Tankthinker
Member
- May 1, 2011
- 58
- 9
Ushauri wangu kwa CCM ni kwamba waache kujidanganya, bali washughulikie kero za wananchi. Kama wanadhani ujanja ujanja utamaliza tatizo la CCM kwa wananchi hii itakuwa ni ndoto kabisa. CCM wanatakiwa wajue kuwa matatizo ya wananchi ni halisi na yanahitaji ufumbuzi halisi, na si kuzunguka zunguuka kupiga siasa kama Mr. Nape anavyo fanya sasa. Ni kweli kuzunguka atazunguka hata kama ataimaliza Tanzania nzima. Ukweli utabaki kuwa wananchi wanahitaji mabadiliko na si masimulizi ya kisiasa. Faida pekee ya uzungukaji wa Mh. Nape ni wingi wa posho atakazo jipatia, na si kuondoa tatizo la CCM machoni pa Watanzania. Kama kweli ninyi viongozi wa CCM mnamasikio basi sikeni, na kama kweli mna macho basi tazameni, nakama kweli mna akili basi eleweni. Vinginevyo 2015 itawahukumuni tena kwa aibu kubwa sana kuliko hii mlio nayo, maana ninyi mkidhani ni ujuzi wa kusimama majukwaani na kupiga kelele kana kwamba CHADEMA ndio tatizo. Watanzania wanataka maisha bora kwa kila Mtanzania, hicho ndicho kilio chao na si vinginevyo. Mkiendelea kupuuza ukweli huu, huku mkitegemea uchakachuaji utawalinda daima, tambueni kuwa mnajindanganya kwa mbali sana. Get ready CCM you are about to be replaced.