Mikopo tarajiwa ya China kwa Tanzania inayofikia Trilioni 46 kwa ajili ya Bagamoyo Port na SGR, hatarini kushikilia vitega uchumi vya Tanzania

Inamaana sisi ni wajinga kiasi gani?
Mpaka Leo tunatembelea mambo ya Nyerere hata kama yana kasoro?

Tukae kumlaumu MTU aliyekufa zaidi ya miaka 20 iliyopita wakati sisi uwezo Wa kurekebisha tunao


Kitu ni simple tu kubadili au kurekebisha katiba baaaaasi
Unasema kweli, huwa sipendi mijadala ya kulaumu mtu ama Chama na kusahau wajibu wa waliowaweka hao madarakani.
Tusisahau kuwa, haki na wajibu ni vitu viwili vinavyoshirikiana katika masuala ya demokrasia na haki za hinadamu.

Ukiwa mzuri kudai haki zako, jitahidi pia uwe mzuri kufahamu wajibu wako katika kuzidai hizo haki hasa mipaka ya haki zako.

Kama Katiba ndilo suala muhimu, mbona wapiga kura huwa hawachagui wanaopiga kampeni za Katiba Mpya. Je, ni kosa sisi kudai kuwa, wanaodai Katiba Mpya ndio hawawaelewi wananchi wanachotaka?
 
Kuna kuchanganya mambo, nadhani kwa kutoelewa.

Mradi wa Bagamoyo ulipangwa kuwa mkopo? Hilo ni moja.

Pili, Rwanda haipitishi asilimia 40 ya bidhaa zake kupitia Bandari ya Dar Es Salaam; na wala kipande walichogomea waChina cha SGR ya Kenya sio Kisumu -Malaba ambacho hata mkopo wake ulikuwa haujajadiliwa. Kipande cha SGR toka Nakuru hadi Kisumu ndicho kimerudishwa kwenye upembuaji, mkopo ulishakubaliwa, lakini ukasitishwa hadi ionekane kama una tija.

Na hapo hapo ni muhimu pia kuelewa kwamba hata SGR ikifika Kampala, hakuna uhakika wowote kuwa itaendelea kutoka Kampala kwenda Kigali. Na hili ndilo lilikuja kuwa zito zaidi, kwa sababu M7 anaiona Sudan ya Kusini kuwa muhimu zaidi kuliko Kigali.

Kuna michanganyo mingi kwenye makala hiyo iliyobandikwa hapo juu.
 
Sisi ni wajinga wacheni wabebe kila kitu.

Watu mna katiba inayolinda watawala badala ya kulinda maliasili za nchi na mmeridhika sasa mnatarajia nini?

Katiba inaruhusu serikali kukopa inavyotaka,kuingia mikataba bila kulishirikisha Bunge,n.k. alafu mnalilia nini?!

Katiba na sheria zetu zimeacha mwanya wa kisheria miswaada inayohusu maliasili za Taifa kupelekwa na kujadiliwa Bungeni kwa hati ya dharura alafu mnatarajia nini?

Kinga ya Raisi haina mashariti yoyote hata kama atatumia madaraka vibaya kwa kuingia mikataba mibovu inayotafuna nchi eti hapaswi kushitakiwi.

Katiba hiyo hiyo imelifanya Bunge kuwa kibogoyo hivyo hata watawala wakiingia mikataba mibovu Bunge halina cha kuwafanya kwani taratibu za Bunge kuisimamia serikali ni kama za kiini macho tu.

Ni katiba hii inafanya vyama vya upinzani visiwe na sauti Bungeni kuweza kuihoji serikali kwani katiba hii inaruhusu Spika,Naibu Spika na wenyeviti wa Bunge watokane na chama cha siasa na kibaya zaidi Katiba na hata sheria zetu pamoja na kanuni za Bunge hazilazimisha uwepo wa Spika au Naibu Spika kutoka upinzani.

Watu wanapodai katiba mpya sio wajinga na bila katiba mpya yenye kuweka mifumo ya kisheria inayolinda maliasilI zetu na si watawala,siku zote tutaendelea kuwa ombaomba na tutawaliw tu na watu weupe kwa mashariti ya ushoga na mashariti mengineyo.
"Book of the People, by the Government, for the President"....... African's KATIBA
 
Kwanini habari hii imeletwa na Mamluki Mgambilwa ni Mmuntu ?
Mamluki ni wewe. Uko hapo kutetea tumbo lako na hauwezi kutofautisha kizuri kipi na kibaya kipi.
Waache wenye mawazo chanya waishauri Serikali juu ya masuala ya kiuchumi ili Serikali ifanye informed decisions.
 
View attachment 950380


Gazeti la The Guardian, lina taarifa inayoeleza kuwa, Mkopo wa China kwa Tanzania, ambao mpaka sasa ni Tsh. Trilioni 5.3 (U$ 2.347 Billion), unaweza kuongezeka maradufu hadi zaidi ya Trilioni 23 (U$ 10 Billion) endapo fedha zilizoombwa kwa ajili ya ujenzi wa Reli ya SGR (U$ 7.6 Billion), pamoja na Mradi wa Makaa ya Mawe na Chuma wa Mchuchuma-Liganga (U$ 3 Billion) utaidhinishwa.

Rais Dk. John Pombe Magufuli amekuwa akipinga kuchukua mkopo mkubwa mwingine wa Trilioni 23 (U$ 10) kwa ajili ya Mradi wa Bandari ya Bagamoyo kwani mikopo hiyo inaweza kuisababishia Tanzania kuingia deni kubwa na China linalofikia Trilioni 46 (U$ 20.6 Billion).

China bado inagumia kimoyomoyo na kuugulia maumivu ya kuumizwa kwa ego yao kwa namna Rais Dk. John Pombe Magufuli alivyofanikiwa kuruka kiunzi chao cha kumzungusha mkopo wa kujenga Reli ya SGR, kwa kuupata Uturuki. Uamuzi wa Magufuli ku-opt Waturuki ulikuwa ni wa kijasiri sana kutokana na kwamba Uturuki haijihusishi sana na Afrika kwenye miundombinu ya kisasa barani Afrika kama zilivyo China, Japan na Ulaya Magharibi.

Aidha, Tanzania ilichelewesha Mradi wa Uwekezaji wa Bandari ya Bagamoyo na kuzua hofu kwa Wachina juu ya uwezekano wa Mradi huo kusitishwa.

Hivyo, kwa namna yoyote Wachina watakuwa na hasira na Tanzania japokuwa hawawezi kuionyesha wazi wazi kutojana na kuona kuwa Tanzania ina Rais asiye na mzaha kabisa kwenye masuala ya kulinda maslahi na rasilimali za Taifa lake, huku muda wote akipigania a win-win situation.

Kenya inayodaiwa na China U$ 9.8 Billion kwa sasa inahenyeshwa sana na China, hali ambayo imepunguza hali ya utulivu wa kiuchumi nchini humo. China imesita kufadhiri SGR kipande cha Kisumu - Malaba kwa kigezo cha kuwa uneconomical.

Kenya ina uchumi mkubwa zaidi kuliko Tanzania na ukiacha Mradi wa Mafuta ya Lokichar (Turkana - Lamu Pipeline) na SGR (Mombasa - Kisumu - Malaba), haina Miradi mikubwa mingi inayoipa headache kama ilivyo kwa Tanzania ambako kuna Miradi mikubwa mingi ikiwemo:
  • Stiegler's Gorge (Rufiji HEP): gharama U$ 3.6 Billion;
  • SGR (Dar - Dodoma - Mwanza & Kigali): gharama U$ 7 Billion;
  • Bomba la Mafuta ya Uganda (Hoima - Tanga Pipeline): gharama U$ 3.5 Billion;
  • Kiwanda cha Kuchakata Gesi (LNG), Lindi: gharama U$ 30 Billion.

Endapo Mkopo huo wa U$ 7.6 Billion utaidhinishwa na China, utaifanya Tanzania ambayo kiuchumi ni ya 10 barani Afrika, ikiwa na GDP (PPP) ya U$175 Billion, kuwa ya pili nyuma tu ya Angola (yenye deni la U$ 42.8 billion) kwa Nchi zenye madeni makubwa kutoka kwa China barani Afrika. Hata hivyo, Angola ina utajiri mkubwa wa mafuta wa kuiwezesha kulipa deni hilo, tofauti na Tanzania ambayo haina chanzo kikuu cha mapato mpaka sasa.

Lisemwalo lipo, kama halipo basi laja. Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuwa, China imetaifisha vitega uchumi kadhaa katika Nchi za Djibouti, Zambia na Kenya kwa kushindwa kulipa madeni.p, kumesababisha hofu kubwa kwa Waafrika dhidi ya China; Nchi iliyoonekana kuwa kimbilio na mkombozi wa Afrika katika miaka ya 2000s lakini leo hii inaanza kuonekana Nchi isiyo na huruma kwa Waafrika.
Licha ya hatua kadhaa kuchukuliwa na Serikali ya China ya ku-address hofu hii ya Waafrika dhidi yao, bado zimeshindwa kuondoa wasiwasi huu kwa wananchi wengi hadi kuwa mojawapo ya ajenda zinazoibuka mara kwa mara katika Sera za uwekezaji na za maendeleo ya kiuchumi.

Ni wazi pia, fursa ya haraka haraka iliyoletwa na Rwanda, ilikuwa ni kubwa sana kiuchumi. Of course, kulegalega kwa kipande cha SGR kutoka Kisumu - Malaba (Kenya) kulionekana machoni mwa Wanyarwanda kuwa, Wakenya hawakuwa serious na Mradi wa SGR kutoka Mombasa - Nairobi - Kisumu - Kampala - Kigali.

Of course, ni wazi Rais Dk. John Magufuli kupitia maelewano na Paul Kagame, ilisaidia sana Rwanda kuigeukia SGR ya Tanzania, ambayo ilkuwa imeshaanza kujengwa katika kipande cha Dar - Morogoro. Sasa, unafanyaje kuifikisha haraka SGR kutoka Dar hadi pale Rusumo, Ngara? Ukichelewa, Rwanda wanaweza kubadilisha tena gia angani na kurudi kwa Wakenya.
Rwanda kwa sasa inapitishia asilimia 40% ya mizigo yake Bandari ya Dar, hivyo SGR ikikamilika, mizigo itaongezeka maradufu siyo ya Rwanda pekee bali ya Mashariki ya DRC, Burundi na Kusini mwa Uganda.

Kwa kuwa, wakati Serikali inatangaza kuanza ujenzi wa SGR na wa Stiegler's (Rufiji) Gorge, kulikuwepo matumaini makubwa kuwa, mapato yatakayokuwa yakipatikana kupitia Bomba la Mafuta ya Uganda (Hoima-Tanga Pipeline), ambayo ni Dola 12 kwa pipa (mapipa 200,000 kwa siku), sawa na Tsh. 5,500,000,000 kwa siku.
Hivyo kwa mwaka, Serikali ingekuwa inapata kodi ya Tsh. 2,000,000,000,000 (Trilioni 2). Fedha hizi zingerahisisha sana ulipaji wa madeni yoyote tuliyoingia na tunayoingia kujenga miundombinu muhimu hapa nchini.
Hata hivyo, kwa kuwa ujenzi umepelekwa tena mbele hadi mwakani 2019, inaweza ikaichukua Tanzania hadi mwaka 2021 kuanza kufaidika na mafuta ya Uganda.

Vilevile, Mradi mwingine mkubwa na super wa kuchakata gesi (LNG), mkoani Lindi, ulionekana kuwa mkombozi mkubwa sana kwa mapato serikalini, huku ukikadiriwa kuwa na uwezo wa kuiingizia Tanzania Tsh. 5,000,000,000,000 (Trilioni 5) kwa mwaka.

Baada ya Makubaliano na Kampuni za Gesi kukwama, Serikali yajipanga upya: Kiwanda cha LNG kuiletea Tanzania Tsh. 5,000,000,000,000 kwa mwaka. - JamiiForums

Ushauri:
Ni vyema Serikali iangalie upya makubaliano ya kukopeshwa fedha za ujenzi wa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ili kuangalia namna ya kuusogeza mbele ujenzi wake ama kusogeza mbele Mpangala wa kulipa mkopo huo.

Serikali iahirishe kwa muda kuchukua mkopo kwa ajili ya ujenzi wa SGR, kipande cha kuanzia Dodoma - Tabara - Mwanza & Kigali ili kusubiri majaliwa ya mapato ya Bomba la Mafuta, mwaka 2021. Hii ni kwa sababu inawezekana ujenzi huo ukachukua muda mrefu zaidi ya mwaka 2021 unaotajwa. Ikumbukwe, awali uzalishaji ulipangwa kuanza mwaka 2019 lakini ikashindikana.

Serikali ihusishe Bunge, juu ya mkwamo wa LNG kwani ndiyo njia pekee ya uhakika kwa sasa ya kuongeza mapato maradufu serikalini. Na kwa kuwa ujenzi unachukua muda mrefu wa hadi miaka mitano, hivyo ni ngumu kuwa na uhakika na bill ya deni la China litajavyokuwa kufikia miaka ya 2023, kipindi ambacho tunaweza kuwa katika mazingira mazuri ya kuweka kuchakata gesi.


View attachment 950402
nimekuelewa sana na uzi wako huu matata good job
 
Mi sikumbuki tumechukua lini mkopo wa uturuki...
Bandari ya bagamoyo ni bonge ya project na ina faida kubwa mno kiuchumi,

hili la kusema wachina wanataifisha njia kuu za uchumi ni propaganda za magharibi tu ili ku counter chinese influence Africa,
hatujasikia mpaka leo hiyo zambia kama kweli imenunuliwa na china au ni mambo ya propaganda,
hivi karibuni china walichukua uendeshaji wa bandari ya israel ya Haifa,
hilo lingefanyika Africa wangesema china imetaifisha,
kwa mawazo yetu tunataka china ije ijenge project ya bagamoyo bure,bila wao kurudisha pesa zao,
hilo halipo,
mtajengewa maktaba bure lakini sio mradi mkubwa kama bandari ya bagamoyo
 
Huyo Nyerere ndiye aliyesumbuka kuleta uhuru lakini ndiye aliyeliunganisha Taifa kwa kiwango kikubwa. Amani ya Tanzania inatokana na vita ya Nyerere kwa ukabila. Isingekuwa Nation-building effort za Nyerere, Tanzania isingekuwa na tofauti na majirani zake ambao hupigana mara kwa mara kutokana na Viongozi wao wa awali kukazania uchumi kwa gharama ya amani, umoja na mshikamano.

Mwenge wa Uhuru unaweza kuwa unadharauliwa kwa sasa lakini believe me, ni moja ya alama muhimu kwa Tanzania kwa namna ulivyoiunganisha Nchi hii hasa miaka ya nyuma.
umenena vizuri sana Mkuu.
 
Chanzo ya katiba mbovu wa kulaumiwa ni Nyerere ndo alieleta shida hii,alitukuza utawala badala ya uchumi. Katiba chakavu ya MWALIMU si katiba ya kizazi cha sasa
Wewe una matatizo kichwani si bbure, hadi leo unawaza eti kumlaumu Nyerere? Nyerere katawala miaka 27, baada ya kuacha madaraka 1985 aliingia Mwinyi (10yrs), Mkapa (10yrs), Kikwete (10yrs), Magufuli (3yrs). Jumla miaka 33.
Sasa wewe unayewaza kumlaumu Nyerere yawezekana unafikiri bado ni rais maana kuna mabongolala mengine hayajui Nyerere aliacha kuwa rais kabla hawajazaliwa.
 
Ni raia wa kawaida wanaoumia na maamuzi ya viongozi wa nchi za dunia ya tatu, ambayo kwa kawaida huamuliwa kama ya kifamilia. Mabunge yakishirikishwa, hushurutishwa kupitisha maamuzi ya ajabu.
 
View attachment 950380


Gazeti la The Guardian, lina taarifa inayoeleza kuwa, Mkopo wa China kwa Tanzania, ambao mpaka sasa ni Tsh. Trilioni 5.3 (U$ 2.347 Billion), unaweza kuongezeka maradufu hadi zaidi ya Trilioni 23 (U$ 10 Billion) endapo fedha zilizoombwa kwa ajili ya ujenzi wa Reli ya SGR (U$ 7.6 Billion), pamoja na Mradi wa Makaa ya Mawe na Chuma wa Mchuchuma-Liganga (U$ 3 Billion) utaidhinishwa.

Rais Dk. John Pombe Magufuli amekuwa akipinga kuchukua mkopo mkubwa mwingine wa Trilioni 23 (U$ 10) kwa ajili ya Mradi wa Bandari ya Bagamoyo kwani mikopo hiyo inaweza kuisababishia Tanzania kuingia deni kubwa na China linalofikia Trilioni 46 (U$ 20.6 Billion).

China bado inagumia kimoyomoyo na kuugulia maumivu ya kuumizwa kwa ego yao kwa namna Rais Dk. John Pombe Magufuli alivyofanikiwa kuruka kiunzi chao cha kumzungusha mkopo wa kujenga Reli ya SGR, kwa kuupata Uturuki. Uamuzi wa Magufuli ku-opt Waturuki ulikuwa ni wa kijasiri sana kutokana na kwamba Uturuki haijihusishi sana na Afrika kwenye miundombinu ya kisasa barani Afrika kama zilivyo China, Japan na Ulaya Magharibi.

Aidha, Tanzania ilichelewesha Mradi wa Uwekezaji wa Bandari ya Bagamoyo na kuzua hofu kwa Wachina juu ya uwezekano wa Mradi huo kusitishwa.

Hivyo, kwa namna yoyote Wachina watakuwa na hasira na Tanzania japokuwa hawawezi kuionyesha wazi wazi kutojana na kuona kuwa Tanzania ina Rais asiye na mzaha kabisa kwenye masuala ya kulinda maslahi na rasilimali za Taifa lake, huku muda wote akipigania a win-win situation.

Kenya inayodaiwa na China U$ 9.8 Billion kwa sasa inahenyeshwa sana na China, hali ambayo imepunguza hali ya utulivu wa kiuchumi nchini humo. China imesita kufadhiri SGR kipande cha Kisumu - Malaba kwa kigezo cha kuwa uneconomical.

Kenya ina uchumi mkubwa zaidi kuliko Tanzania na ukiacha Mradi wa Mafuta ya Lokichar (Turkana - Lamu Pipeline) na SGR (Mombasa - Kisumu - Malaba), haina Miradi mikubwa mingi inayoipa headache kama ilivyo kwa Tanzania ambako kuna Miradi mikubwa mingi ikiwemo:
  • Stiegler's Gorge (Rufiji HEP): gharama U$ 3.6 Billion;
  • SGR (Dar - Dodoma - Mwanza & Kigali): gharama U$ 7 Billion;
  • Bomba la Mafuta ya Uganda (Hoima - Tanga Pipeline): gharama U$ 3.5 Billion;
  • Kiwanda cha Kuchakata Gesi (LNG), Lindi: gharama U$ 30 Billion.

Endapo Mkopo huo wa U$ 7.6 Billion utaidhinishwa na China, utaifanya Tanzania ambayo kiuchumi ni ya 10 barani Afrika, ikiwa na GDP (PPP) ya U$175 Billion, kuwa ya pili nyuma tu ya Angola (yenye deni la U$ 42.8 billion) kwa Nchi zenye madeni makubwa kutoka kwa China barani Afrika. Hata hivyo, Angola ina utajiri mkubwa wa mafuta wa kuiwezesha kulipa deni hilo, tofauti na Tanzania ambayo haina chanzo kikuu cha mapato mpaka sasa.

Lisemwalo lipo, kama halipo basi laja. Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuwa, China imetaifisha vitega uchumi kadhaa katika Nchi za Djibouti, Zambia na Kenya kwa kushindwa kulipa madeni.p, kumesababisha hofu kubwa kwa Waafrika dhidi ya China; Nchi iliyoonekana kuwa kimbilio na mkombozi wa Afrika katika miaka ya 2000s lakini leo hii inaanza kuonekana Nchi isiyo na huruma kwa Waafrika.
Licha ya hatua kadhaa kuchukuliwa na Serikali ya China ya ku-address hofu hii ya Waafrika dhidi yao, bado zimeshindwa kuondoa wasiwasi huu kwa wananchi wengi hadi kuwa mojawapo ya ajenda zinazoibuka mara kwa mara katika Sera za uwekezaji na za maendeleo ya kiuchumi.

Ni wazi pia, fursa ya haraka haraka iliyoletwa na Rwanda, ilikuwa ni kubwa sana kiuchumi. Of course, kulegalega kwa kipande cha SGR kutoka Kisumu - Malaba (Kenya) kulionekana machoni mwa Wanyarwanda kuwa, Wakenya hawakuwa serious na Mradi wa SGR kutoka Mombasa - Nairobi - Kisumu - Kampala - Kigali.

Of course, ni wazi Rais Dk. John Magufuli kupitia maelewano na Paul Kagame, ilisaidia sana Rwanda kuigeukia SGR ya Tanzania, ambayo ilkuwa imeshaanza kujengwa katika kipande cha Dar - Morogoro. Sasa, unafanyaje kuifikisha haraka SGR kutoka Dar hadi pale Rusumo, Ngara? Ukichelewa, Rwanda wanaweza kubadilisha tena gia angani na kurudi kwa Wakenya.
Rwanda kwa sasa inapitishia asilimia 40% ya mizigo yake Bandari ya Dar, hivyo SGR ikikamilika, mizigo itaongezeka maradufu siyo ya Rwanda pekee bali ya Mashariki ya DRC, Burundi na Kusini mwa Uganda.

Kwa kuwa, wakati Serikali inatangaza kuanza ujenzi wa SGR na wa Stiegler's (Rufiji) Gorge, kulikuwepo matumaini makubwa kuwa, mapato yatakayokuwa yakipatikana kupitia Bomba la Mafuta ya Uganda (Hoima-Tanga Pipeline), ambayo ni Dola 12 kwa pipa (mapipa 200,000 kwa siku), sawa na Tsh. 5,500,000,000 kwa siku.
Hivyo kwa mwaka, Serikali ingekuwa inapata kodi ya Tsh. 2,000,000,000,000 (Trilioni 2). Fedha hizi zingerahisisha sana ulipaji wa madeni yoyote tuliyoingia na tunayoingia kujenga miundombinu muhimu hapa nchini.
Hata hivyo, kwa kuwa ujenzi umepelekwa tena mbele hadi mwakani 2019, inaweza ikaichukua Tanzania hadi mwaka 2021 kuanza kufaidika na mafuta ya Uganda.

Vilevile, Mradi mwingine mkubwa na super wa kuchakata gesi (LNG), mkoani Lindi, ulionekana kuwa mkombozi mkubwa sana kwa mapato serikalini, huku ukikadiriwa kuwa na uwezo wa kuiingizia Tanzania Tsh. 5,000,000,000,000 (Trilioni 5) kwa mwaka.

Baada ya Makubaliano na Kampuni za Gesi kukwama, Serikali yajipanga upya: Kiwanda cha LNG kuiletea Tanzania Tsh. 5,000,000,000,000 kwa mwaka. - JamiiForums

Ushauri:
Ni vyema Serikali iangalie upya makubaliano ya kukopeshwa fedha za ujenzi wa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ili kuangalia namna ya kuusogeza mbele ujenzi wake ama kusogeza mbele Mpangala wa kulipa mkopo huo.

Serikali iahirishe kwa muda kuchukua mkopo kwa ajili ya ujenzi wa SGR, kipande cha kuanzia Dodoma - Tabara - Mwanza & Kigali ili kusubiri majaliwa ya mapato ya Bomba la Mafuta, mwaka 2021. Hii ni kwa sababu inawezekana ujenzi huo ukachukua muda mrefu zaidi ya mwaka 2021 unaotajwa. Ikumbukwe, awali uzalishaji ulipangwa kuanza mwaka 2019 lakini ikashindikana.

Serikali ihusishe Bunge, juu ya mkwamo wa LNG kwani ndiyo njia pekee ya uhakika kwa sasa ya kuongeza mapato maradufu serikalini. Na kwa kuwa ujenzi unachukua muda mrefu wa hadi miaka mitano, hivyo ni ngumu kuwa na uhakika na bill ya deni la China litajavyokuwa kufikia miaka ya 2023, kipindi ambacho tunaweza kuwa katika mazingira mazuri ya kuweka kuchakata gesi.


View attachment 950402
There is no justification to construct/build another port at Bagamoyo! The question is, are these three ports of Dar, Tanga & Mtwara been fully utilised? The answer is no!
 
Sisi ni wajinga wacheni wabebe kila kitu.

Watu mna katiba inayolinda watawala badala ya kulinda maliasili za nchi na mmeridhika sasa mnatarajia nini?

Katiba inaruhusu serikali kukopa inavyotaka,kuingia mikataba bila kulishirikisha Bunge,n.k. alafu mnalilia nini?!

Katiba na sheria zetu zimeacha mwanya wa kisheria miswaada inayohusu maliasili za Taifa kupelekwa na kujadiliwa Bungeni kwa hati ya dharura alafu mnatarajia nini?

Kinga ya Raisi haina mashariti yoyote hata kama atatumia madaraka vibaya kwa kuingia mikataba mibovu inayotafuna nchi eti hapaswi kushitakiwi!

Katiba hiyo hiyo imelifanya Bunge kukosa meno hivyo hata watawala wakiingia mikataba mibovu Bunge halina cha kuwafanya kwani taratibu za Bunge kuisimamia serikali ni kama za kiini macho tu.

Ni katiba hii inafanya vyama vya upinzani visiwe na sauti Bungeni kuweza kuihoji serikali kwani katiba hii inaruhusu Spika,Naibu Spika na wenyeviti wa Bunge watokane na chama cha siasa na kibaya zaidi Katiba na hata sheria zetu pamoja na kanuni za Bunge hazilazimisha uwepo wa Spika au Naibu Spika kutoka upinzani.

Watu wanapodai katiba mpya sio wajinga, bali wanajua umuhimu wake na tujue bila katiba mpya yenye kuweka mifumo ya kisheria inayolinda maliasilI zetu na si watawala,siku zote tutaendelea kuwa ombaomba na tutawaliwa tu na watu weupe kwa mashariti ya ushoga na mashariti mengineyo watakayopenda kutuwekea.
Maajabu kuna binadamu watakwambia hayo uliyosema siyo kipaumbele cha watanzania eti wa tanzania wanataka barabala na maji. "Mungu rudi upesi tupumnzike"
 
There is no justification to construct/build another port at Bagamoyo! The question is, are these three ports of Dar, Tanga & Mtwara been fully utilised? The answer is no!

Mkuu, chukua muda ulitafakari vizuri hilo swali la Bandari ya Bagamoyo pamoja na vikorombwezo vinavyohusika na mradi huo.

Ni dhahiri kabisa kwa mawazo yako haya hapa hujakaa ukaliwaza vizuri jambo hili. Soma taarifa mbali mbali zinazohusu mradi huo ujiridhishe kabisa kuwa unao uelewa mzuri.

Ukimaliza kufanya hivyo, usiwe mlafi, rudi hapa utumwagie madini mapya uliyogundua katika utafiti wako huo.

Bagamoyo ni Johari mpya kwa Tanzania ya kesho na keshokutwa. Tazama li-nchi hilo hapo kubwa kabisa uani kwako, halafu uje useme huoni faida ya mradi huo, wewe utakuwa ni mlemavu wa macho.
 
Wewe una matatizo kichwani si bbure, hadi leo unawaza eti kumlaumu Nyerere? Nyerere katawala miaka 27, baada ya kuacha madaraka 1985 aliingia Mwinyi (10yrs), Mkapa (10yrs), Kikwete (10yrs), Magufuli (3yrs). Jumla miaka 33.
Sasa wewe unayewaza kumlaumu Nyerere yawezekana unafikiri bado ni rais maana kuna mabongolala mengine hayajui Nyerere aliacha kuwa rais kabla hawajazaliwa.
Ujui historia,katiba iliyopo Ni lini ilifanyiwa mabadiliko, alieanzisha Kofia Mbili ni nani?
 
Unasema kweli, huwa sipendi mijadala ya kulaumu mtu ama Chama na kusahau wajibu wa waliowaweka hao madarakani.
Tusisahau kuwa, haki na wajibu ni vitu viwili vinavyoshirikiana katika masuala ya demokrasia na haki za hinadamu.

Ukiwa mzuri kudai haki zako, jitahidi pia uwe mzuri kufahamu wajibu wako katika kuzidai hizo haki hasa mipaka ya haki zako.

Kama Katiba ndilo suala muhimu, mbona wapiga kura huwa hawachagui wanaopiga kampeni za Katiba Mpya. Je, ni kosa sisi kudai kuwa, wanaodai Katiba Mpya ndio hawawaelewi wananchi wanachotaka?
wewe nae ni mjinga pia
 
Back
Top Bottom