Mikopo serikalini ni chanzo wazazi/ndugu kubweteka na kushindwa kusomesha vijana elimu ya juu

fierceman

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
553
757
habar wana jf

naweza sema wazazi/ndugu wamekuwa wavivu kufanya bidii ya kutosha kutafuta pesa ili vijana wakasome elimu ya juu kwa kutegemea mikopo toka serikalini
binafsi nachukia sana mikopo naona ni kama sehemu ya kukandamiza vijana maishani...yani unakuta kijana hata kijiko au godoro hajaanza miliki ila anaanza na deni si chini ya milioni 10 toka serikalini

tujiulize hivi serikali ingekuwa haito mikopo je vijana wasingeweza kweli kusoma elimu ya juu kwa sababu za kifedha?
katika nchi zilizoendelea mtoto kuanzia awali hadi chuo kikuu anasoma kwa pesa ya wazazi/ndugu na si serikali kwa kuwa haitoi mikopo

tunapozaa watoto tunakuwa hatujui kuwa itawabidi wasome,wale,wavae na kulala pazuri sasa je hili ni jukumu la serikali au wazazi/ndugu?

kiupande wangu naona kabisa wazazi/ndugu wanawaombea vijana wao mikopo serikalini si kwamba hawana pesa bali ni mazoea tu waliyojiwekea kwa kuwa wanajua mikopo hiyo italipwa na vijana wao wenyewe wapatapo ajira na si wao sababu mkopo ni mkataba kati ya serikali na mwanafunzi na si wazazi/ndugu...sasa hapa inakuwa kama wazazi/ndugu wanabebesha mzigo vijana wao

kwa wale vijana mlioshindwa kwenda vyuoni sababu mmekosa mikopo msikate tamaa muwapo mtaani mtafute pesa mkasome muache ubishoo na usistadu fanyeni kazi halali msitegemee sana wazazi/ndugu na kama unaona wewe huwezi jisomesha hivi jiulize katika umri wako huo wa miaka18+ ghafla wazazi/ndugu hawapo duniani na serikali haitoi mikopo nani angekusomesha?
na kuwa mtaani si kwamba ndio mwisho wako sababu hata leo hii ungekwenda chuo bado mtaani utarudi tu...tafuta pesa ukasome huku ukiwa umeacha biashara zako mtaani
 
nikiongezea kitu kingine kinachowafanya wazazi/ndugu zetu kushindwa kusomesha ni ukosefu wa ushirikiano mzuri katika familia na koo kiujumla
kuifupi kama koo ina upendo basi hakuna kijana ambaye atashindwa soma kwa maana unakuta katika koo familia kama 3,4 ,5,10 na kuendelea zinashirikiana vyema katika kusomesha vijana wao hakika hiyo koo itakuwa ni koo ya wasomi milele lakini kama hakuna ushirikiano hiyo koo itakuwa na watu wakuishia form 4 hadi form 6

namaliza kwa kusema ukitaka uliweze jambo inakubidi ulivae kwanza ni sawa na mtoto wa kiume asemavyo awezi lea mtoto sababu hana pesa na kazi ya kufanya ila akiweka mimba sehemu ilo jukumu atalivaa tu na kuliweza...watanzania wenzagu tuache kuiogopa milioni kwa kuitamka tu mdomoni tukifanya jitihadi ni pesa ndogo sana hiyo....!

nasema haya yote baada ya kuona vijana wengi wameshindwa kwenda chuo sababu wamekosa mikopo na wengine wamekata tamaa kabisa ya kusoma tena

nawasilisha na najua kuna watu wataongea kama wamekatwa vichwa vile kwa kuwa wanauwezo mdogo wa kufikiri
 
Kama serikali inakopa kwanini mtu binafsi tena mwanafunzi ambaye ni mtoto wa masikini iwe nongwa??

Acha roho mbaya mkuu acha serikali ikopeshe watoto wa masikini wajikomboe na kukomboa familia zao. Wewe kama uko vizuri kiuchumi wasaidie wanaoomba mikopo walipie ada hizo mkuu ili tukupongeze kwa uzalendo.
 
lete hoja utazoweza nishawishi ni badili idea yangu usiwe unapopoma tu
Maisha halisi ya watanzia nadhan unayajua, gharama za kumudu masomo elimu ya juu ni kubwa mno, kiasi kwamba kwa maisha ya mkulima wa jembe la mkono anayetegemea kilimo cha msimu n ngumu sana kuzimdu ,think twice
 
Kama serikali inakopa kwanini mtu binafsi tena mwanafunzi ambaye ni mtoto wa masikini iwe nongwa??

Acha roho mbaya mkuu acha serikali ikopeshe watoto wa masikini wajikomboe na kukomboa familia zao. Wewe kama uko vizuri kiuchumi wasaidie wanaoomba mikopo walipie ada hizo mkuu ili tukupongeze kwa uzalendo.
mkuu serikali kukopa si kwamba haina pesa bali ni utaratibu ambao umewekwa kwa lengo la kubebana tu kiuchumi na ndio maana hakuna serikali isiyo na deni....na unaposema familia za masikini hivi unajua kweli maana ya masikini?
hii ndio shida ya sisi watanzania kuishi kwa kulinganisha zaidi alafu tanapenda kulinganisha udhaifu tu na si uimara...?

bado narudi kwenye swali langu palepale je kusingekuwa na mikopo toka serikalini vijana wangeshindwa kusoma elimu ya juu kwa kigezo cha fedha?
 
mkuu serikali kukopa si kwamba haina pesa bali ni utaratibu ambao umewekwa kwa lengo la kubebana tu kiuchumi na ndio maana hakuna serikali isiyo na deni....na unaposema familia za masikini hivi unakua kweli maana ya masikini?
hii ndio shida ya sisi watanzania kuishi kwa kulinganisha zaidi alafu tanapenda kulinganisha udhaifu tu na si uimara...?

bado narudi kwenye swali langu palepale je kusingekuwa na mikopo toka serikalini vijana wangeshindwa kusoma elimu ya juu kwa kigeza cha fedha?
Nikijbu swali lako la msingi ni kwamba, baadhi wangesoma na wengine wasingepata elimu ya juu kwa sababu za kimasikini mkuu.

Kwa sisi ambao tunaishi vijijini tunabmengi ya kusimulia......mama au baba anaamka asubuhi kwenda kulima kibarua cha 1500 hapo ndio familia ile je huyo mzazi atamudua kulipia mamilioni ya chuo kikuu bila mkopo?

Tanzania na Afrika yote bado tuna safari ndefu kujikwamua kiuchumi na kuweza kumudu gharama za huduma mbalimbali.


Ni hiyo ni elimu tu bado afya, maji, malazi, chakula bora, umeme......mkuu haya mambo yanahitaji mjadala mpana sana. Chukulia mfano Rais alipotangaza elimu bure kwanini uandikishaji wa wanafunzi wa darasa kwanza ulipanda kwa zaidi ya 100%?
 
Maisha halisi ya watanzia nadhan unayajua, gharama za kumudu masomo elimu ya juu ni kubwa mno, kiasi kwamba kwa maisha ya mkulima wa jembe la mkono anayetegemea kilimo cha msimu n ngumu sana kuzimdu ,think twice
mkuu nani kakuaminisha kuwa mkulima wa jembe la mkono ni moja ya mfano wa watu ambao hawajiwezi kifedha alafu jiulize huyo mtu analima ili atafute pesa sasa je pesa yake hiyo iko kwa ajili ya matumizi gani?
ukiwa na utaratibu mzuri wa pesa hakuna kitu kigumu kitakacho hitaji pesa na ukashindwa kuafford
 
Unaweza ukawa una point ila kuna familia naamini haziwezi kumudu gharama za kusomesha vijana wao chuo mfano kuna vyuo ada ni hadi 6.7M hapo bado meals and accomodation..mkuu sio mchezo

Lakini pia nakubaliana na wewe kuwa kuna familia zimebweteka tu kwa kuona serikali inaweza kukopesha kupitia bodi yao,,lakini kama bodi hiyo isingekuwepo bado wangekuwa na uwezo mzuri tu wa kusomesha vijana wao..

Nikukumbushe tu kuwa hata marekani kuna system ya mikopo kwa ajili ya elimu kwa wasioweza kulipia gharama kwa mara moja..sema kwa sababu wenzetu wanajua nini wanafanya basi kila mtu anabeba jukumu lake
 
Nikijbu swali lako la msingi ni kwamba, baadhi wangesoma na wengine wasingepata elimu ya juu kwa sababu za kimasikini mkuu.

Kwa sisi ambao tunaishi vijijini tunabmengi ya kusimulia......mama au baba anaamka asubuhi kwenda kulima kibarua cha 1500 hapo ndio familia ile je huyo mzazi atamudua kulipia mamilioni ya chuo kikuu bila mkopo?

Tanzania na Afrika yote bado tuna safari ndefu kujikwamua kiuchumi na kuweza kumudu gharama za huduma mbalimbali.


Ni hiyo ni elimu tu bado afya, maji, malazi, chakula bora, umeme......mkuu haya mambo yanahitaji mjadala mpana sana. Chukulia mfano Rais alipotangaza elimu bure kwanini uandikishaji wa wanafunzi wa darasa kwanza ulipanda kwa zaidi ya 100%?
sawa mkuu ila kumbuka uandikishaji wa watoto wa darasa la kwanza ulipanda si kwamba et watanzania wengi walipenda somesha ila kuna kitisho mkuu wa nchi alikitoa akisema kwamba ole wake aone mtoto yuko mtaani na wakati elimu ya msingi na sekondari ni bure alaf katika maelezo yangu kwenye uzi nimemgusia kijana mwenyewe anapaswa afanye nini ebu soma tena utaona iyo sehemu na ukitaka kuona maajabu ya watanzania sisi angalia takwimu ya uandikishaji wa watoto mwanzo na baada ya mda fulani utakuta idadi ya watoto mashuleni imepungua sasa je wanakwenda wapi wakati elimu ni bure?
 
Kama serikali inakopa kwanini mtu binafsi tena mwanafunzi ambaye ni mtoto wa masikini iwe nongwa??

Acha roho mbaya mkuu acha serikali ikopeshe watoto wa masikini wajikomboe na kukomboa familia zao. Wewe kama uko vizuri kiuchumi wasaidie wanaoomba mikopo walipie ada hizo mkuu ili tukupongeze kwa uzalendo.

Kama ulimsoma na kumuelewa mleta mada nadhani hakuna popote aliposema kuwa serekali isiwakopeshe vijana wetu hela ya vyuo vikuu.
Tatizo ni kwamba; Serekali hiyo hiyo badala ya kukubali kuwa haijisumbui sana kufikiri habari za hao vijana, imeweka mlolongo mreefu namna ya kuupata huo mkopo na hata hivyo vijana/wazazi wamepambana na hivyo vizuizi na kufanikiwa kuvishinda. Mwishoni pia wakakuta giza nene. Hakuna mkopo.
Sasa, tusibweteke kuwa tutapata mikopo. Tukomae hivyo hivyo hadi kieleweke. Tuufuate huo ushauri kuwa; Turudi kwenye "Koo" zetu. Tushikamane. Kama kijana wetu ameweza kutuonesha kuwa akili zipo, ametuletea div. 1 au2 nzuri tumsaidie. Twende hata makanisani na misikitini tuwasomeshe hawa ":vichwa" na mafanikio tutayaona baadaye. Mbona tunawachangia hawa hawa kwa ajili ya ubarikio na maarusi mamilioni ya fedha?
Ila, kwa watoto hawa wa siku hizi; Sidhani kama nitamchangia mtoto wa mtu tena. Si kwa nia mbaya lakini hiki kizazi kisichomjua mkubwa nakihofia. Ukimkuta kaketi kwenye daladala sahau akupishe. Ukiwa naye njiani, japo anakufahamu kuwa wewe ni baba flan mtaani kwao, hilo zigo utalibeba mwenyewe hadi kwenyu. Kha! Nitoe msaada wa nini??
 
sawa mkuu ila kumbuka uandikishaji wa watoto wa darasa la kwanza ulipanda si kwamba et watanzania wengi walipenda somesha ila kuna kitisho mkuu wa nchi alikitoa akisema kwamba ole wake aone mtoto yuko mtaani na wakati elimu ya msingi na sekondari ni bure alaf katika maelezo yangu kwenye uzi nimemgusia kijana mwenyewe anapaswa afanye nini ebu soma tena utaona iyo sehemu na ukitaka kuona maajabu ya watanzania sisi angalia takwimu ya uandikishaji wa watoto mwanzo na baada ya mda fulani utakuta idadi ya watoto mashuleni imepungua sasa je wanakwenda wapi wakati elimu ni bure?
Mkuu ushauri ulioutoa kwa vijana qanaoshindwa kuendelea na masomo hawawezi kuufanyia kazi sababu hiki ni kizazi doti com. Fanya utafiti mdogo tu kwa wale vijana waliomaliza chuo na wengine kufeli kidato cha nne hawana walifanyalo wamekaa kama mazombi tu.

Hawafanyi kazi yoyote ya kujiingizia kipato kisa wana elimu ya chuo kikuu na hawawezi kufanya kazi ngumu. Wanajiita wasomi.
 
Mkuu ushauri ulioutoa kwa vijana qanaoshindwa kuendelea na masomo hawawezi kuufanyia kazi sababu hiki ni kizazi doti com. Fanya utafiti mdogo tu kwa wale vijana waliomaliza chuo na wengine kufeli kidato cha nne hawana walifanyalo wamekaa kama mazombi tu.

Hawafanyi kazi yoyote ya kujiingizia kipato kisa wana elimu ya chuo kikuu na hawawezi kufanya kazi ngumu. Wanajiita wasomi.
sawa mkuu kama na wewe umeliona hilo ndio maana nimewaambia waache ubishoo na usistaduu waache kuthaminisha elimu zao wafanye kazi ilimradi tu ziwe za halali....na si kwamba et ajira hazipo kwa asilimia mia laasha zipo nyingi tu sema vijana wetu wamekuwa wa kuchagua sana cha kufanya
 
sawa mkuu kama na wewe umeliona hilo ndio maana nimewaambia waache ubishoo na usistaduu waacha kuthaminisha elimu zao wafanye kazi ilimradi tu ziwe za halali....na si kwamba et ajira hazipo kwa asilimia mia laasha zipo nyingi tu sema vijana wetu wamekuwa wa kuchagua sana cha kufanya
Kweli mkuu siku hizi tunaoenda sana kitonga lakini kuna nyingi ukiondoa huzi ajira za maofisini zilizojaa manyanyaso kuna fursa nyingi sana kama vile uvuvi,kilimo,ufugaji,biashara vijana tujikite huko na serikali itengeneze maizngira wezeshi ya kufanikisha fursa hizo.
 
ungeshauri serkali kupunguza ada ya vyuo na hata mamlaka za ukopeshaji ziwe nje ya serkali ili mkopaji aamue wapi apate mkopo na kwa masharti nafuu.
kuwa nchi zlizoendelea wanajisomesha wafunz nadhani hujafuatilia kwa undani.
 
ungeshauri serkali kupunguza ada ya vyuo na hata mamlaka za ukopeshaji ziwe nje ya serkali ili mkopaji aamue wapi apate mkopo na kwa masharti nafuu.
kuwa nchi zlizoendelea wanajisomesha wafunz nadhani hujafuatilia kwa undani.
sawa mkuu lakini kiufupi hakuna chuo cha serikali ambacho kinatoa programmes ambazo ada zake kuanzia milion 2 programm yenye ada kubwa serikalini ni medical doctor ambayo ni milion 1.8 sasa na kuna vyuo vya binafsi hapahapa tanzania ambayo programm hiyo ni kuanzia milion 5 hadi 7 sasa je we unataka serikali ifanyaje au ituhurumiaje na wanafanya hivyo ili hata mtoto ambaye mzazi wake hana uwezo mkubwa naye aweze kusoma but people still fail
 
Mkuu hujui maana ya ufukara

Ili upate exposure karibu kutembea vijijin uone jinsi maisha halisi yalivyo

Sikatai Kuna wazazi wazembe wasiojushughulisha ila Kuna wazazi wanapambana sana lkn mambo hayabadiliki
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom