Mikopo ya wanafunzi haipaswi kutoka kwa serikali (HESLB)

Kessy Wa Kilimanjaro

JF-Expert Member
Jan 23, 2016
327
208
Tuiangalie elimu kama bidhaa na huduma zingine kwenye soko la biashara. Bidhaa yeyote ile kukiwa na demand ikipanda basi na bei itapanda. Lakini bei inashuka kukiwa na mashindano. Sasa kukiwa na watu walio na hela nyingi za kutumia na kununua hiyo bidhaa basi watoa bidhaa wanapandisha bei wakijua watu wataweza kulipa.

Elimu ya juu ya University ndivyo hivyo hivyo. Kuna demand ya elimu ya juu sasahivi kwahiyo bei inapanda.

Kinachozidi kuipandisha bei ni mikopo kutoka kwa serikali kwenda kwa wanafunzi. Haijalishi hao wanafunzi wanasoma nini lakini as long as kuna hela ambayo hao wanafunzi wakiidai kutoka kwa serikali wataipata basi watoa huduma au wauza elimu ambao ni university wataongeza bei kwasababu bidhaa yao iko in demand.

Serikali haielewi matatizo inayoyasababisha kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi. Cha kwanza ni kwamba inaongeza bei ya elimu kukua kwasababu inaongeza demand.
Cha pili ni kwamba kila mtu atataka mkopo akati wengine hawana akili za kwenda elimu ya juu na wanaenda kusomea mambo ambayo hayahitaji university.
Hao wataishia kumaliza kusoma na kukosa kazi na kukosa uwezo wa kulipa mikopo.

Mikopo ingekuwa inatolewa na benki binafsi, benki zenyewe zingekuwa zinafanya jitihada kubwa zaidi ya kuchagua nani mwenye akili anayeweza kutumia mkopo huo kusoma kwa bidii na anafaa kupata mkopo. Hii ni kwasababu ingekua ni hela ya hizo benki ambazo zingepotea kama wangechagua kuwapa wanafunzi wajinga mikopo. Kwahiyo wangekua makini kuto toa mikopo ovyo ovyo na hii hatua ingepunguza idadi ya demand ambayo ingepunguza bei ya elimu ya juu.
 
wewe ni mchumi kutoka chuo gani hapa Tanzania? Tehe tehe tehe!
 
Tuiangalie elimu kama bidhaa na huduma zingine kwenye soko la biashara. Bidhaa yeyote ile kukiwa na demand ikipanda basi na bei itapanda. Lakini bei inashuka kukiwa na mashindano. Sasa kukiwa na watu walio na hela nyingi za kutumia na kununua hiyo bidhaa basi watoa bidhaa wanapandisha bei wakijua watu wataweza kulipa.

Elimu ya juu ya University ndivyo hivyo hivyo. Kuna demand ya elimu ya juu sasahivi kwahiyo bei inapanda.

Kinachozidi kuipandisha bei ni mikopo kutoka kwa serikali kwenda kwa wanafunzi. Haijalishi hao wanafunzi wanasoma nini lakini as long as kuna hela ambayo hao wanafunzi wakiidai kutoka kwa serikali wataipata basi watoa huduma au wauza elimu ambao ni university wataongeza bei kwasababu bidhaa yao iko in demand.

Serikali haielewi matatizo inayoyasababisha kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi. Cha kwanza ni kwamba inaongeza bei ya elimu kukua kwasababu inaongeza demand.
Cha pili ni kwamba kila mtu atataka mkopo akati wengine hawana akili za kwenda elimu ya juu na wanaenda kusomea mambo ambayo hayahitaji university.
Hao wataishia kumaliza kusoma na kukosa kazi na kukosa uwezo wa kulipa mikopo.

Mikopo ingekuwa inatolewa na benki binafsi, benki zenyewe zingekuwa zinafanya jitihada kubwa zaidi ya kuchagua nani mwenye akili anayeweza kutumia mkopo huo kusoma kwa bidii na anafaa kupata mkopo. Hii ni kwasababu ingekua ni hela ya hizo benki ambazo zingepotea kama wangechagua kuwapa wanafunzi wajinga mikopo. Kwahiyo wangekua makini kuto toa mikopo ovyo ovyo na hii hatua ingepunguza idadi ya demand ambayo ingepunguza bei ya elimu ya juu.
mmmmmmmh ambao hautna akili tunaonewaga kinyamaaaa
nashukuru kaka kwa mandiko yako
 
Mi naona mpaka mtu kwanza kuvuka tu form four akili tosha. Wangapi wanashindwa? Pili mpaka anamaliza fm six nakuchaguliwa, at least anajitambua
 
Nadhani huu ni.mwendelezo wa zile hoja zako.za kuamini.kuwa hakuna umuhimu wa kuwa.na serikali. Huu ni.mtizamo wako usio na tija kwa yeyote.yule.
 
wewe ni mchumi kutoka chuo gani hapa Tanzania? Tehe tehe tehe!

hahaha niko Liberty University lakini uchumi nimesoma vitabu viwili tu ambavyo ni principles of macroeconomics na microeconomics na nimechukua darasa moja na hilo pekee limenielewesha suply and demand.
 
Nadhani huu ni.mwendelezo wa zile hoja zako.za kuamini.kuwa hakuna umuhimu wa kuwa.na serikali. Huu ni.mtizamo wako usio na tija kwa yeyote.yule.

Kwanza hapo umeruka mbali sana. Hoja yangu inahusu mikopo ya wanafunzi na inapopaswa kutoka. Wewe umerukia umuhimu wa kuwa na serikali.

Hivi unaelewa kwamba kwenye nchi zilizoendelea walivyoanza kutoa mikopo ya University kupita serikali bei ya elimu na yakwenda shule ikapanda kwa 100%. Kila pale serikali inapo toa hela itumike kwenye sekta moja hiyo sekta itapandisha bei ya huduma/bidhaa zake kwasababu inajua watu wanapata hela ya kuinunua na watu wataendelea kuzichukua hizo hela kutoka kwa serikali kwasababu wanazigawa tu ovyo ovyo.

serikali kama mpango wake ni kukuwa kwa ukubwa na matumizi kila siku na matumizi yenyewe yanatoka kwenye hela ya wananchi basi hamna maana yakuwa na serikali. Inapaswa kuwa inawaachia wananchi wawe wanakuwa kwenye kujitegemea, siyo kuwafanya wananchi waitegemee serikali.

Uhuru wa soko na wa wateja kuchagua wanachotaka ndiyo unaoleta innovation. Kulivokuwa na demand ya transportation ambayo ni bora kuliko farasi au kutembea watu wabunifu wakatengeneza suply kwasababu walikuwa na incentive. Kulivokuwa na demand ya mwanga usiotumia mafuta mtu mbunifu akatengeneza supply ya light bulb. Kulivokuwa na demand ya inventions kama air conditioning, engine, nyumba za kisasa, internet websites kama hii au facebook zote hizi zilitengenezwa na demand na supply kwenye free market. Serikali haikuhitajika. Ninachosema mimi ni serikali hisijihusishe na free market kwasababu ni wateja watakao tengeneza demand na watakao chagua bidhaa au huduma ipi ni bora.
 
Mi naona mpaka mtu kwanza kuvuka tu form four akili tosha. Wangapi wanashindwa? Pili mpaka anamaliza fm six nakuchaguliwa, at least anajitambua

Kwahiyo unachosema ni kwamba hapana haja ya kila mtu kwenda elimu ya University? Kama hiyo ndiyo mada yako hapo nakubaliana na wewe. Unakuta kazi nyingi zinaishia kuanza kuchagua watu wenye elimu ya juu kwasababu ndiyo inafanya biashara yao ionekane ya maana lakini ukiangalia watu wanachofanya kwenye hizo biashara ni mambo ambayo unahitaji tu experience ya communication, na skills za kusoma na kuandika na accounting. Yani ni mambo ya networking ambayo unahitaji tu kujua jinsi ya kutumia mitandao lakini waaajiri wanaishia kuangalia diploma kwasababu ya mtindo na umaarufu wa diploma. Ukweli ni kinachohitajika ni work ethic, communication skills, na ubunifu.
 
umechambua vizuri sana na huja andika kisiasa. Ila watu watakubishia tu bila kuwa na hoja yoyote

najua naleta fikra na hoja ambazo watanzania wengi hawajazoea. Wana imani kwamba kila kukiwa na tatizo serikali itowe hela lakini wanasahau hiyo hela inatoka wapi na kwamba muongezeko wa kutegemea hela ya serikali ni muongezeko wa kodi na deni la taifa.
 
Duh! nadhani mimi ndio kilaza kumbe kuna wewe mwenzangu unasaidia huu mzingo wa Ukilaza, Karibu sana Kilaza mwenzangu
 
serikali ipo mkuu,hujui umuhimu wa serikali kwenye price mechanism(demand and supply forces)? serikali ina wajibu wa ku-intervene endapo price mechanism itakuwa sio suluhisho la kuweka bei za huduma/bidhaa MUHIMU stable.bidhaa au huduma muhimu kama chakula,mafuta ya petrol nk zikiwa zinapanda bei kiholela(sometimes hata kushuka kwa bei kulikokithiri serikali inaingilia kati) ktk soko lazima gvt iingilie kati kwa kuweka stategies mbalimbali(price ceiling au price floor:mojawapo)ili kustabilize bei kwa bidhaa zenye umuhimu/impact kubwa kwa welfare za watu na uchumi kwa ujumla.swali,je elimu sio bidhaa/huduma muhimu? jibu ni ndio.huduma hii haiwez achwa tuu price mechanism i-decide bei yake sokoni.by the way umessugest njia lakini serikali ina nguvu ya kutunga sheria na kutoa tamko kwa taasisi za elimu na wakatii tuu.
 
Back
Top Bottom