Mikopo na madeni nimepoteza amani na watu ninaowapenda. Nimekuwa mzigo kwa familia. Nitasimama tena?

Hukujarb kuuza illegal issues ufidie deni
2018 nilikuwa na ndoto kubwa, niliona matumaini na mafanikio ya kiuchumi. Nilikopa nikawekeza, 2019 mambo yalibadirika biashara zikagoma kwa uzembe na nyingine ilikuwa lazima zife hasa za kilimo mvua ilisomba mazao. Madeni yakaingia yakakuwa , nikakwama siwezi yalipa yote, wadai hawaelewi ukiwaambia ukweli wanaona unawadharau, ukiomba muda zaidi hawaelewi wanataka niwape tumaini kuwa nitawalipa haraka naogopa kudanganya, nakaa kimya nikiendelea kuomba Mungu afungue milango nilipe madeni ya watu. Nashukuru Mungu familia inanilisha . Ni mtumishi mshahara mdogo nalipa madeni wote hata sadaka sibakiwi nayo. Nashukuru kazini ni karibu sihitaji nauli. Madeni mabaya wapendwa, ukiweza usikope kabisa , nimeharibu undugu, urafiki ,familia, naishi kwa Neema ya Mungu na kuomba nisipate stress. Mbinu zote za kibinadamu nimetumia ili nilipe madeni nimeshindwa, sasa hivi natumaini Mungu tu. Wapendwa msikope madeni in utumwa in kifungo kibaya.
 
Ndugu tupo wengi kwenye hili ila tunapambana hapo usingz hauj kbsa, asikuambie mtuaden yanatesa
 
Madeni hayafai japo ni ya lazima. Utavuka na kuondoka katika utumwa huo. Na utakuwa umejifunza kitu!
20201219_070558.jpg
 
Pole mkuu endelea kupambana wewe ni mwanaume na ujitahidi kidogo unachopata upunguze madeni mkuu sababu huna majukumu
 
Madeni huwa yanavuruga sana aisee, nilimkopesha rafiki yangu tukavutana sana. Ikawa tena hapokei calls zangu. Ikabidi nimsake anapopatikana anieleze kinagaubaga nini kinamsibu. Aisee mambo alokuwa anapitia nikajikuta mimi kumbe shida zangu zina kaunafuu. Ikabidi tu nimsamehe deni nimtafutie na zingine zimboost kidogo.

Kuna wakati mambo yanavurugika hadi unahisi dunia imekuelemea. Usikate tamaa mkuu, pambana tu kitaeleweka.
Auntie acha tu mwenyewe namdai laki 6 rafiki yangu imenibidi tu nimwache akijisikia kunipa atanipa ila nimeshamwambia sitamdai hapo kati alikuwa anapitia kipindi kigumu ila sasa hivi naona amerudi kwenye hali yake
 
Namchukia sana mtu anayekopa halafu harejeshi kwa mujibu wa makubaliano
Wewe sio mwelewa na mbinafsi.
Rejea habari ya mleta uzi...alikuwa na malengo thabiti lkn yameenda kinyume, mvua imesomba mazao unategemea sksyarudishe?
 
2018 nilikuwa na ndoto kubwa, niliona matumaini na mafanikio ya kiuchumi.

Nilikopa nikawekeza, 2019 mambo yalibadirika biashara zikagoma kwa uzembe na nyingine ilikuwa lazima zife hasa za kilimo mvua ilisomba mazao.

Madeni yakaingia yakakuwa , nikakwama siwezi yalipa yote, wadai hawaelewi ukiwaambia ukweli wanaona unawadharau, ukiomba muda zaidi hawaelewi wanataka niwape tumaini kuwa nitawalipa haraka naogopa kudanganya, nakaa kimya nikiendelea kuomba Mungu afungue milango nilipe madeni ya watu.

Nashukuru Mungu familia inanilisha . Ni mtumishi mshahara mdogo nalipa madeni wote hata sadaka sibakiwi nayo. Nashukuru kazini ni karibu sihitaji nauli.

Madeni mabaya wapendwa, ukiweza usikope kabisa , nimeharibu undugu, urafiki ,familia, naishi kwa Neema ya Mungu na kuomba nisipate stress.

Mbinu zote za kibinadamu nimetumia ili nilipe madeni nimeshindwa, sasa hivi natumaini Mungu tu. Wapendwa msikope madeni ni utumw, ni kifungo kibaya.
Kwanza mshukurie mungu. Kwa kua hupo pamoja nawe. Na amekuwezesha njia za kupita. Usife moyo. Angalia wapi ulioteleza kisha nyanyuka na uwanze upya.
 
Kukopa ni laana mkuu, hii kitu naiogopa iliniharibia uchumi wangu...siitaki kabisa
Kopesha kisha usirejeshewe uskilizie maumivu yake. Watu wengine wanakopa sehemu kibao kisha mambo yakiwaendea isivyo inakuwa taabu hata simu hawapokei kero kubwa
Wewe sio mwelewa na mbinafsi.
Rejea habari ya mleta uzi...alikuwa na malengo thabiti lkn yameenda kinyume, mvua imesomba mazao unategemea sksyarudishe?
 
Kukopa ni laana mkuu, hii kitu naiogopa iliniharibia uchumi wangu...siitaki kabisa
binafsi naichukia sana mikopo, niliwahi chukua mambo yakaenda kombo nikakopa kwingine kuhamisha deni nikidhani karibuni mambo yatakua sawia bt mambo ndo yakaenda kombo zaidi, after kumaliza deni niliapa juu ya mikopo mpaka naingia kaburini.
 
Mapito tu hayo,.Kuna jamaa kwaajili ya maden mshahara akawa anapokea 40000,.ila miaka ilienda akatoboa..maisha Sasa hv anapokea 950000
 
Auntie acha tu mwenyewe namdai laki 6 rafiki yangu imenibidi tu nimwache akijisikia kunipa atanipa ila nimeshamwambia sitamdai hapo kati alikuwa anapitia kipindi kigumu ila sasa hivi naona amerudi kwenye hali yake
Auntie kuna wakati unaweza kukomaa tu kumdai mtu kumbe ndio unamzidishia maumivu maana anayopitia ni mazito haswa. Ukiweza kama ni mtu wako wa karibu na unajua sio msanii basi unamuacha tu.
 
Back
Top Bottom