Mikopo Elimu ya Juu: Waziri wa Elimu, Prof. Joyce Ndalichako asema walio na fedha wasisubiri kukatwa 15%

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Waziri wa Elimu, Prof. Joyce Ndalichako amewataka wanufaika wa Mikopo ya Elimu ya Juu kuona umuhimu wa kulipa, na wenye fedha wasisubiri kukatwa 15% ili Wanafunzi wengine waweze kunufaika na kupata Ajira.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Esther Matiko aliyehoji ni lini Serikali italeta mabadiliko ya Sheria ili kupunguza makato kufikia angalau 8%, Waziri Ndalichako amesema Mnufaika anakatwa 15% na kubakia na 85%

Ameeleza, "Tukumbuke kwamba Mkopo wa Bodi ndio uliotangulia kabla ya Mikopo mingine, na kwa Kanuni Utumishi, Mtumishi anatakiwa abaki theluthi moja ya mshahara"

Aidha, ameeleza kuwa, lengo la kuanzisha mfuko wa Mikopo ilikuwa ni watu wafanye marejesho, Mikopo ijiendeshe yenyewe na kutosheleza kuwapatia Wanafunzi wengine.
 
Mnufaika anakatwa 15% na kubakia na 85% sina uhakika kama Mh Waziri anafahamu alichojibu. Kwa kifupi, mfanyakazi mwenye mshahara wa TZS 1,000,000 mwenye mkopo na amejiunga na bima ya afya, makato yake ni kama ifuatavyo:-
Namexxxxxxxxx
Name of Bankxxxxxx
Account numberxxxxxx
TZS
Basic salay1,000,000.00
Other earnings
-
Round off-
-
Gross salary (a)1,000,000.00
Less: Pension100,000.00
Taxable salary900,000.00
DEDUCTIONS
PAYE(105,500.00)
HESLB(150,000.00)
Pension(100,000.00)
Health insurance(30,000.00)
Total deductions (b)(385,500.00)
Net salary payable in TZS (a) +(b)
614,500.00​
61%
 
Sidhani hata kama alilielewa swali, au pengine kwa makusudi kabisa kaa. UA kujifanya hajalielewa.
 
Wala sihangaiki, nasubilia Mgombea urais ajaye maana hiyo ndiyo sera yake kubwa inatosha ile ile mliyochukua miezi Mi4 saizi hamnipati tena, nyie mlisoma bure na Mikate ya bure, saizi mnataka kutuzima pumzi kabisa.
 
Waziri wa Elimu, Prof. Joyce Ndalichako amewataka wanufaika wa Mikopo ya Elimu ya Juu kuona umuhimu wa kulipa, na wenye fedha wasisubiri kukatwa 15% ili Wanafunzi wengine waweze kunufaika na kupata Ajira.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Esther Matiko aliyehoji ni lini Serikali italeta mabadiliko ya Sheria ili kupunguza makato kufikia angalau 8%, Waziri Ndalichako amesema Mnufaika anakatwa 15% na kubakia na 85%

Ameeleza, "Tukumbuke kwamba Mkopo wa Bodi ndio uliotangulia kabla ya Mikopo mingine, na kwa Kanuni Utumishi, Mtumishi anatakiwa abaki theluthi moja ya mshahara"

Aidha, ameeleza kuwa, lengo la kuanzisha mfuko wa Mikopo ilikuwa ni watu wafanye marejesho, Mikopo ijiendeshe yenyewe na kutosheleza kuwapatia Wanafunzi wengine.
Kama profesa amejibu hivi acha nibaki na degree yangu tu
 
NIKIONA MACHUNGU YA WALE WANAOKATWA MKOPO NA KUNA KITU WANAITA KITUNZIA MKOPO NACHOKA SANA
 
Kwa Umri wake Prof Ndalichako atakuwa alisomeshwa bure na Serikali kabla haijaanzishwa hiyo Loans board, hivyo hajali machungu ya wanaokatwa hizo 15%

Wakati mwingine Watanzania watajifunza kuchagua vizuri watakao wasaidia sio hawa wanaokata 15% loans board, wala wasiotoa increment za mishahara wala hawa wasiojali wimbi kubwa la vijana wasio na ajira
 
Back
Top Bottom