweli tunalo jukumu la kuandaa mgombea atakayekubalika zaidi na anayeendana na mazingira ya sasa.mgombea mwenye nguvu ya kupambana
 
..100% correct.

..alitakiwa mtu anayeweza kumshambulia Magufuli na ccm.

..Magufuli ana mapungufu mengi ambayo ukiyapeleka kwa wapiga kura uwezekano wa kumshinda upo.

..pia Magufuli amewaahidi waTz maajabu. Sasa asipotimiza, na hizo kauli zake zenye ukakasi ,pamoja na ufisadi aliowahi kuufanya, ukichanganya na tabia yake ya ubaguzi, vyote hivyo vinatoa nafasi kwa mgombea wa upinzani

..sasa ni juu ya upinzani kutafuta mgombea mzuri. Mimi kwa mtizamo wangu nadhani Tundu Lissu anafaa.
Kua kiongoz nchi hii hakutokan na sera au unajua kuongea kias gan bali ni jins gan umejipanga nje ya uwanja na unapata sapoti toka mamlak gani.Mambo yakujua kuongea au sera bado sana kwa akili hiz zamtz.Ndo mana wako waliofanya mazoez tu uwanjan na walishinda.Had siku tutakayoamka ndo kutakua na uwanja sawa wakufanya ayo uliyosema.
 
Asichokijua ni kuwa kuwazuia kusema sasa ni kulikuza jipu alilo nalo. Siku wakipata muda wa kumtumbua hilo donda litakalo jitokeza hapo hataweza hata kusimama. Na litakuwa lineoza hakuna atakaye himili harufu yake
bahati mbaya ccm wanataka yote.Wanataka pora ubunge,udiwani etc.Wakishapora hata mmoja wa chadema .Kipenda kikilia watakimbia jukwaa, watapanda wote na yatasemwa yote.
 
Kila alifanyalo au kusema lingekuwa na majibu kisiasa na ni majukwaani kila mtu anasikia.

Hivi sasa wanasiasa wa upinzani hawana pa kuzungumzia lakini ni kama vile kauli za Mhe Rais, matendo yake na hali halisi ya maisha na kiuchumi yanajichanganya na kujijibu na nyota yake kufanya ififie.

Jee wanasiasa hao nayo wangekuwa huru kujibu kama katiba inavyo waruhusu hali ya bwana mkubwa kisiasa ingekuwaje?

Au alilijua hilo ndio maana kaamua kuweka zuio?
Waseme chochote tokea majimboni kwao, media zipo tutasikia walichokizungumza.
 
Back
Top Bottom